Balozi Amina Salum Ali awataka watendaji Wizarani kuleta mabadiliko katika utendaji wa kazi
WAZIRI
 wa Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar,  Balozi Amina Salum Ali 
amewataka watendaji wa Wizara hiyo kuleta mabadiliko katika utendaji wa 
kazi, ili kuifanya Zanzibar iweze kufikia katika uchumi wa kati.
Alisema
 kuwa, Wizara imeandaa sera  mbali mbali ambazo zinaweza kuifanya 
Zanzibar kufikia uchumi wa kati, ikiwa ni pamoja na sera ya biashara, 
viwanda na sera ya mpangokazi ambao utekelezaji wake utaanza leo (jana).
Akizuzungumza
 na watendaji wa Wizara hiyo pamoja na waandishi wa habari kutoka vyombo
 tofauti katika ukumbi wa Makonyo Chake Chake, alisema ipo haja kwa 
watendaji wake kujibadilisha kwa kuwa na sera madhubuti ya  kuwa na 
viwanda vikubwa, ambavyo vitaifanya Zanzibar kufikia uchumi wa kati.
Alieleza
 suala la kukuza viwanda Zanzibar kuwa, Wizara inataka kukiendeleza 
kiwanada cha sukari Mahonda, kujenga kiwanda cha maziwa, kiwanda cha 
Zanzibar Milin na kiwanda cha makonyo ambacho hutoa mafuta ya karafuu, 
makonyo na mafuta mengine ya mimea.
 ”Kuna
 mambo lazima tuyabadilishe, kwanza utendaji wa kazi wa silka ya kawaida
 ambapo wanataraji matokeo yatakayobadilisha maisha ya wananchi, 
utendaji utakaotuletea mapato na maendeleo, hii ndio itakayoifanya 
Zanzibar kufikia uchumi wa kati”, alisema Balozi huyo.
Balozi
 Amina aliwataka watendaji hao kufanya kazi ya ziada katika kubadilisha 
Zanzibar  na kuwa ya maendeleo zaidi kwa kutumia bidhaa zinazotokana na 
kilimo.
Alisema
 kuwa, asilimia 85 ya viwanda Zanzibar ni vya wananchi, hivyo ni vyema 
juhudi zikatendeka katika kuvibadilisha na kufikia viwanda vikubwa, 
kwani Zanzibar inayo nafasi kubwa ya kuzalisha na kuuza bidhaa 
zinazotokana na kilimo.
”Tunatakiwa
 tufanye kazi ya kuibadilisha Zanzibar kwa kutumia bidhaa zinazotokana 
na mimea, kwani uzalishaji unataka bidii kubwa, hivyo ipo haja ya 
kuwashirikisha wa Zanzibar na nje yake kwa kutembeleanaili kuona wenzetu
 wanafanya nini na sisi tuweze kufuata”, alieleza Waziri huyo.
Waziri
 huyo alisema, ipo haja ya kutolewa elimu kwa wajasiriamali na 
kuwezeshwa kwa kupitia sehemu za nje zenye maeneo ya kiuchumi ili 
kujifunza mambo mbali mbali ambayo wataiga kutoka huko.
”Ili
 tufikie huo uchumi wa kati ni lazima Serikali ijipange kuwawezesha 
wajasiriamali na wawekeze kupitia sehemu za wenzao ka kuwatembeza, 
kupatiwa elimu na soko, jambo ambalo ni changamoto kubwa kwetu”, 
alieleza.
Akizungumzia
 suala la karafuu alieleza kuwa, Zanzibar imefanya vizuri kwa miaka 
mitano iliyopita kwa uzalishali wa zao hilo, ambapo Serikali imenunua 
tani elfu 20 kutoka kwa wananchi, ikiwa na thamani ya shilingi billioni 
285.89.
”Serikali
 imejiandaa vizuri na bei itaendelea kuwa ile ile kama alivyoahidi Rais 
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed 
Shein, lengo ni kuivusha Zanzibar kwenda katika uchumi wa kati”, 
alisema.
Alisema
 bei ya ununuzi wa zao la karafuu haijashushwa kama baadhi ya wananchi 
wanavyodai, kwani hiyo ni ahadi ya serikali katika kustawisha maisha ya 
wakulima wa zao hilo.
Aliwataka
 wananchi kuacha kabisa uuzaji wa karafuu kwa njia ya magendo na 
waendelee kuuza hapa Zanzibar, kwani fedha zinapoingia serikalini 
huwafaa wananchi wenyewe kutokana na huduma za kijamii.
”Pia
 tufanye biashara inayokubalika kimataifa, karafuu zetu tusuzichanganye 
na makonyo kwa sababu kuna ushindani mkubwa wa soko, hivyo ni vyema 
tukazianika sehemu sahihi na kuwa kavu kabisa”, alifahamisha.
Aidha
 alisema kuwa, Wizara itakuwa na utaratibu wa kuangalia bei ya vyakula 
na kuhakikisha kwamba vyakula vinavyoingia vinakuwa na viwango vya 
kimataifa pamoja na usafi.
”Tuko
 tayari kuingia katika mapambano, kwa nini tusiwe na viwango vya vyakula
 vinavyoingia wakati nchi nyengine wanavyo, tutahakikisha zinaingia 
bidha zenye ubora na viwango”, alisisitiza.
Mwandishi
 wa habari Salim Ali Mselem kutoka redio Istiqama akiuliza swali, 
alisema serikali itapanga sera ipi ambayo itawawezesha wananchi wote 
wakati wanapoimarisha upande huu, wananchi hukwama kwa upande wapili.
”Zao
 la karafuu limeongezwa bei lakini na kodi inaongezeka kwa 
wafanyabiashara siku hadi siku, jambo ambalo wenye kipato cha chini 
wanaumia, kwa mfano wafanyabiashara wa sokoni hapa Chake Chake wanatozwa
 kodi elfu 60 badala ya elfu 30, kweli wananchi wanawezeshwa hivi”, 
alihoji Salim.
Nae
 Nasra Mohamedi kutoka ZBC televisheni akitoa hoja yake kuwa, kama 
iliyoelezwa wajasiriamali wapo asilimia  85, hivyo serikali itafute njia
 mbadala ya kuwawezesha ili kutumia njia ya digital katika kufanya kazi 
zao ili kufikia maendeleo zaidi.
Waziri
 Amina alikuwa kwenye ziara ya kutembelea vitengo mbali mbali vya 
Wizara, ambapo aliona jitihada mbali mbali zinazofanywa na wajsiriamali 
na kujionea mambo mbali mbali ambayo hufanywa katika kiwanda cha makonyo
 Wawi Chake Chake, ikiwa ni pamoja na mafuta yanayotengenezwa kwa 
karafuu na makonyo
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni