TRA yakutanisha wadau wa kodi kujadili uanzishwaji wa chombo cha kuratibu na kusimamia wanataaluma wa kodi
TRA yakutanisha wadau wa kodi kujadili uanzishwaji wa chombo cha kuratibu na kusimamia wanataaluma wa kodi
Katika kuendelea kuimarisha 
ushirikiano uliopo kati ya walipa kodi na wakusanyaji wa kodi, Mamlaka 
ya Mapato nchini (TRA) imefanya kongamano la pamoja na wadau wa kodi 
nchini likiwa na lengo la kujadili kwa pamoja kuhusu uanzishwaji wa 
chombo cha kuratibu na kusimamia wanataaluma wa kodi.
Akizungumza wakati wa ufunguzi 
wa kongamano hilo, Kamishna wa Sera na Bajeti kutoka Wizara ya Fedha na 
Mipango, Shogholo Msangi alisema wamekutanisha wadau hao wa kodi ili 
waweze kutoa maoni na kukubaliana kwa pamoja jinsi gani chombo hicho 
kitaweza kufanya kazi.
“Kutakuwa na chombo ambacho 
kitakuwa kinaratibu na kusimamia wanataaluma wa kodi na lengo ni kupitia
 kongamano hilo wadau wa kodi wataweza kukubaliana kwa pamoja kuona ni 
jinsi gani chombo hicho kitafanya kazi,
Kamishna wa Sera na Bajeti 
kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Shogholo Msangi akitoa neno la 
ufunguzi katika kongamano lililoandaliwa na TRA na kukutanisha wadau 
mbalimbali wa kodi. (Picha zote na Rabi Hume – MO Blog)
“Unaweza kukuta kuwa mlipa kodi
 kwa sasa ndiyo anaumia au TRA ndiyo inaumia lakini chombo hicho 
kitaweza kusimamia na kuweka kila jambo sehemu sahihi kama linavyotakiwa
 kuwapo,” alisema Msangi.
Nae Mkuu wa Chuo cha Taifa cha 
Kodi (ITA), Prof. Isaya Jairo alisema kuwa chombo hicho kama 
kikianzishwa kitaweza kufanya kazi zake kwa uhuru bila kuingiliwa na TRA
 ili kuhakikisha kuwa kinatoa na haki kati ya mlipa kodi na wakusanyaji 
wa kodi (TRA) bila kuumiza upande wowote kwani jambo hilo linawahusu 
wote.
Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Kodi
 (ITA), Prof. Isaya Jairo akitoa neno la ukaribisho katika ufunguzi wa 
kongamano hilo lililofanyika Bagamoyo, Pwani.
Alisema kupitia kongamano hilo 
wamekutanisha wataalam wa kodi, wahasibu, walipa kodi, wanasheria, 
washauri wa kodi na walimu wa kodi kutoka vyuoni ili kuweza kupata maoni
 ya pamoja na kupata maoni ya makubaliano ya pande zote ambayo 
yatatumika katika kuendesha chombo hicho.
Na Rabi Hume – MO Blog)
Baadhi ya wadau waliohudhuria kongamano hilo la siku moja lililofanyika Bagamoyo, Pwani.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni