DC HAPI ATEMBELEA WANANCHI WA BUNJU, MBWENI WALIOKUMBWA NA MAFURIKO
Mkuu
wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam Mh. Ally Hapi leo
amewatembelea wananchi maeneo ya Bunju na Mbweni waliokuwa na kero
mbalimbali.
Katika eneo la Bunju Kilungule, baadhi ya wananchi nyumba zao zimezungukwa na maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Mkuu wa Wilaya akiambatana na Katibu tawala wa Mkoa wa Dar es salaam na mainjinia wa manispaa alitembelea eneo hilo na kuona adha inayowapata wananchi.
Akipokea maelezo ya Mwenyekiti wa serikali ya mtaa na baadae kuzungumza na wananchi wa eneo hilo, mkuu wa wilaya aliambiwa na baadhi ya wakazi wa asili wa eneo hilo kuwa sehemu hiyo ilikua ni bwawa la maji miaka yote.
Wakazi hao ambao nyumba zao zimezungukwa na maji walimuomba Mkuu wa wilaya kusaidiwa pampu kubwa ili maji hayo yavutwe na kupelekwa kwenye mitaro upande wa pili wa barabara.
Katika eneo la Bunju Kilungule, baadhi ya wananchi nyumba zao zimezungukwa na maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Mkuu wa Wilaya akiambatana na Katibu tawala wa Mkoa wa Dar es salaam na mainjinia wa manispaa alitembelea eneo hilo na kuona adha inayowapata wananchi.
Akipokea maelezo ya Mwenyekiti wa serikali ya mtaa na baadae kuzungumza na wananchi wa eneo hilo, mkuu wa wilaya aliambiwa na baadhi ya wakazi wa asili wa eneo hilo kuwa sehemu hiyo ilikua ni bwawa la maji miaka yote.
Wakazi hao ambao nyumba zao zimezungukwa na maji walimuomba Mkuu wa wilaya kusaidiwa pampu kubwa ili maji hayo yavutwe na kupelekwa kwenye mitaro upande wa pili wa barabara.
Akijibu maombi hayo Mh. Hapi
aliwaagiza mainjinia wa manispaa kuhakikisha kuwa wanafanya utaratibu wa
kupata pampu kubwa ya kuvuta maji hayo. Aidha, Mkuu huyo wa wilaya ya
Kinondoni aliwaambia wananchi kuwa wale wote waliojenga katika eneo
hilo ambalo ramani inaonesha kuwa ni eneo la wazi wajiandae kuondoka.
“Serikali itawasaidia kutoa haya
maji kama hatua ya dharura. Lakini suluhu ya kudumu ni kuwa waliojenga
hapa wote wamejenga eneo la wazi tena ni bwawa. Hivyo lazima wajiandae
kuhama.
Serikali kazi yake ni kuwaambia wananchi ukweli, hata kama ukweli huo utakua na maumivu. Hivyo ukweli wa jambo hili ni kuwa waliojenga hapa wahame.”
Serikali kazi yake ni kuwaambia wananchi ukweli, hata kama ukweli huo utakua na maumivu. Hivyo ukweli wa jambo hili ni kuwa waliojenga hapa wahame.”
Akitoa rai kwa viongozi wa
serikali ya mtaa ambao wameshiriki katika kuuza eneo hilo kinyume na
taratibu mh. Mkuu wa Wilaya aliagiza na kusema
” kila Mwananchi aliyejenga hapa
aende ofisi ya mtaa kujisajili akiwa na vielelezo vyote vya kumiliki
eneo hili na alikonunua. Kisha nipewe taarifa na uhakiki utafanyika.
Kama kuna viongozi wa serikali ya mtaa walishiriki kuuzia watu viwanja
hapa kinyume na ramani ambayo wao wana nakala yao basi wajiandae
kuwajibishwa.”
Katika hatua nyingine Mkuu wa
Wilaya alitembelea eneo la Mbweni ambako Mwananchi asiyefahamika
amejenga ukuta kuzunguka eneo la wazi. Hapi alifika eneo hilo na
kujionea ukuta huo kisha akaagiza mtendaji wa mtaa pamoja na anayejenga
ukuta huo kufika ofisini kwake kesho Ijumaa mchana wakiwa na vielelezo
vyote na vibali vya ujenzi kama wanavyo.
Ziara ya mkuu wa wilaya inaendelea muda huu katika maeneo ya barabara za Sinza ambazo wakandarasi walipewa kujenga
Ziara ya mkuu wa wilaya inaendelea muda huu katika maeneo ya barabara za Sinza ambazo wakandarasi walipewa kujenga
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni