Waziri Mkuu alitaka Tamasha la Krismasi, Pasaka mikoa ya Kusini
NA MWANDISHI WETU, DODOMA
WAZIRI MKUU wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, amemuomba Mwenyekiti wa Kamati ya 
Maandalizi ya Tamasha la Pasaka Alex Msama, kupeleka huduma hiyo katika 
mikoa ya Kusini kwa sababu wanakosa huduma ya neno la Mungu.
Kampuni ya Msama huandaa Tamasha 
la Krismasi linalotarajia kufanyika Desemba mwaka huu na Pasaka 
linalotarajia kufanyika mwakani hapa nchini.
Majaliwa alisema kwa sasa tamasha
 hilo limekuwa na nguvu kubwa ya kuhakikisha inahamasisha jamii katika 
mambo mbalimbali hivyo ni wakati wa mikoa ya kusini kufaidika.
Alisema kuwa serikali yake 
imejipanga kuhakikisha kuwa kila Mtanzania ana haki ya kuona serikali 
yake inawajali na kuwapenda hivyo taasisi kama Msama Promotions, sasa 
inahitaji kujitanua na kufika mikoa mingi ya Tanzania.
Waziri Mkuu alisema kuwa amekuwa 
akifuatilia namna Tamasha la Pasaka linavyojitahidi katika kuelimisha na
 kupiga vita unyanyasaji wa kijinsia hasa wajane na yatima hivyo na 
mikoa kama Lindi na  Mtwara nayo inahitaji huduma hiyo.
“Nimefarijika sana na namna 
kampuni ya Msama Promotions chini ya Mkurugenzi wake, Alex Msama namna 
inavyofanyakazi zake katika kutoa burudani na kuelimisha jamii kwa maana
 hivyo ningependa kuwaunga mkono katika hilo,”  alisema Majaliwa.
Alisema mikoa mingi ikiwamo Lindi
 na Mtwara nayo inachangamoto nyingi hivyo wanahitaji ujumbe kama 
unatolewa katika Tamasha la Pasaka kuhakikisha kila kitu kinakwenda 
sawa.
“Kutoa misaada kwa yatima sio 
kitu kidogo lakini kubwa ni namna kampuni ya Msama Promotions chini ya 
Mkurugenzi wake Alex Msama, inavyofanyakazi zake kwa kufuata sheria 
katika hili nawapongeza lakini kubwa ni kukumbuka mikoa ya Kusini nayo 
inahitaji huduma hiyo.
Alisema kuwa kuna waimbaji wengi 
wakubwa ambao kwa sasa wamekuwa wakifanya kazi kwa ushirikiano na Msama 
lakini bado hawajawahi kufika katika mikoa ya kusini hivyo ni wakati 
wake kuhakikisha nao wananufaika na tamasha hilo.
Majaliwa amemtaka Msama kuendelea na huduma hiyo kwani serikali iko tayari kutoa msaada wa hali na mali.
Aidha Mkurugenzi wa Msama 
Promotions Alex Msama amemshukuru Waziri Mkuu Majaliwa na kusema kuwa 
atajitahidi kuboresha na kuhakikisha wananchi wote wa Tanzania 
wananufaika na huduma hiyo.
Msama amesema kuwa amesikia kilio
 cha Waziri Mkuu nakusema kuwa kamati yake iko makini na inajipanga 
kuhakikisha ombi hilo linafanyiwa kazi.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni