Alhamisi, 14 Aprili 2016


Mcheza kikapu maarufu wa Marekani, Kobe Bryant amestaafu kucheza mpira wa kikapu.

Nyota huyo wa LA Lakers amestaafu na kuagwa na mashabiki kibao wakiwemo nyota wa muziki kama Jay Z, soka wakiongozwa na David Beckham na kikapu wakiongozwa na Magic Johnson.

Katika siku hiyo ya kuagwa, Kobe aliyechezea kwenye NBA kwa miaka 20, aliingoza Lakers kushinda kwa pointi 101-96 dhidi ya Utah Jazz huku yeye akifunga pointi 60 na kuweka rekodi ya aina yake.





















Hakuna maoni:

Chapisha Maoni