NEC YAPONGEZWA KWA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU 2015
Na Beatrice Lyimo – MAELEZO
 Dar es Salaam
……………………………………………………………………..
Wadau mbalimbali kutoka vyama 
vya Siasa vilivyoshiriki katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Octoba 25, 
2015 wameipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa kuendesha zoezi 
hilo kwa Uwazi, Haki, Amani na kwa kuzingatia Sheria na Kanuni.
Hayo yamesemwa leo na Katibu 
Mkuu wa Chama cha NRA Bw. Hassan Kasabya alipokuwa akitoa pongezi kwa 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kutoa vyeti vya shukrani kwa washiriki hao
 katika huo kwa vyama vya siasa na wadau wengine.
Bw. Kasabya amesema kuwa Taifa 
ya Uchaguzi (NEC) iliona umuhimu wa vyama hivyo kama wadau wa uchaguzi 
na chaguzi zote hapa nchini na kuamua kutoa kutoa vyeti vya shukrani kwa
 kufanikisha uchaguzi huo.
“Vyeti hivi ni kielelezo tosha 
cha umakini wa Tume yetu na jinsi gani wamejali na kuthamini ushiriki wa
 vyama vyetu, kwani pasipo vyama vyetu hivi uchaguzi mkuu hauwezi 
kufanyika” ameongeza Katibu  Mkuu huyo.
Aidha, kwa upande wake Katibu 
Mkuu kutoka Chama cha AFP Rashid Rai ametoa wito kwa Serikali kuzidi 
kuiwezesha Tume ya Taifa ya Uchaguzi hususan uboreshwaji wa daftari la 
kudumu la wapiga kura na kuzidi kutoa elimu ya uraia kwa wapiga kura.
Mbali na hayo, Wadau hao 
wameipongeza Tume hiyo kwa mabadiliko makubwa ya kiutendaji 
yaliyofanyika katika uchaguzi mkuu uliopita kulinganisha uchaguzi wa 
mwaka 2010, 2005, 2000 na 1995.
Wadau walioshiriki kuipongeza 
NEC kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana ni pamoja na Chama cha 
National Alliance and Reconstruction (NRA), Chama cha Alliance for 
Tanzania Farmers (AFP), Chama cha United Peoples Democratic Party 
(UPDP), Chama cha UMD, Chama cha Demokrasia Makini (MAKINI) na Chama cha
 Haki na Ustawi (CHAUSTA).
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni