SAGCOT WASAINI MKATABA NA MAKAMPUNI YALIYOOMBA UFADHILI KWA AJILI YA UKUZAJI KILIMO NA VIWANDA
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Joel Malongo akizungumza na vongozi wa Mfuko Kichocheo wa SAGCOT, wawakilishi
wa vyama vya wakulima na wawakilishi wa wabia wa Maendeleo jijini Dar
es Salaam leo wakati wa kusaini mikataba ya makubaliano ya ufadhili wa
Fedha katika mfuko wa Kichocheo wa SAGCOT pamoja na kampuni zilizoibuka
kidedea kwenye kinyang’anyiro cha kuomba ufadhili kutoka kwenye mfuko.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Joel Malongo (Mwenye tai nyekundu waliosimama) akishuhudia wawakilishi wa vyama vya wakulima wakisaini
mikataba ya makubaliano ya ufadhili wa Fedha katika mfuko wa Kichocheo
wa SAGCOT pamoja na kampuni zilizoibuka kidedea kwenye kinyang’anyiro
cha kuomba ufadhili kutoka kwenye mfuko huo jijini Dar es Salaam leo.
wanaosaini hati hizo kutoka kulia ni Mkulima wa miwa Dk George Mlingwa
Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Germao Cane Estate, Mwenyekiti wa
Bodi ya Mfuko Kichocheo wa SAGCOT, Ami Mpungwe, Roy Omulo kutoka kiwanda
cha Maziwa cha Asas Dairies Iringa na Lutengano Peter Mwenyekiti wa
MUWAMARU Tukuyu mkoani Mbeya.
Baadhi ya viongozi hao wakiwa katika mkutano huo leo
Baadhi ya wafadhili wakiwa katika mkutano huo
Washiriki wa mkutano huo kutoka makampuni mbalimbali na serikali
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Joel Malongo akizungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko Kichocheo wa SAGCOT, Ami Mpungwe wakati wa mkutano huo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni