WANAMTANDAO WAITAKA DAWASCO KUTUPIA JICHO TABAKA LA WASIOJIWEZAWANAMTANDAO WAITAKA DAWASCO KUTUPIA JICHO TABAKA LA WASIOJIWEZA
Mtendaji
 Mkuu wa Shirika la Maji safi na Usafi wa Mazingira jijini Dar es Salaam
 (DAWASCO) Mhandisi Cyprian Luhemeja akifurahia jambo na ujumbe kutoka  
Mtandao Kijinsia Tanzania (TGNP) walipofika ofsini hapo kwa ajili ya 
kutoa shukrani zao.
…………………………………………………………………………………………
WANAMTANDAO WAITAKA DAWASCO KUTUPIA JICHO TABAKA LA WASIOJIWEZA
WANAHARAKATI
 WA Mtandao wa kijinsia “TGNP” wamepongeza juhudi zinazofanywa na 
Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es salaam (Dawasco), kutokana na 
Mabadiliko na jitihada zinazofanywa na Dawasco za kuboresha huduma ya 
Maji pamoja na kufanya kazi za kusaidia jamii inayoizunguka.
Akizungumza
 katika kikao cha pamoja na Dawasco, Mratibu wa kampeni ya Maji ya “MAMA
 TUA NDOO KICHWANI” kutoka Mtandao wa Kijinsia Bi. Martha Samwel. 
Ameitaka
 Dawasco kuhakikisha inapeleka huduma ya Majisafi na salama katika 
sehemu zote muhimu ikiwamo mashuleni na hospitalini ili kumpunguzia 
mwanamke adha ya kutafuta Maji kutoka umbali mrefu pamoja na kumuondolea
 mwanamke adha ya kubakwa na hata kupigwa kutokana na kuhangaika 
kutafuta Maji. 
“Tunataka
 kutoa salamu za pongezi kwa DAWASCO kwa mabadiliko na  jitihada 
tunazoziona za kuboresha huduma ya Maji na kufanya kazi ya kusaidia 
jamii, tumefurahishwa na jitihada zenu,  tutafanya kazi pamoja ili 
kuhakikisha tunamuondolea mwanamke shida ya kupoteza muda mwingi 
kuhangaika kutafuta Maji  kwani kampeni yenu ya “MAMA TUA NDOO YA MAJI 
KICHWANI” ndio kampeni yetu” alisema Bi. Martha. 
Aidha,
 Mwanaharakati wa mtandao wa kijinsia Bi. Gema Akilimali, amefurahishwa 
ya kampeni ya Mama tua ndoo kichwani kwani itamsaidia mwanamke kwa kiasi
 kikubwa kushiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa nchi, kitendo 
ambacho kwa sasa hatimizi ipasavyo kutokana na kutumia muda mwingi 
kutafuta maji, pia anaamini utaongeza ufaulu mashuleni kwani badala ya 
watoto wa kike kutumia muda mwingi kutafuta Maji sasa wataweza kuokoa 
muda na kuwa kushiriki masomo ipasavyo.
 “Wanawake wanatumia muda mwingi kutafuta Maji, hivi ni saa ngapi ataleta maendeleo ya nchi? Lazima tumkwamue mama katika janga
hili ili na yeye aweze kujenga nchi yake” alisema Bi. Akilimali.
hili ili na yeye aweze kujenga nchi yake” alisema Bi. Akilimali.
Kwa
 upande wake Afisa Mtendaji mkuu wa Dawasco, Mhandisi Cyprian Luhemeja, 
amehaidi hadi kufikia Disemba 31 watahakikisha kampeni ya mama tua ndoo 
ya Maji kichwani itawafikia wakazi wengi wa Dar hususani wale walio 
katika tabaka la chini.
Aidha
 amehaidi kutoa huduma ya Majisafi na salama bure kwa wazee, walemavu na
 yatima wote ambao hawana uwezo wa kumudu gharama za kuunganisha huduma 
ya Maji, pamoja na kujenga pointi za ya kunywea Maji katika sehemu 
mbalimbali za Jiji ikiwa nipamoja na maeneo ya  stendi ya Mabasi ya 
Ubungo, Buguruni chama, Magomeni Mapipa na Kisutu stendi ya zamani.
“Mimi
 pamoja na menejimenti yangu tunaenda kumtua mama ndoo ya Maji kichwani 
mpaka kufikia mwishoni wa mwaka huu, kwani Maji yatakuwa mengi katika 
maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam pamoja na Pwani” alimalizia 
Mhandisi Luhemeja
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni