DKT. NDUGULILE ATAKA MABUNGE KUSHIRIKISHWA KWENYE MPANGO WA “AFYA MOJA” (ONE HEALTH)
By Newsroom n June 29, 2016
Mbunge wa Jimbo la 
Kigamboni (CCM) Dkt Faustine Ndugulile(Mb) ameyataka Mataifa 
kushirikisha Mabunge katika kufanikisha mpango wa Usalama wa Afya 
Duniani (Global Health Security Agenda).
Akizungumza kwenye mkutano wa 
masuala ya Usalama wa Afya ulioandaliwa na Shirika la Afya Duniani (WHO)
 na kufanyika Jijini Bali, Indonesia,, Dkt Ndugulile alisema, “Mabunge 
yanaweza kutoa mchango mkubwa sana kwenye utekelezaji wa Mpango wa 
Usalama wa Afya Duniani kwa kusimamia Serikali na kuhakikisha hatua zote
 muhimu zinatekelezwa; kutunga Sheria zitakazosimamia utekelezaji wa 
mpango huu pamoja na kuhakikisha mpango huu unapata fedha za kutosha 
kutoka kwenye Bajeti ya Serikali”.
Dkt Ndugulile alisema kuwa 
muingiliano wa shughuli za kilimo, mifugo na shughuli nyingine za 
kibinadamu zimesababisha baadhi ya magonjwa ya wanyama kuleta athari kwa
 binadamu na pia usugu wa madawa ya aina ya antibiotiki. Hivyo, kuna 
haja ya wadau wa sekta hizi kuwa na ushirikiano wa karibu chini ya 
mpango wa “Afya Moja” (One Health). 
Mbunge wa Jimbo la Kigamboni 
(CCM) Dkt Faustine Ndugulile (Mb) (kulia), akizungumza kwenye mkutano wa
 masuala ya Usalama wa Afya ulioandaliwa na Shirika la Afya Duniani 
(WHO) na kufanyika Jijini Bali, Indonesia.
Alisema kuwaIli mpango wa “Afya
 Moja” ufanikiwe in lazima maboresho yafanyike kwenye uratibu wa sekta 
mbalimbali ndani ya nchi na pia kuandaa mpango wa pamoja wa udhibiti na 
kushughulikia majanga.
Dkt Ndugulile aliyasema hayo 
kwenye mkutano wa Mpango wa Usalama wa Afya Duniani unaofanyika mjini 
Bali, Indonesia. Mkutano huu ulioanza tarehe 27 Juni unatarajia kuisha 
tarehe 30 Juni.
Dkt Ndugulile mbali ya kuwa 
Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya 
Mabunge Duniani (Inter Parliamentary Union) kuhusiana na masuala ya 
UKIMWI, Afya ya Wanawake, Vijana na Watoto.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni