TAMKO KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI
By Newsroom on June 13, 2016
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
TAMKO
KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI LILILOTOLEWA NA MHE.
UMMY MWALIMU (MB); WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA
WATOTO, TAREHE 13 JUNI, 2016
Serikali
kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto
inaendelea na utaratibu wa kutoa taarifa ya mwenendo wa mlipuko wa
ugonjwa Kipindupindu nchini kila wiki kama tulivyoahidi, ili kutoa
tahadhari kwa wananchi na maelekezo ya hatua za kuchukua ili kukabiliana
na mlipuko huu. Hadi kufikia tarehe 12 Juni 2016, jumla ya wagonjwa
21,786 nchini wametolewa taarifa,na kati yao Ndugu zetu 342 wamepoteza
maisha tangu ugonjwa huu uliporipotiwa Agosti 2015.
Takwimu
zinaonyesha kuwa, katika wiki hii inayoishia tarehe 12 Juni 2016,
Idadi ya wagonjwa walioripotiwa nchi nzima ni 78 na kati yao mmoja
alipoteza maisha. Wiki iliyotangulia kulikuwa na wagomjwa 62
waliotolewa taarifa na kati yao watatu walipoteza maisha. Hii ikionyesha
kuna ongezeko la wagonjwa walioripotiwa wiki hii ikilinganishwa na wiki
iliyotangulia ingawa kuna kupungua kwa Idadi ya waliopoteza maisha.
Mikoa
iliyoripoti ugonjwa wa kipindupindu wiki hii ni mitano(5), Morogoro (
wagonjwa 43 na kifo 1), Mwanza (21), Mara (7), Lindi (4) na Manyara
(3). Aidha wiki hii wilaya zilizoripoti ugonjwa wa Kipindupindu ni
Morogoro vijijini (wagonjwa 27 na kifo 1), Morogoro mjini (8), Mvomero
(8), Ilemela (12), Nyamagana (9), Tarime vijijini (5), Tarime mjini (2),
Kilwa (4) na Simanjiro (3). Mpaka sasa bado mikoa ya Njombe na
Ruvuma haijaripoti mgonjwa yeyote wa Kipndupindu tangu mlipuko huu
uanze mnamo mwezi Agosti mwaka 2015
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni