Mwenyekiti wa Tume ya kurekebisha sheria Zanzibar Jaji Mshibe Ali Bakar asema kesi nyingi zinazofunguliwa Zanzibar hazina mashiko
Na Masanja Mabula –Pemba
MWENYEKITI wa Tume ya 
kurekebisha sheria Zanzibar Jaji Mshibe Ali Bakar amesema kuwa kesi 
nyingi zinazofunguliwa katika mahakama za Zanzibar hazina mashiko na 
zilipaswa kusuluhishwa na jamii kabla ya hazijafikishwa mahakamani .
Amesema kwamba hali hiyo 
inasababisha kuwepo na mrundikano wa kesi  katika mahakama , kutokana na
 jamii kuina mahakama kama  sehemu ya kuwasilisha malalamiko hata yale 
yasiyo na mashiko .
Jaji Mshibe ameyabainisha hayo 
wakati akifungua kikao cha siku moja cha kukusanya maoni juu ya sheria 
ya mirathi kwa viongozi wa dini , mahakimu , walemavu pamoja na viongozi
 wa kisiasa Kisiwani Pemba  katika ukumbi wa Benjemini Mkapa Wete .
Amefahamsha pamoja na kuwepo 
kwa vyombo vya ulinziz na viongozi wa serikali za mitaa (masheha) lakini
 wameshindwa kutimiza wajibu wao wa kuzuia matendo maovu yasitokea ndani
 ya jamii kabla ya kuwafikisha mahakamani .
“Kwa kipindi kimekuwako na 
ongezeko kubwa na kesi katika mahakama za Zanzibar na ikizifuatilia 
utabaini kwamba hazina mashiko , ambazo zilipaswa kusuluhishwa kabla 
hazijafikishwa mahakamani ”alieleza.
Aidha Mshibe alizidi 
kufahamisha kwamba kitendo cha jamii kusuluhisha kesi badala ya 
kufikishwa mahakamani pia kutaokoa fedha nyingi ambazo zilikuwa zitumike
 kwa ajili ya kuandaa shauri hilo  .
Alieleza kwamba iwapo kila 
mmoja atawajibika kuzuia matukio yasitokee ndani ya jamii , kutaleta 
ufanisi wa utendaji wa kazi  serikalini kwani watumishi wake hususani wa
 mahakama watapunguziwa mzigo wa kupokea mashauri mengi kupita uwezo wa 
wa kufanya kazi .
“Kama kila mmoja atawajibika 
kuzuia kesi kufikishwa kutaongeza pia ufanisi wa kazi kwa watendaji wa 
mahakama zetu , ambao kwa sasa wanapokea kesi nyingi kupita uwezo wa 
mahakama zenyewe ”alifahamisha.
Hata hivyo akizungumzia suala 
la kuongezwa watendaji wa Idara ya Mahakama , Jaji Mshibe alisema suwala
 hilo tayari limepatiwa ufumbuzi , lakini bado changamoto ni jamii 
yenyewe kutokuwa tayari kufanya suluhu kwa kesi za kawaida .
Akichangia kwenye kikao hicho ,
 Padri wa kanisa la Anglikana Pemba Massoud Emmanuel alisema kwamba , 
bado jamii haijawa tayari kupokea ushauri na maelekezo kutoka kwa 
wananchi wa kawaida hata kama utakuwa na maana au faida kwao .
Amesema kwamba viongozi wa dini
 wanapowajibika katika kuelimisha jamii , hushushiwa zigo wakidaiwa 
kwamba wamekuwa wanasiasa , jambao ambalo linawawia vigumu kuufikisha 
ujumbe kwa jamii inayaowzunguka .
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni