Jumatatu, 25 Aprili 2016


UKWELI UKO WAPI KUHUSU KUSITISHWA KWA MATIBABU YA WAGONJWA WA SELIMUNDU (SICKE CELL) ?


Yasmini Razack wanaharakati wa Ugonjwa wa Selimundu ( Sicke Cell ).

Kwa mujibu wa Muongozo wa Wizara ya Afya Sikoseli inaingia katika orodha ya magonjwa yanayotakiwa kutibiwa bure, na imekuwa ikifanyika hivyo lakini kuanzia tarehe 21 April mwaka huu, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa walezi wenye watoto wanaugua ugonjwa wa Sikoseli kuwa wamekuwa wakitozwa pesa na matibabu ya ugonjwa huo yamesitishwa katika hospitali ya Muhimbili.


 


Kufuatia hayo Mwanaharakati wa ugonjwa wa Sikoseli Yasmini Razaak amelaani kitendo hicho alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo na kuongeza kuwa wagonjwa hao wameandikiwa barua na kupelekwa hospitali ambazo hazina wataalamu wa ugonjwa huo ikwemo hospitali ya Amana na Temeke, hivyo wamemuomba Rais Magufuli kuibeba agenda ya ugonjwa wa Sikoseli kama Rais Kikwete alivyoibeba agenda ya ugonjwa wa Malaria na kuja na kampeni ya Zinduka.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Lawrence Msemu  ( Kulia), akizungumza na waandishi kuhusiana na ufafanuzi wa matibabu ya wagonjwa wa Selimundu ( Sicke cell)  wa habari jijini Dar es salaam jana . Picha zote na Raymond Urio

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya  Taifa ya Muhimbili Lawrance Msemu amekanusha kusitishwa kwa huduma za matibabu na kutozwa pesa kwa wagonjwa wa sikoseli huku akieleza kuwa kilicho sitishwa ni utafiti dhidi ya ugojwa huo hivyo wananchi wataendelea na huduma hizo kama kawaida.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ameeleza kuwa hospitali yake imeamua kufanya utaratibu kutokana na kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa waliopo hospitalini hapo (zaidi ya 6000), hivyo wagonjwa hao watapangiwa hospitali zingine na endapo itashindikana kupata tiba stahiki watapewa rufaa kwenda kwenye Hospitali hiyo ya Muhimbili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni