MABONDIA GALILE NA MAPAMBANO KUMALIZA UBISHI JULAI 24 MUSOMA BAR
Mdau wa masumbwi nchini Jumanne
Mbwembwe akiwainua mikono juu mabondia Imani Mapambano kushoto na
Seleman Galile kwa ajili ya kutambulisha mpambano wao wa julai 24
katika ukumbi wa Musoma Bar Tandika Picha na SUPER D BOXING NEWS
| Mabondia Iani Mapambano kushoto na Selemani Galile wakiwa katika pozi wakati wa utambulisho wa mpambano wao wa julai 24 katika ukumbi wa Musoma Bar tasndika Picha na SUPER D BOXING NEWS |
Mabondia
Imani Mapambano kushoto akitunishiana misuli na Selemani Galile baada
ya kusaini mkataba wa kuzipiga julai 24 katika ukumbi wa Musoma Bar
tandika Picha na SUPER D BOXING NEWS.
………………………………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu
MABONDIA Imani Mapambano na
Selemani Galile wamesaini mkataba wa kuzipiga Julai 24 katika ukumbi wa
Musoma Bar uliopo Tandika Dar es salaam
Akizungumza baada ya kusainishwa kwa mabondia hao mratibu wa mpambano huo Rajabu Mhamila ‘Super D’
amesema kuasini mkataba kwa
mabondia hao baada ya kutambiana mara kwa mara utaonyesha nani ni mbabe
kati yao watakapopanda ulingoni Julai 24 mwaka huu, nimeamua wapambane
julai 24 katika ukumbi wa Musoma Bar ili kumaliza ubisha wao.
Mpambano huo utakuwa wa ubingwa wa Taifa utakaosimamiwa na TPBO chini ya rais wake Yassin Abdallah ‘Ustaadhi’
Aliongeza kwa kusema kuwa mipambano mingine ya utangulizi itatangazwa kadri watakavyo ingia mikataba na mabondia mbali mbali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni