Alhamisi, 30 Juni 2016

MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA VIWANGO TANZANIA (TBS),JOSEPH MASIKITIKO,ASIMAMISHWA KAZI KUPISHA UCHUNGUZI 

By Newsroom on, June 30 2016 
 Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS),Joseph Masikitiko (pichani)



Baada ya kusubiriwa kwa muda mwingi, hatimaye Manchester United inatarajia kumtangaza rasmi Zlatan Ibrahimovic kuwa mchezaji wake mpya.

Zlatan,34, atatangazwa Ijumaa hii kuwa mchezaji wa Man United iliyo chini ya Jose Mourinho.

Raia huyo wa Sweden amemaliza mkataba wake na PSG ya Ufaransa ambako alifanya vema baada ya maisha yake ya soka akiwa Ajax nchini Uholanzi baadaye nchini Italia akiwa na Juventus, Inter Milan na AC Milan, pia Barcelona ya Hispania.
Taarifa zinaeleza kwamba Man United na Zlatan kila kitu kipo katika hatua za mwisho kabisa.


Si unamjua Ryan Giggs? Ameamua kuondoka Manchester United baada ya kuitumikia kwa miaka 29 akiwa mchezaji na kocha msaidizi.

Giggs anaondoka baada ya kukataa ofa ya kuwa kocha msaidizi chini ya Kocha Mpya, Jose Mourinho.


Kabla, amekuwa kocha msaidizi chini ya makocha wawili David Moyes na Louis van Gaal ambaye alifanikiwa kubeba Kombe la FA.

Giggs ,44, alijiunga Man United mwaka 1987 akiwa ndiyo anasherekea siku yake ya kuzaliwa wakati akitimiza miaka 14. Alitokea timu ya watoto ya Manchester City.




Mshambuliaji nyota wa Zenit St Petersburg, Hulk ametua Shanghai SIPG kwa dau nono la pauni milioni 48.
Raia huyo wa Brazil, amevunja rekodi ya uhamisho iliyokuwa inashikiliwa na Alex Teixeira aliyesajiliwa Jiangsu Suning akitokea Shakhtar Donetsk, Februari, mwaka huu.
REKODI ZAKE:
2004: Vitoria Games 2 Goals 0
2005: Kawasaki Frontale Games 12 Goals 3
2006: Consadole Sapporo Games 41 Goals 26
2007: Tokyo Verdy Games 42 Goals 37
2008: Tokyo Verdy Games 14 Goals 8
2008-2012: Porto Games 170 Goals 89

2012-2016: Zenit Games 144 Goals 75




Kurejea kwa Kocha Jose Mourinho katika Ligi Kuu England na ugeni wa Pep Guardiola kutaamsha utamu wa ligi hiyo.

Gumzo zaidi kwa makocha wao ni vikosi vyao, vitakuwaje? Lakini kwa usajili ambao wanaendelea kufanya inaonekana vikosi vyao vitakuwa hivi ifuatavyo na vitarejesha raha na ushindani wa juu wa ligi kuu hiyo maarufu. 

VIKOSI:
United (4-2-3-1): De Gea; Fosu-Mensah, Smalling, Bailly, Shaw; Rooney, Schneiderlin; Rashford, Mkhitaryan, Martial; Ibrahimovic.

City (4-2-3-1): Hart; Sagna, Kompany, Otamendi, Clichy; Fernandinho, Gundogan; De Bruyne, Silva, Nolito; Aguero.

MECHI TATU ZA MWANZO:
MANCHESTER CITY
July 22 - Bayern Munich (A)
July 25 - Manchester United (N)
July 28 - Borussia Dortmund (N)
MANCHESTER UNITED 
July 22 - Borussia Dortmund (N)
July 25 - Manchester City (N)
August 3 - Everton (H)

MAGULI HUYO "OMAN"

Maguli-uarabuni 1

MSHAMBULIZI wa Taifa Stars, Elius Maguli amekamilisha usajili wake kutoka Stand United ya Shinyanga kama mchezaji huru na kujiunga katika klabu ya Dhofar SC ya Oman Professional League.
Kila mmoja anakumbuka namna mchezaji huyo alivyopitia kipindi kigumu msimu wa 2014/15 akiwa na kikosi cha Simba SC ambacho kabla ya kuanza kwa msimu wa 2015/16 kocha aliyepita wa kikosi hicho, Dylan Kerr alitangaza kutomuhitaji na uongozi ukavunja mkataba wake akiwa bado na mwaka mmoja zaidi.
Kitendo cha kujiunga na kocha Mfaransa, Patrick Liewig katika timu ya Stand kabla ya kuanza kwa msimu uliopita hakikuonekana kuwastua wengi lakini game 9 za mwanzo wa msimu ziliambatana na magoli 9 kwa mchezaji huyo wa zamani wa Ruvu Shooting, pia alishinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi katika VPL na kujumuhishwa katika timu ya Taifa kwa mara ya kwanza baada ya miaka mitatu.
Kujiunga na Dhofar timu iliyomaliza katika nafasi ya tano katika ligi ya kulipwa mwaka mmoja uliopita ni hatua kubwa kwa mchezaji kijana kama Maguli ambaye ameondoka VPL akiwa amefunga jumla ya magoli 33 katika misimu yake mitatu aliyocheza kama mchezaji wa vilabu vya Shooting, Simba na Stand United.
Ameruka vikwazo vingi katika ‘soka lenye fitna’ na matatizo mengi ya watendaji. Mfano, katika misimu yake miwili ya mwisho VPL (Simba na Stand) timu hizo zote mbili zimejaa migogoro ya kiutendaji kati ya viongozi na wachezaji au viongozi kwa viongozi.
Katika mazingira hayo si rahisi kwa mchezaji kutimiza malengo yake na inapotokea nafasi kama hii ya Maguli-Kusajiliwa moja kwa moja na timu ya kulipwa ukiwa U25 ni jambo la kumshukuru Mungu na pengine ni sehemu ya kufanya kazi nzuri zaidi kwa jitihada ili kuthibitisha kwa wale waliokusaini kuwa hawakufanya makosa.
Maguli ni mshambuliaji wa kikosi cha kwanza katika timu ya Taifa ya Tanzania kwa mwaka mmoja sasa akicheza sambamba na Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta katika safu ya mashambulizi kwa maana hiyo, kocha Charles Mkwassa ataendelea kufurahia vijana wake watatu wakiwa ng’ambo ya nchi kuendeleza vipaji vyao na kudumisha viwango vyao vya kiuchezaji.
Kama Hamis Mroki anayecheza Thailand, huyu ni nahodha wa kikosi cha vijana kilichokuwa kikiwajumuhisha kina Ulimwengu, Himid Mao na wengine ni zao la TSA, Samatta, Tom, Maguli, Mrisho Ngassa watatupiwa jicho la 3 bila shaka timu ya Taifa Stars itaimarika licha ya kwamba bado hatuna ligi makini ya ndani.
Dhofar ni timu iliyoanzishwa miaka 44 iliyopita, na Oman kuna mishahara mikubwa hadi kufikia dola 30,000 kwa mchezaji wa kiwango cha Maguli. Mchezaji wa kikosi cha kwanza wa timu ya Taifa. Sasa mastaa watatu wa Stars katika kikosi cha mashambulizi wapo ng’ambo. Kila la heri Elius Maguli.
Kwa ukaribu zaidi, tafadhali unaweza ku-LIKE PAGE yangu BSports. Utapata Updates za michuano mbalimbali.

Ulinzi vituo vya DART kuimarishwa

DARAJANI

Baadhi ya abiria wanaotumia usafiri wa mabasi yaendayo kasi maarufu kama mwendo kasi wameilalamikia kampuni hiyo kwa kushindwa kudhibiti vitendo vya wizi vinavyoendelea katika baadhi ya vituo hivyo.
Bw. Juma Ally mkazi wa Kimara mwisho anasema vitendo hivyo hutokea nyakati za usiku kwa baadhi ya vijana kujifanya nao ni miongoni mwa watumiaji daraja hilo na kupelekea abiria kuibiwa vitu vyao ikiwa ni pamoja na kujeruhiwa.
Aliongezea kuwa walinzi wa kituo hicho wamekuwa wakifanya kazi ya kuwapanga abiria na kusahau majukumu yao ya kulinda usalama wa kituo hicho pamoja na mali zao.
“Tunashangaa hawa walinzi wanaolinda vituo hivi, abiria wamekuwa wakilalamika kila siku kuibiwa nyakati za usiku lakini tunaona abiria wakiendelea kuibiwa sijui wahusika wapo wapi?”Aliuliza Bw. Ally.
Nae Bi. Herrieth Shangaa aliongezea kuwa licha ya vitendo vya wizi vinavyoendelea katika vituo hivyo kuna baadhi ya vitendo vikiwemo vya kujisaidia katika madaraja hayo hivyo kupelekea uchafuzi wa mazingira
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi msimamizi wa vituo hivyo ambae hakutaja kutajwa jina lake amesema kuna baadhi ya vituo ni vikubwa na wanawalinzi wachache hivyo wamejipanga kuongeza ulinzi ikiwa ni pamoja na kufunga mfumo wa kidigitali wa kudhibiti wahalifu
Mradi wa mabasi yaendayo haraka ulioanza rasmi terehe 10, mei, 2016 umeonesha ni jinsi gani kero ya foleni itakavyopungua kwa kuwa mabasi hayo yanatumia njia yake ambayo ni miundombinu  iliyojengwa kwa  gharama kubwa  sana.

siku ya mwisho wa zoezi la kuhakiki silaha

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TZ
TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI
Ndugu zangu waandishi wa habari,
Leo tarehe 30.6.2016 ndiyo tarehe na siku ya mwisho wa zoezi la kuhakiki silaha. Kwa mujibu wa takwimu za silaha tulizonazo inaonyesha kwamba wapo baadhi ya wamiliki wa silaha ambao hawajatekeleza agizo la kuhakiki silaha wanazozimiliki.
Kufutia hali hiyo, natoa angalizo kwa wale wote ambao hawajahikiki silaha zao kwamba muda wowote kuanzia sasa tutaanza operesheni maalum ya kutafuta silaha ambazo hazijahikikiwa.  Ifahamike kwamba yeyote atakaye kutwa na silaha ambayo haijahakikiwa atachuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo  kupoteza sifa ya kuwa mmiliki halali wa silaha hiyo.
Tunatoa agizo kwa wamiliki binafsi wa maghala ya silaha waziwasilishe silaha hizo pamoja na nyaraka zake katika vituo vya karibu vya Polisi kwa ajili ya uhakiki.
Imetolewa:-
Nsato M. Mssanzya – CP
Kamishina wa Polisi Operesheni na Mafunzo
Makao Makuu ya Polisi

KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI-MNH

M1 
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Taifa Muhimbili   Profesa Lawrence Museru  akifungua kikao cha 16 cha Baraza hilo kilichofanyika  leo Juni 30, 2016  katika ukumbi wa NACTE Mikocheni jijini Dar es salaam. Kulia ni Katibu wa Baraza hilo Dk. Kisah Mwambene na kushoto ni Katibu Msaidizi Enezer Msuya.
M2 
Katibu wa TUGHE mkoa Bwana.  Gaudence  Kadyango   akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa mikataba ya hali bora za kazi na faida zake.
M3 
Bwana.  Andrew Mwalwisi  kutoka Tume ya Usuluhishi  -CMA-   akiwasilisha mada  katika kikao cha Baraza la wafanyakazi  wa MNH .
M4Mwenyekiti wa TUGHE  Tawi la Muhimbili Mziwanda Salum Chimwege akiuza swali   kwa viongozi wa Baraza  la MNH  katika kikao hicho  .
M5 
Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa- MNH -Alex   Samweli  akitoa hoja katika kikao hicho  kilichofayika leo.

Mlipuko wa bomu wawaua watu 18 Somalia

  • By Newsroom on June 30 2016
Mlipuko wa bomu Somalia
Habari kutoka Somalia zinasema kuwa watu 18 wameuawa baada ya bomu kulipuka na kuharibu kabisa basi walimokuwa wakisafiria katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
Bomu lililokuwa limetegwa kando ya barabara lililipua gari lililokuwa limewabeba abiria. Wote waliouawa walikuwa raia.
Mashambulizi hayo yalitokea katika mji wa karibu wa Lafole.
Inadhaniwa kuwa washambuliaji hao walikuwa wakilenga gari la wanajeshi lililokuwa karibu.
Mara kwa mara wapiganaji wa Al Shaabab hulenga wanajeshi wa Serikali.

Mwandishi wa ''The Concubine'' afariki







Marehemu Elechi Amadi
Mwandishi maarufu wa Nigeria Elechi Amadi amefariki akiwa na umri wa miaka 82.
Amadi ambaye aliandika vitabu maarufu kama vile The Concubine,Isiburu,Sunset in Biafra,Peppersoup na The Road to Ibadan alifariki siku ya Jumatano mwendo wa saa tisa,wiki moja moja baada ya kuripotiwa kuugua.
Duru zimearifu kuwa marehemu alitarajiwa kuhudhuria hafla ya kusoma vitabu katika bandari ya Hacourt lakini hakuweza kutokana na kuugua kwake.
Akiwa mzaliwa wa eneo la Aluu katika jimbo la Riverstate mwaka 1934,Elecchi Amadi alisoma katika taasis ya Umuahia,Oyo na chuo kikuu cha Ibadan ambapo alipata shahada yake katika somo la fizikia na hesabati.
Pia aliwahi kufanya kazi kama mpimaji wa mashamba.

SERIKALI YATANGAZA KIAMA CHA WAUZA DAWA NA VIPODOZI HATARI MITANDAONI

TZNa Fatma Salum (MAELEZO)
——————————
Serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imesema hivi karibuni itaanza msako mkali wa kuwatafuta na kuwakamata wauzaji wa dawa zinazokatazwa pamoja na vipodozi vikali ambao wanajitangaza kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.
Hayo yamesemwa na Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Umma kutoka TFDA Bi. Gaudensia Simwanza wakati wa mahojiano na mwandishi wa habari hii kuhusu kuibuka kwa watu wanaotangaza  biashara ya dawa na vipodozi ambavyo Serikali imevipiga marufuku.
Akitaja bidhaa hizo Bi. Simwanza alisema ni pamoja na dawa za kuongeza ukubwa wa viungo vya mwili, kupunguza uzito wa mwili na vipodozi vyenye kemikali za kuchubua ngozi bidhaa ambazo zinasababisha madhara makubwa kwa binadamu ikiwemo ugonjwa wa Saratani.
“Kumezuka wafanyabiashara holela wanaotumia mitandao ya kijamii kama vile Instagram, Facebook, Whatsup Groups na kwengineko  kutangaza biashara ya dawa na vipodozi vyenye kemikali hatari ambavyo vimepigwa marufuku na TFDA hivyo wanaohusika wajiandae, hivi karibuni tutaanza kuwashughulikia.” Alisema Simwanza.
Alibainisha kuwa bidhaa hizo nyingi hazijathibitishwa na kupewa kibali na TFDA hivyo wauzaji wanakiuka Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi Sura ya 219 inayowataka wafanyabiashara wote wa bidhaa hizo kuzisajili kabla hazijaenda kwa  mtumiaji na kutofanya hivyo ni kwenda kinyume na Sheria.
Alieleza kuwa TFDA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wameandaa mkakati madhubuti wa kuhakikisha wanawabaini na kuwakamata wafanyabiashara wote wanaouza dawa na vipodozi hivyo kupitia mitandao na kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafikisha mahakamani au kuwatoza faini.
“Wengi wa wafanyabiashara hao hawaweki anuani za maeneo wanayopatikana na hawana maduka rasmi bali huweka namba za simu za mkononi lakini kwa kutumia vyombo vya dola tutawabaini tu na kuwatia mbaroni.” Alisisitiza Simwanza.
Kwa upande wake Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Innocent Mungy amewatahadharisha watumiaji wa huduma za mawasiliano hasa matangazo ya biashara kuwa makini na matangazo hayo kwani baadhi ya wafanyabiashara hizo wanaweza kuwa ni watu wenye nia mbaya.
Hivi karibuni kumeibuka wimbi la wafanyabiashara wa dawa mbalimbali pamoja na vipodozi ambao wanajitangaza kupitia mitandao ya kijamii na kuna baadhi ya watu wananunua bidhaa hizo bila ya kuhakikisha usalama wake jambo ambalo ni hatari kwa afya zao.

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA (NHC) LAANZA KUTOA HUDUMA KATIKA MAONESHO YA 40 YA KIMATAIFA ya SABASABA

1 2 
Banda  la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) likiwa katika  Maonesho ya 40 ya Kimataifa ya Biashara, yanayofanyika kila mwaka katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Sabasaba  jijini Dar es salaam tayari limeanza rasmi kutoa huduma zake katika viwanja hivyo.
3 
Afisa Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),Bi Edith Nguruwe akiwapa maelezo wananchi waliotembelea banda la (NHC) kuhusina na huduma zinazotolewa na Shirika hilo.
4 
Afisa Mauzo Mwandamizi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Emmanuel Limo (kushoto), akimuelezea Wananchi Kuhusiana na mradi wa SAFARI CITY  uliopo Arusha alipotembelea banda hilo katika maonesho ya Sabasaba.
5 
Afisa biashara (NHC), Clara Lubanga akitoa ufafanuzi kwa mmoja wa Wananchi aliotembelea banda hilo kuhusiana uzwaji wa nyumba (katikati), Afisa Mauzo wa (NHC), Joseph Haule.
6 
Afisa Mauzo (NHC), Jasson Ipyana akimuelezea mwananchi kuhusina na miradi ya nyumba y
a bei nafuu ilioko nchini.
7 
Bw: Klison Sanane (kushoto), akifafanua miradi mbalimbali ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
8 
Aika Swai (kushoto), akielezea kuhusiana na utaratibu wa unaoutumika katika ununuzi wa  nyumba za  (NHC) huku baadhi ya wadau kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wakimsikiliza kwa umakini.
PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMON-FULLSHANGWEBLOG.

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam YASHIRIKI MAONESHO YA SABASABA

1 
Mtendaji Mkuu wa Mahakama  Tanzania Bw. Hussein Kattanga akisikiliza maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam Bi. Mary Shirima wakati wa maonyesho ya kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijin Dar es Salaam
3Wanausalama wakiimarisha ulinzi katika viwanja vya sabasaba ili wafanyabiashara na wananchi waweze kufanya shughuli zao kwa amani.
4Mwanafunzi kutoka chuo cha VETA wa pili kutoka kulia akiwaelekeza baadhi ya wananchi ubunifu wa kutengeneza boti itakayokuwa inatembea barabarani kwa kuendeshwa na dereva mpaka baharini
Picha na Benjamin Sawe

MFUKO WA PENSHENI WA PPF KUTOA HUDUMA ZOTE KWA WATEJA WAKE VIWANJA VYA SABASABA

By Newsroom on June 29, 2016
Muonekano wa nje ya Jengo la PPF lililopo Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa vya Mwalimu Nyerere jijini Dar esSalaam (Sabasaba).
 Maandalizi
 Afisa Mafao wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Tulla Mwigune (kulia) Afisa Michango wa Mfuko huo, Saluna Aziz Ally (katikati) na Afisa Michango Glory Maboya, wakijiandaa kuhudumia wateja leo asubuhi katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba.
 Afisa Utafiti Neema Mjema (nyuma) na Mwanasheria wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Nyambilila Ndoboka, pia wakijiandaa kuweka mambo sawa kabla ya kuanza kupokea wateja katika Bandao lao la Maonesho kwenye Viwanja vya Sabasaba leo.
 Afisa Uwekezaji wa Mfuko huo, Jonas Mbwambo akiweka mambo sawa kabla ya kuanza kupokea wateja katika Banda lao namba 86 viwanja vya Saba saba.
 Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Pauline Msanga, akitoa maelezo kwa wananchi kuhusu Huduma za uendeshaji Mfuko huo, wakati walipotembelea katika Banda lao lililopo kwenye Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam, leo. 
 Sehemu ya wananchi waliotembelea Banda la Mfuko wa Pensheni wa PPF wakipata elimu kuhusu Mafao yatolewayo na Mfuko huo na jinsi mwanachama anavyoweza kujiunga na kuchangia.
Continue reading →

HABARI ZA KIMICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA

tffKIKOSI CHA TWIGA STARS
Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Mpira wa Miguu ya Wanawake Tanzania, Nasra Juma ametangaza majina ya wachezaji 23 watakaounda kikosi cha Twiga Stars.
Kikosi hicho kinatarajiwa kwenda Kigali, Rwanda Julai 15, 2016 kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Rwanda ikiwa ni mwaliko maalumu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Rwanda (Ferwafa).
Wakati Ferwafa likiingiza mchezo huo wa Julai 17, 2016 kwenye orodha ya michezo inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira na Miguu la Kimataifa (Fifa), lakini Mheshimiwa Rais wa Rwanda Paul Kagame kuwa sehemu ya burudani ya burudani mbele ya wageni wake ambao ni wakuu mbalimbali wanaounda Umoja wa Nchi za Afrika (AU) ambao watakuwa na mkutano wao nchini Rwanda.
Mbali ya soka kama burudani, pia Rais Kagame atatumia mchezo huo kama hamasa kwa wakuu wa nchi ili kutoa kipaumbele kwenye soka la wanawake ambako kwa sasa ni ajira ambayo inakwenda sambamba na kuitikia wito wa kupambana na changamoto za malengo ya millennia (MCC) ambayo pia yanataka wanawake wapate nafasi.
Makipa:
  1. Fatma Omary
  2. Belina Julius
  3. Najiat Abbas
Walinzi:
  1. Stumai Abdallah
  2. Fatma Issa
  3. Anastazia Antony
  4. Happuness Henziron
  5. Maimuna Khamis
Viungo:
  1. Donisia Daniel
  2. Amina Ali
  3. Amina Ramadhani
  4. Fatuma Bashiri
  5. Wema Richard
  6. Fadhila Hamadi
  7. Mwajuma Abdallah
  8. Anna Hebron
  9. Sophia Mwasikili
Washambuaji:
  1. Tumaini Michael
  2. Johari Shaaban
  3. Fatma Idd
  4. Shelder Bonifdace Mafuru
  5. Asha Saada Rashid
  6. Mwanakhamisi Omar 
…………………………………………………………………….
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA

Viwanda visivyo endelezwa kurudishwa kwa watanzania

W1 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage
—————————————————
Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma
Viwanda vilivyobinafsishwa na Serikali ambavyo haviendelezwi kutwaliwa ili kutolewa kwa wawekezaji wenye uwezo wa kuviendesha.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage ameyasema hayo leo mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Tabora Mjini Mhe. Emmanuel Mwakasaka aliyetaka kujua hatua zinazochukuliwa juu ya mwekezaji wa kiwanda cha nyuzi Tabora kwa kushindwa kuendeleza kiwanda hicho.
“Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina inaendelea na tathmini ya viwanda vyote vilivyobinafsishwa na Serikali kikiwemo kiwanda cha nyuzi cha Tabora ili kujiridhisha kama wawekezaji wa viwanda hivyo wanatimiza matakwa ya mkataba na Serikali,” alifafanua Mhe. Mwijage.
Aliendelea kwa kusema kuwa, ikiwa viwanda hivyo vitabainika kubadilishwa matumizi yake au kutoendelezwa basi Serikali itavirudisha kwa watanzani ili viweze kuendelezwa.
Aidha Mhe. Mwijage amesema kuwa, kwa sasa mwitikio wa kuviendeleza viwanda ambavyo vilikuwa havizalishi ni mzuri kwani viwanda vingi vimeanza kufanya kazi lakini kwa wale ambao watashindwa kabisa  kuviendeleza basi viwanda hivyo vitarejeshwa kwa watanzania.
Vile vile Mhe. Mwijage amesema kuwa dhana ya Serikali ya awamu ya Tano ya kujenga uchumi wa viwanda inaenda pamoja na kurejesha Serikalini viwanda vyote vilivyobinafsishwa lakini haviendelezwi ili vitolewe kwa wawekezaji wengine.
Sambamba na hayo Mhe. Mwijage amesema kuwa kufufua viwanda, hasa viwanda vya nguo ni pamoja na wakulima wa pamba kulima zao hilo kwa wingi kwa ajili ya uchakataji pamoja na kudhoofisha uingizaji wa nguo za mitumba nchini.
Wizara hiyo inaendelea na kushawishi wawekezaji mbalimbali ili kujenga viwanda vingi iwezekavyo kwa ajili ya uchakataji wa mazao yanayolimwa nchini pamoja na mifugo.

Bunge limepitisha muswada wa marekebisha ya sheria ya ununuzi wa umma wa mwaka 2016

3Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma
——————–
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo limepitisha muswada wa marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa Mwaka 2016 wenye lengo la kupunguza gharama na muda wa mchakato wa manunuzi Serikalini.
Marekebisho hayo yametokana na gharama kubwa ambayo Serikali imekuwa ikitumia kutokana na huduma na Bidhaa zinazonunuliwa na Serikali kuwa za juu ikilinganishwa na bei ya wastani ya soko.
“Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa mwaka 2016 una lengo la kuongeza ufanisi katika ununuzi wa Umma kwa kuondoa mapungufu yaliyopo katika Sheria ya sasa kwa kupunguza gharama na muda wa michakato ya ununuzi, kutoa upendeleo kwa kampuni za ndani, vikundi maalum, malighafi na bidhaa zinazozalishwa nchini pamoja na kuweka viwango mahsusi kwa bidhaa zitakazotumiwa na Serikali,” alifafanua Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju.
Mhe. Masaju ameendelea kwa kusema kuwa sheria hiyo imeweka kifungu cha dharura  ili kuwezesha vitu vya kuokoa uhai na vinginevyo kununuliwa kwa dharura pindi inapobidi.
Kwa upande wake Mbunge wa Babati Vijijini Mhe. Jitu Soni yeye ameiomba Serikali kuruhusu kununua vifaa tiba vilivyotumika ambavyo muda wake wa kutumia hauna mwisho, kwa mfano vitanda vya kujifungulia  ili kupunguza gharama ya kununua vitanda vipya na kuweza kununua vitanda vingi kwa wakati mmoja.
Aidha Mhe. Jitu ameiomba Serikali kuirudisha tena Sheria hiyo Bungeni baada ya mwaka mmoja ili kufanyiwa marekebisho na kuziba mianya yote ambayo itakuwa imebainika mara baada ya utekelezaji wake kuanza.
Muswada wa marekebisho ya sheria hiyo yanasubiri kusainiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli ili kuanza utekelezaji wake.

MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI DODOMA

B1 
Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akijibu maswali ya Wabunge Leo Bungeni Mjini Dodoma kuhusu mpango wa Serikali wa kuimarisha Viwanda  vilivyopo hapa nchini na kujenga vipya katika Mikoa mbalimbali.
B2 
Waziri wa Elimu Sayansi Teknolojia na Mafunzo ya ufundi Mhe. Dkt. Joyce Ndalichako akieleza juu ya mkakati wa Serikali kuimarisha vyuo vya Ufundi Stadi hapa nchini wakati wa kipindi cha maswali na majibu Bungeni Mjini Dodoma.
B3 
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakiyembe akiteta jambo na Mbunge wa Korogwe Vijijini Mhe. Steven Ngonyani Bungeni Mjini Dodoma Leo.
B4 
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.Philip Mpango  akijibu hoja za wabunge kuhusu Muswada wa Marekebisha ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa mwaka 2016 Leo Bungeni Mjini Dodoma.
B5 
Naibu Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Edwin Ngonyani akitoa ufafanuzi kuhusu mikakati ya Serikali kuimarisha miundombinu ya Barabara hapa Nchini.
B6 
Naibu Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Edwin Ngonyani akitoa ufafanuzi kuhusu mikakati ya Serikali kuimarisha miundombinu ya Barabara hapa Nchini.
B8 
Mbunge Viti Maalum Mhe. Martha Mlata akichangia hoja wakati wa uwasilishwaji wa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa mwaka 2016.
B7 
Baadhi ya Wabunge wakimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (wa katikati) mara baada ya kupitishwa kwa muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma.
(Picha zote na Frank Mvungi-Dodoma)