Watanzania waaswa kuzingatia umri katika kuangalia filamu na maigizo.
Katibu
 Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fisso akizungumza na 
waandishi wa habari ( hawapo pichani) kuhusu mambo mbalimbali yahusuyo 
tasnia ya filamu nchini katika kuazimisha wiki ya Utumishi wa Umma. 
————————————————————
Na Raymond Mushumbusi WHUSM
Watanzania wameaswa kuzingatia umri katika kungalia filamu katika majumba ya sinema na sehemu mbalimbali.
Wito huo umetolewa leo Jijini Dar 
es Salaam na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce 
Fisso wakati akifafanua masuala mbalimbali kuhusu tasnia ya filamu 
nchini  kwa  waandishi wa habari.
Bibi Joyce Fisso amesema kuwa Bodi
 yake inafanya kazi ya kuzipa kiwango kazi za filamu na maigizo ikiwemo 
umri sahihi wa kuangalia filamu  na hili linapaswa kuzingatiwa na 
waoneshaji na waangaliaji wa Filamu.
“ Natoa wito kwa watanzania hasa 
wazazi kuzingatia umri katika kuangalia filamu, ukiona imeandikwa umri 
wa miaka 18 ujue ni maalum kwa ajili ya umri huo na mtoto chini ya hapo 
hatakiwa kuangalia kwasababu maudhui ya filamu au maigizo hayo 
hayamuhusu alisisitiza Bibi. Joyce.
Bibi Joyce Fisso ameongeza kuwa 
jukumu la kujenga maadili kwa watanzania hasa watoto lipo mikononi mwa 
wazazi wao na kuwaasa wazazi kuzingatia umri katika kuangali filamu na 
maigizo mbalimbali ili kupunguza wimbi la mmomonyoko wa maadili nchini.
Aidha Bibi Joyce Fisso ameshauri 
waandaaji wa filamu na maigizo nchini kuandaa filamu na maagizo yenye 
maudhui ya watoto  ya kuwajenga katika Mila, Desturi na Tamaduni za 
kitanzania kwa kuwa ndio kizazi cha baadae na kinatakiwa kulelewa katika
 maadili mema.
Bodi ya Filamu inapokea filamu na 
maigizo mbalimbali kwa ajili ya kupata kibali cha kusambazwa na zaidi ya
 asilimia 70 ya filamu hizo maudhui yake ni mapenzi  hivyo basi jamii 
inatahadharishwa kuzingatia umri uliowekwa katika filamu na maigizo hayo
 ili kuepukana na mmomonyoko wa maadili kwa watoto uanaozidi kuongezeka 
siku hadi siku kwa kuangalia filamu na maigizo yenye maudhui 
yasiyowahusu.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni