SERENGETI BOYS YAPAA, MCHAWI MWEUSI ATAMBA
Serengeti
 Boys inaondoka na matumaini makubwa ya kuiondoa Shelisheli katika mbio 
hizo baada ya kuvuna ushindi mnono wa mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza 
uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Jumapili ya Juni 26, 2016. 
Ili ifuzu, Serengeti Boys inahitaji kusimama imara katika matokeo hayo 
ama kwa kupata sare ya aina yoyote, kushinda au ikitokea kupoteza, basi 
isifungwe zaidi ya mabao 2-0.
Lakini
 Kocha Mkuu wa vijana hao, Bakari Shime maarufu kama Mchawi Mweusi 
kutoka Tanga, amesema, “Nawaheshimu Shelisheli, lakini vijana wangu 
hawawezi kuwapa nafasi hata kidogo wapinzani wetu. Hapa tulishinda, na 
kwako tunakokwenda tunakwenda kushinda. Vijana wangu wa Serengeti Boys 
wako vizuri. Nawapenda na wao wanatupenda makocha wao na viongozi wote 
wa TFF.”
Katika
 mchezo wa Dar es Salaam waliozifumania nyavu walikuwa Nickson Kibabage,
 Ibrahim Abdallah na Ally Hussein ambaye alifunga ambao kila mmoja 
amepania kufunga kama kocha akiwapa nafasi ya kuanza katika kikosi cha 
kwanza kwa sababu Mchawi Mweusi amefunga safari hiyo akiwa na kikosi cha
 nyota 20 wa timu hiyo inayolelewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu 
Tanzania (TFF) chini ya Rais Jamal Malinzi.
Nyota
 waliosafiri ni pamoja na makipa, Ramadhani Awm Kabwili na Samwel Edward
 Brazio wakati mabeki wako Kibwana Ally Shomari, Nickson Clement 
Kibabage, Israel Patrick Mwenda, Dickson Nickson Job, Ally Hussein 
Msengi, Issa Abdi Makamba.
Viungo
 ni Kelvin Nashon Naftal, Ally Hamisi Ng’anzi, Asadi Ali Juma Ali, 
Syprian Benedictor Mtesigwa, Ibrahim Abdallah Ali, Yassin Muhidini 
Mohamed, Shaban Zuberi Ada huku washambuliaji wakiwa ni Rashid Mohammed 
Chambo, Mohammed Abdallah Rashid, Yohana Oscar Mkomola, Muhsin Malima 
Makame na Enrick Vitalis Nkosi.
Serengeti
 Boys ambayo haina mdhamini badala yake ikihudumiwa na TFF yenyewe 
ilikuwa kambini tangu Juni 14, 2016 kujiandaa na mechi hizo za kufuzu 
fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Shelisheli na Afrika 
Kusini ambayo itapambana nayo baadaye mwezi ujao.
Katika
 kuajindaa na mchezo huo, Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako 
walishiriki mashindano ya vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na FIFA 
(AIFF International Youth Tournament 2016) kabla ya kurudi na rekodi ya 
kupigiwa mfano si tu katika Tanzania na kwa nchi za Afrika Mashariki. 
Ilishika nafasi ya tutu nyuma ya Korea Kusini na Marekani.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni