UHURU WA VYOMBO VYA HABARI NCHINI
…………….
Wanadamu
 wameumbwa kwa hulka na silika ya kuwa na uwezo wa kuwasiliana miongoni 
mwao, jamii wanamoishi, taifa na hata ulimwenguni ili waweze kutimiza 
nia na azma yao ya kuwasiliana.
Ili mawasiliano hayo yakamilike ni lazima yabebe ujumbe unaokusudiwa kufikishwa katika jamii.
Ujumbe
 huo ili uweze kumfikia mlengwa, ni lazima iwepo njia ya kuufikisha 
ujumbe huo kwa mlengwa ambao huwasilishwa kwa maandishi (magazeti), 
sauti (redio) na picha (TV) pamoja na mitandao ya kijamii kupitia huduma
 ya inteneti.
Vyombo
 hivyo vya habari vinahusisha wataalamu ambao kazi yao ni kuhakikisha 
jamii inapata ujumbe kwa wakati ili kuweza kujenga, kuboresha na 
kuimarisha maisha yao kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni.
Vyombo
 vya habari hakika vimekuwa ndio macho na masikio ya wananchi ili 
kufikisha ujumbe unaohusu mambo mbalimbali yanayofanyika ndani na nje ya
 nchi.
Tunapoelekea
 siku ya maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari duniani ambayo 
huadhimishwa kila mwaka Mei 2 na 3, maadhimisho hayo mwaka huu 
yataadhimishwa nchini Finland, ambapo wanahabari wote duniani wataungana
 kuwakumbuka wenzao waliofariki dunia walipokuwa wakitekeleza majukumu 
yao na kupanga mipango mipya ya namna watakavyoboresha kazi zao ziwe za 
ufanisi zaidi.
Tanzania ikiwa miongoni mwa mataifa ya dunia hii, nayo haipo nyuma katika suala la uwepo wa vyombo vya habari.
Ni 
dhahiri vyombo vya habari nchini vimekuwa kiungo muhimu katika kisaidia 
Serikali kutoa taarifa mbalimbali na ajira hatua ambayo imesaidia 
kupunguza tatizo la ajira nchini.
Ukilinganisha
 na nchi nyingine za Afrika Mashariki, Tanzania inayoongoza kwa kuwa na 
vyombo vingi vya habari, hali ambayo ni msingi wa kuajiri watu wengi 
zaidi katika tasnia hiyo.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye ambaye ndiye mwenye 
dhamana ya habari nchini anasema Serikali inaunga mkono juhudi 
zinazofanywa na vyombo vya habari nchini.
“Tulipofika
 ni pazuri ukilinganisha na tulipotoka, mengi yamefanyika hasa 
ukiangalia idadi ya vyombo vya habari nchini na uhuru wa waandishi wa 
habari wanavyoanadika na wanavyofikisha ujumbe kwa wasomaji, 
wasikilizaji na watazamaji” alisema Waziri Nape.
Aidha,
 Waziri Nape amesema kuwa bado Serikali inakusudia kuboresha mazingira 
ya waandishi wa habari ili waweze kufanya kazi zao kwa hali ya uhuru 
hasa wanapotimiza majukumu yao ya kiundishi wa habari.
Kwa 
mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambacho ni 
chombo kilichoanzishwa kisheria kusimamia sekta za mawasiliano na 
utangazaji nchini hadi sasa kuna jumla ya vituo kadhaa vya radio na 
televisheni vilivyosajiliwa.
Idadi
 ya vituo vya redio vilivyosajiliwa nchini hadi sasa ni 123 ambavyo ni 
sawa na asilimia 43.4 katika ukanda wa Afrika Mashariki huku miongoni 
mwa vituo hivyo vinamilikiwa na makampuni binafsi, taasisi na mashirirka
 ya dini, jamii na Serikali ambayo inayomiliki kituo kimoja cha TBC 
Taifa inayoendeshwa chini ya Shirika la Taifa la Utangazaji (TBC), 
nchini Kenya vipo vituo vya redio 118 sawa na asilimia 41.7, Uganda 37 
sawa na asilimia 13.1, Rwanda vituo vitatu sawa na asilimia 1.1 wakati 
Burundi ina vituo vya redio viwili ambavyo ni sawa na asilimia 0.7.
Kwa 
upande wa vituo vya televisheni, Uganda inaongoza kwa kuwa na vituo 
vingi ambavyo idadi yake ni 44 sawa na asilimia 53.6, ikifuatiwa na 
Tanzania yenye vituo 24 sawa na asilimia 29.3, Kenya vituo 10 sawa na 
asilimia 12.2, Rwanda vituo vitatu ambavyo ni sawa na asilimia 3.7 na 
Burundi ikiwa na kituo kimoja cha televisheni ambacho ni sawa na 
asilimia 1.2
Kwa 
kuzingatia maslahi ya wananchi na wamiliki wa vyombo vya habari na 
wanahabari wenyewe, TCRA imekuwa ikihimiza juu ya ufanisi wa ushindani 
na uchumi, kulinda maslahi ya walaji, kulinda uwezo wa fedha na ufanisi 
wa wagavi.
Pia 
inahimiza upatikanaji wa huduma zinazosimamiwa kisheria kwa walaji 
wakiwemo wenye kipato cha chini na walaji wa vijijini na wa pembezoni, 
kukuza mwamko, maarifa na uelewa wa jamii kuhusu sekta zinazosimamiwa 
ikiwemo kuzingatia haja ya kulinda na kuhifadhi mazingira, haki na 
wajibu wa walaji na wagavi wanaosimamiwa.
Katika
 kuonesha Tanzania inavyosimamia uhuru wa vyombo vya habari, TCRA ina 
jukumu lingine la kusimamia malalamiko na migogoro inayoweza kujitokeza 
miongoni mwa wateja wake wakiwemo wamiliki wa vyombo vya habari, 
wananchi na kupatia ufumbuzi changamoto hizo.
Aidha,
 hadi Aprili 22, 2016, Tanzania imekuwa ndio nchi inayoongoza Afrika 
Mashariki kwa kuwa na idadi kubwa ya magazeti yaliyosajiliwa ambapo 
idadi yake ni 881 licha ya magazeti na majarida mengi kusajiliwa, mengi 
huchapishwa mara chache na mengine kutokuchapishwa na kusambazwa baada 
ya kusajiliwa.
Kwa 
idadi ya magazeti nchi za Uganda, Rwanda na Burundi yapo magazeti matano
 yanayotumika katika nchi hizo wakati Kenya ina magazeti saba ambayo 
husomwa na kufikisha ujumbe kwa walengwa katika mataifa hayo.
Wingi
 huo wa vyombo vya habari nchini imekuwa ishara njema ya kujali uhuru wa
 kuanzishwa kwa vyombo vya habari kwa makampuni binafsi, taasisi na 
mashirika ya dini pamoja na jamii mbalimbali ili kuweza kuwa ndio namna 
yao ya kupata taarifa.  
Katika
 ulimwengu wa leo, uhuru wa habari ni suala la msingi na lina umuhimu 
mkubwa katika kutekeleza haki za binadamu katika kutafuta, kupata, 
kupokea na kutoa habari ambazo ni muhimu kwa nchi katika kujiletea 
maendeleo endelevu.
Kauli
 mbiu ya maadhimisho hayo mwaka huu inawahimiza wanahabari na watu wote 
kutambua “Kupata Habari ni Uhuru wa Kimsingi: Hii ni haki yako!” 
ikilinganishwa na kauli mbiu ya mwaka uliyopita ambayo ilisema “Achia 
uwandishi habari ustawi! Kuelekea upashaji habari bora, usawa wa jinsia 
na usalama wa vyombo vya habari katika enzi ya dijitali”.
Kwa 
mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Shirika la 
Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Aprili 8, 2016 
imebainisha kuwa katika maadhimisho ya Siku ya vyombo vya habari duniani
 mwaka huu, mwandishi wa habari za uchunguzi kutoka Azerbaijan Khadija 
Ismayilova amechaguliwa kupokea tuzo ya uandishi wa habari za uchunguzi 
ijulikanayo “Guillermo Cano” inayotolewa na Shirika hilo.
Tuzo 
hiyo ina thamani ya Dola za Kimarekani 25,000, na imepoewa jina hilo kwa
 heshima ya Guillermo Cano Isaza, mwandishi wa habari wa Colombia 
aliyefariki Desemba 17, 1986 akiwa kazini.
Jukumu
 la kuenzi na kutoa tuzo ya heshima kwa waandishi wa habari duniani 
linafadhiliwa na taasisi ya Cano Foundation kutoka nchini Colombia na 
Helsingin Sanomat Foundation kutoka nchini Finland.
Msaidizi
 wa Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano na Habari UNESCO Frank La Rue anasema
 “Uhuru wa vyombo vya habari ni muhimu kwa taarifa muhimu na uwazi ni 
ambao ni mahitaji ya jamii ya kidemokrasia. Lakini leo tunaona ongezeko 
la ghasia na vitisho dhidi ya waandishi ambayo mimi napendekeza nchi 
zote duniani kuanzisha utaratibu wa habari na ulinzi kwa ajili ya 
usalama wa waandishi wa habari”
Moja 
ya changamoto za kuweka utaratibu wa usalama wa waandishi wa habari ni 
idadi ndogo ya mifano ya taratibu zilizopo ambayo inaweza kuwa somo ili 
wengine waweze kujifunza kutokana na taratibu zilizopo.
Masuala
 muhimu ya kuzingatiwa wakati wa kuanzisha utaratibu huo ni pamoja na 
kuwepo kwa makundi matatu ambayo ni wigo wa utaratibu, ushirikishwaji wa
 wadau muhimu pamoja na taasisi kubuni  na kutathmini hatua ambayo 
itasaidia kufikia malengo ya kumlinda mwandishi wa habari.
Akizungumzia
 maandalizi ya maadhimisho kitaifa ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari
 nchini ambayo yanafanikia jijini Mwanza Mei 2 na 3, mwaka huu, 
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya maadhimisho hayo Andrew Marawiti 
amesema kuwa yanaendelea vizuri kulingana na ratiba ilivyopangwa.
Katika
 maadhimisho hayo, Marawiti amesema kuwa Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa 
Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Othman Chande ambapo wakati
 wa ufunguzi wa maadhimisho hayo mada mbalimbali zitawasilishwa na 
watoaKuhusu ratiba ya siku mbili za maadhimisho hayo, Marawiti amesema 
kuwa zitawasilishwa zikiandamana na majadiliano kwa washiriki wote.
Miongoni
 mwa washiriki wanaotarajiwa kuwepo katika maadhimisho hayo ni wadau 
mbalimbali wa habari wakiwemo viongozi wa Serikali, Mabalozi 
wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini, wawakilishi wa Mashirika ya 
Kimataifa, wamiliki wa vyombo vya habari, waandishi wa habari na 
wananchi.
Kulingana
 na takwimu zilizopo, mwandishi wa habari mkongwe nchini, Mzee Willie 
Mbunga amesema kuwa Tanzania ina vyombo vingi vya habari ikilinganishwa 
na hali ilivyokuwa miaka ya nyuma ambapo kulikuwa vyombo vichache vya 
habari ambavyo ni redio Tanzania Dar es salaam, Tanganyika Standard, 
Mambo Leo, Uhuru, Mzalendo na Ngurumo.
Aidha,
 amesema kuwa changamoto ya baadhi ya watu kujisahau na kuweka pembeni 
maadili ya uandishi wa habari ni suala ambalo si la kufumbiwa macho, ni 
vema litiliwe maanani ili kukiokoa kizazi cha sasa na kijacho katika 
kujenga jamii inayojali na kusimamia maadili ya taaluma na ya jamii.
Katika
 upashanaji habari, dunia sasa imekuwa sawa na kijiji hasa katika 
kipindi hiki cha sayansi na teknolojia ambapo mawasiliano ndio imekuwa 
nguzo ya kila kitu.
Awali
 makala haya yameonesha kuwa ujumbe katika jamiiulifikishwa kwa njia ya 
redio, magazeti na TV, zaidi ya vyombo hivyo, mitandao ya kijamii kwa 
sasa imekuwa nguzo mahiri na vyanzo vikuu vya habari kwa waandishi wa 
habari na wananchi.
Miongoni
 mwa mitandao hiyo ya kijamii ni pamoja na blog ya Serikali, Michuzi, 
fullshangwe, bayana, milardayo, mwamba wa habari, businessmagnetblogs, 
mpekuzi, moh Dewji na mitandao mingine.
Mwandishi
 wa habari Majid Mjengwa ambaye pia ni mwanzilishi na mmiliki wa blog ya
 mjengwa anasema “Mitandao ya kijamii imekuwa ni eneo la upashanaji 
habari linalofanya kazi kama vyombo vingine vya habari”.
Ili 
kufikisha ujumbe kwa jamii, Mjengwa amesema kuwa watu wote wanaofanya 
kazi katika mitandao ya kijamii wanapaswa kufuata maadili ya taaluma ya 
habari pamoja na sheria na taratibu za nchi husika ili kuondoa mgongano 
wa maslahi katika kufikisha ujumbe kwa jamii.
Ni 
dhahiri haki na wajibu ni vitu ambavyo haviachani, hivyo ni jukumu la 
kila mdau wa habari nchini wakiwemo Serikali, waandishi wa habari, 
wamiliki wa vyombo vya habari na wananchi kuzingatia sheria, kanuni, 
taratibu pamoja na maadili ya jamii.
Hatua
 hiyo itasaidia kuimarisha na kuhakikisha wadau hao wanakuwa sehemu ya 
kujenga uhuru wa vyombo vya habari ambavyo vitakuwa chachu ya kujenga 
taifa imara lenye uchumi bora kwa manufaa ya Watanzania ifikapo mwaka 
2025. 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni