 Miss
 Dar Indian Ocean aliyemaliza muda wake, Camilla John (katikati) 
akimvisha skafu Mshindi wa Mashindano ya Miss Tanzania Indian Ocean 2016
 Jackline Kimambo (kushoto) mara baada ya kuibuka mshindi katika 
mashindano hayo yaliyofanyika 30 Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko
 Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Miss
 Dar Indian Ocean aliyemaliza muda wake, Camilla John (katikati) 
akimvisha skafu Mshindi wa Mashindano ya Miss Tanzania Indian Ocean 2016
 Jackline Kimambo (kushoto) mara baada ya kuibuka mshindi katika 
mashindano hayo yaliyofanyika 30 Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko
 Mikocheni jijini Dar es Salaam. 
  Miss
 Tanzania Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo (aliyekaa katikati) akiwa 
katika picha ya pamoja na warembo wenzie ambaye ni Mshindi wa pili na wa
 tatu mara baada ya kumalizika kwa mashindano hayo yaliyofanyika 30 
Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Miss
 Tanzania Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo (aliyekaa katikati) akiwa 
katika picha ya pamoja na warembo wenzie ambaye ni Mshindi wa pili na wa
 tatu mara baada ya kumalizika kwa mashindano hayo yaliyofanyika 30 
Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni jijini Dar es Salaam. 
  Kaimu
 Mkuregenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa Wizara ya Habari, Utamaduni, 
Sanaa na Michezo, Bw. Francis Songoro (kulia) akimpongeza Miss Tanzania 
Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo kwa kuibuka mshindi wa mashindano 
hayo baada ya kumalizika kwa mashindano hayo yaliyofanyika 30 Julai, 
2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Kaimu
 Mkuregenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa Wizara ya Habari, Utamaduni, 
Sanaa na Michezo, Bw. Francis Songoro (kulia) akimpongeza Miss Tanzania 
Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo kwa kuibuka mshindi wa mashindano 
hayo baada ya kumalizika kwa mashindano hayo yaliyofanyika 30 Julai, 
2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni jijini Dar es Salaam. 
  Miss
 Tanzania Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo akiwa katika picha ya 
pamoja na baadhi ya washiriki baada ya kumalizika kwa mashindano hayo 
yaliyofanyika 30 Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni 
jijini Dar es Salaam.
Miss
 Tanzania Indian Ocean 2016 Jackline Kimambo akiwa katika picha ya 
pamoja na baadhi ya washiriki baada ya kumalizika kwa mashindano hayo 
yaliyofanyika 30 Julai, 2016 katika Ukumbi wa MRC Ulioko Mikocheni 
jijini Dar es Salaam. 
……………………………………………………………………………………………..
Na. Benedict Liwenga-WHUSM.
Wadau
 wanaojishughulisha na masuala ya Sanaa nchini wamehamishwa kujitokeza 
kwa wingi katika kusaidia maendeleo ya Sanaa kwa kudhamini na kufadhili 
mashindano ya urembo bila kubagua.
Kauli
 hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Idara ya 
Maendeleo ya Sanaa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. 
Francis Songoro wakati alipokuwa akiwasilisha hotuba ya Naibu Waziri wa 
Wizara hiyo, Mhe. Anastazia Wambura ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi 
katika Mashindano ya Miss Tanzania Indian Ocean 2016 yaliyofanyika 
katika Ukumbi wa MRC uliopo Mikocheni jijini hapa.
Akiwasilisha
 hotuba hiyo, Songoro amesema kwamba kazi inayofanywa na wadau wa sanaa 
ni hatua ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Utamaduni ambayo inasisitiza
 jamii na wakuzaji sanaa kuendeleza ubunifu katika kazi za kiutamaduni.
Ameeleza
 kuwa, Serikali kupitia Wizara yake inathamini na kuunga mkono juhudi 
zinazofanywa na wadau hao hasa katika kukuza na kuviendeleza vipaji vya 
vijana nchini, hivyo amewapongeza wadau hao kwa moyo wao wa kujitoa na 
kuwataka kuendeleza kwa vitendo Sera ya Taifa ya Utamaduni ya mwaka 1997
 katika Sura ya 9 kifungu cha 9:5:8 ambacho kinasisitiza na kuhimiza 
watu binafsi pamoja na Mashirika kuwekeza rasilimali katika sekta ya 
utamaduni.
‘’Maonyesho
 haya ni ishara tosha kuwa sanaa ni kazi, ajira, biashara na burudani, 
hivyo kipekee nawapongeza sana’’, alisema Songoro.
Aliongeza
 kuwa, Warembo ambao wameshiriki katika mashindano hayo wanautangaza 
utalii wa ndani na nje ya nchi na kwa kufanya hivyo wanaiwakilisha vyema
 Tanzania Duniani katika mashindano ya Miss World na pia kukuza uchumi 
wa nchi.
Aidha,
 amewataka warembo ambao hawakubahatika kuibuka washindi katika 
mashindano hayo kutokata tamaa, bali waitumie fursa hiyo hususani ya 
elimu waliyoipata wakiwa kambini kwa kuisadia jamii inayowazunguka na 
kuwa wanawake wa mfano wa kuigwa katika kujitambua na kujiamini.
‘’Mtambue
 kwamba, siyo wote mtakaoibuka washindi na kuendelea mbele katika 
mashindano haya, niwaombe wale ambao hamtashinda msivunjike moyo, bali 
mkaitumie elimu mliyoipata na yale ambayo mmejifunza mkiwa kambini kwa 
kuisaidia jamii inayowazunguka na muwe wanawake wa mfano wa kuigwa’’, 
alisema Songoro.
Katika
 mashindano hayo, Mshindi wa Kwanza aliyeibuka na kunyakua taji hilo ni 
Jackline Kimambo ambaye alipatikana kati ya tano bora  na kuvikwa taji 
la Miss Tanzania Indian Ocean 2016 na Mshindi wa pili ni Regina Ndimbo 
huku wengine waliobaki kwenye tano bora wamepata fursa ya kuingia katika
 mashindano ya Miss Kinondoni.
Shindano
 hilo lilihusisha jumla ya washiriki wapatao 20 ambapo mmoja kati yao 
ndiyo aliyeibuka mshindi na lilidhaminiwa na wadau mbalimbali wakiwemo 
Mikocheni Resort Centre, Mlimani TV, Channel Ten, Darling, Helmic, 
Tanzania Breast Cancer Foundation, Magic FM, Jozi Lounge, Kiss Printers 
pamoja na NTS.