RC MAKONDA ATEMBELEA BANDA LA UN KATIKA VIWANJA VYA SABASABA
Katika kuelekea kilele 
cha Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba, Mkuu wa Mkoa wa 
Dar es Salaam, Paul Makonda ametembelea banda la Umoja wa Mataifa (UN) 
lililopo katika ukumbi wa Karume kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere 
barabara ya Kilwa jijini Dar.
Makonda alifika katika banda 
hilo na kupata nafasi ya kupata maelezo kutoka kwa wafanyakazi wa UN 
kuhusu kazi ambazo zinafanywa na shirika hilo hapa nchini.
Mtaalamu wa Mawasiliano wa 
Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu (kulia) akitoa maelezo ya 
shughuli mbalimbali zinazofanywa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini
 kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (katikati) alipotembea 
banda la shirika hilo lililopo katika ukumbi wa Karume kwenye Maonyesho 
ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu 
Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, 
Paul Makonda akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja
 wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu kuhusu Malengo 17 ya Maendeleo 
Endelevu (SDGs) ambayo yanatakiwa kumfikia kila mwananchi alipotembelea 
banda la Umoja wa Mataifa lillilopo katika ukumbi wa Karume kwenye 
Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja 
vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar.
Mtaalamu wa Mawasiliano wa 
Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu akimwonyesha Mkuu wa Mkoa wa 
Dar es Salaam, Paul Makonda Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) 
yaliyobandikwa katika banda la UN na jinsi walivyojipanga katika 
kuelimisha wananchi kuhusiana na malengo hayo kwenye Maonyesho ya 40 ya 
Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere 
barabara ya Kilwa jijini Dar.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, 
Paul Makonda akisaini kitabu cha wageni katika banda la Shirika la Umoja
 wa Mataifa lililopo katika ukumbi wa Karume kwenye Maonyesho ya 40 ya 
Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere 
barabara ya Kilwa jijini Dar. Kulia ni Maafisa Habari wa Umoja wa 
Mataifa, Hoyce Temu na Usia Nkhoma Ledama. RC Makonda amekuwa mgeni 
kwanza mashuhuri kutembelea banda hilo na kutoa baraka zake kwenye 
maonyesho hayo.
Mtaalamu wa Mawasiliano wa 
Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu katika picha ya pamoja huku 
wakiwa na bango maalum linalowakilisha rangi za malengo 17 ya SDGs na 
mmoja wa vijana aliyetembelea banda la Umoja wa Mataifa lililopo kwenye 
ukumbi wa Karume kwenye maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa 
yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa 
jijini Dar.
Afisa Habari wa kituo cha 
Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama akizungumza na 
waandishi wa habari kwa lengo la kuhamasisha wananchi kutembelea banda 
hilo na kujifunza Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu SDGs na kujua 
shughuli mbalimbali zinazofanywa na Shirika hilo hapa nchini.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni