DR. SHEIN KUONGOZA KAMATI MAALUM YA NEC ZANZIBAR
Kwa 
mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Katibu wa Kamati 
Maalum ya NEC Zanzibar wa Idara ya Itikadi na Uenezi Mama Waride Bakari 
Jabu imesema kikao hicho kitafanyika Afisi Kuu ya CCM, iliyopo mtaa wa 
Kisiwandui, Mjini Unguja.
Taarifa
 imesema kikao hicho kawaida cha siku moja, pamoja na mambo mengine 
kitapokea na kujadili taarifa kadhaa kutoka Idara na Vitengo mbali mbali
 vya Chama hicho, ikiwemo taarifa ya hali ya kisiasa ya Zanzibar, kabla 
na baada ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Marudio wa Zanzibar.
Kikao
 hicho kilitanguliwa na kikao cha Sekretarieti ya Kamati Maalum ya NEC 
Zanzibar, kilichofanyika  April 20, mwaka huu, chini ya M/kiti wake 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg. Vuai Ali Vuai, kwa ajili ya 
kuandaa ajenda za kikao hicho.
Taarifa
  imesema kikao hicho kinafanyika kwa mujibu wa Ibara ya 114 (b) ya 
Katiba ya CCM, Toleo la mwaka 2012 na kwamba maandalizi yote 
yamekamilika.
Sgd.
(Waride B. Jabu),
Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,
Idara ya Itikadi na Uenezi – CCM,
ZANZIBAR. 22/04/2016.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni