Ijumaa, 24 Juni 2016

MSWADA WA SHERIA YA MANUNUZI YA UMMA WA MWAKA 2106

IMG_20160624_151157_421 
Katika kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia matakwa ya Kanuni ya 117(9) ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Januari 2016; Kamati ya Bunge ya Bajeti imepanga kufanya mkutano wa kusikiliza maoni ya wadau wote wa masuala ya Ugavi (Public Hearing) kuhusu Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma wa Mwaka 2016 (Public Procurement Act 2016) kabla Muswada huo haujapitishwa na Bunge kuwa Sheria.
Mkutano huo wa kusikiliza maoni ya wadau (Public Hearing) unatarajiwa kufanyika siku ya Jumatatu Juni 27, 2016 Bungeni Dodoma kuanzia saaTanoAsubuhi katika Ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni – Dodoma.
Kwa kuzingatia umuhimu wa Muswada huo, Kamati inawaalika wadau wote kufika na kuwasilisha maoni yao mbele ya Kamati kabla kupelekwa katika hatua nyingine. Maoni ya wadau yanaweza pia kuwasilishwa kwa njia ya Posta au Barua pepe kwa anuani ifuatayo:
Katibuwa Bunge,
Ofisi ya Bunge,
S.L.P. 941,
DODOMA
Baruapepe: cna@bunge.go.tz

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni