MSWADA WA SHERIA YA MANUNUZI YA UMMA WA MWAKA 2106
Katika
 kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia matakwa ya Kanuni ya 117(9) ya 
Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Januari 2016; Kamati ya Bunge ya 
Bajeti imepanga kufanya mkutano wa kusikiliza maoni ya wadau wote wa 
masuala ya Ugavi (Public Hearing) kuhusu Muswada wa Sheria ya Manunuzi 
ya Umma wa Mwaka 2016 (Public Procurement Act 2016) kabla Muswada huo haujapitishwa na Bunge kuwa Sheria.
Mkutano
 huo wa kusikiliza maoni ya wadau (Public Hearing) unatarajiwa kufanyika
 siku ya Jumatatu Juni 27, 2016 Bungeni Dodoma kuanzia saaTanoAsubuhi 
katika Ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni – Dodoma.
Kwa 
kuzingatia umuhimu wa Muswada huo, Kamati inawaalika wadau wote kufika 
na kuwasilisha maoni yao mbele ya Kamati kabla kupelekwa katika hatua 
nyingine. Maoni ya wadau yanaweza pia kuwasilishwa kwa njia ya Posta au 
Barua pepe kwa anuani ifuatayo:
Katibuwa Bunge,
Ofisi ya Bunge,
S.L.P. 941,
DODOMA
Baruapepe: cna@bunge.go.tz
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni