Mtafiti wa Hesabu aomba Milioni 12 kufanikisha safari ya Marekani kuwasilisha Utafiti wake.
Anitha Jonas – MAELEZO
Dar es Salaam.
Mtanzania aliyevumbua Fomula ya
Hesabu yenye uwezo wa kutumika katika Hesabu za Viwandani Mhandisi
Mazoleka Maziku awaomba watanzania, Taasisi za Serikali na zisizo za
Kiserikali,Kimataifa na za watu binafsi kumchangia kiasi cha Shilingi
Milioni 12 kwa ajili ya kuwasilisha utafiti wake katika Mkutano wa Mwaka
wa wataalamu wa Hesabu za Viwandani nchini Marekani.
Bw. Maziku ameomba msaada huo
alipokuwa akizungumza na waaandishi wa Habari kuhusu utafiti huo
aliyoufanya kwa lengo la kuboresha fomula zinazotumika sasa hivi ambapo
kama utafiti huu utakubalika na kuanza kutumika basi unaweza kurahisisha
ukokotoaji wa hesabu zinazotumika viwandani.
Mbali na hayo mtafiti huyo
alisema fomula hiyo aliyogundua inauwezo wa kukokotoa hesabu za aina
mbili ambazo hujulikana kama (Arithmetic Progression na Sums of Powers)
ambapo hapo mwanzo zilikuwa zikitumia fomula tofauti.
“Baada ya kuwasilisha utafiti
wangu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kitivo cha Hesabu (UDSM)kwa
ajili ya kufanya uchunguzi na uhakiki, wataalam hao walijiridhisha na
kuona vyema watume utafiti huo katika Chuo Kikuu cha Manchester
Uingereza, ambapo chuo hicho ni miongoni mwa vyuo bora Duniani na ndipo
nilipotumiwa mwaliko huu,” alisema Mhandisi Maziku.
Hata hivyo mtafiti huyo amewasihi
watanzania watakaoguswa kumchangia wanaweza kuwasiliana naye kupitia
namba 0686-632 262 au 0713 037 123 kwa ajili ya kufanikisha safari hiyo,
kwani safari hiyo itasaidia kuitangaza nchi yetu pamoja na kupata
mtandao wa wanasayansi Duniani.
Mkutano huo unatarajiwa kufanyika
huko Marekani kuanzia tarehe Julai 11 hadi 15 mwaka huu katika Chuo
Kikuu cha Massachusetts na Utahushisha wanachama zaidi ya 13,000 Duniani
pamoja na Vyuo Vikuu vya Kisayansi takribani 500 Duniani kote.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni