TANAPA KUZINDUA KAMPENI YA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO
Picha zote na Mahmoud Ahmad Arusha
…………………………………………………………..
Na Mahmoud Ahmad,Arusha.
Shirika
 la Hifadhi za Taifa TANAPA limejipanga kuzindua kampeni ya kitaifa ya 
 kufanya usafi mlima Kilimanjaro ambao unakusanya mapato ya shilingi 
bilioni 60 kwa mwaka na kuajiri Watanzania laki 3.
Meneja
 Mawasiliano wa TANAPA Pascal Shelutete akizungumza na Waandishi wa 
Habari amesema kuwa kampeni hiyo itasaidia kuboresha mazingira safi ya 
Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro na kuinusuru na uchafuzi wa mazingira wa 
kidunia (Global warming), Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), 
inatarajia kuzindua kampeni ya usafi wa mlima Kilimanjaro kesho ambayo 
itadumu kwa siku kumi.
“Tumeamua
 kufanya usafi katika mlima huo ikiwa ni jitihada za kuunga mkono juhudi
 za Rais John Pombe Magufuli katika kuweka mazingira katika hali ya 
usafi hususan hifadhi za taifa” Alisema Shelutete
Katibu
 Mkuu wa Chama cha Mawakala wa Utalii Sirili Akko amesema kuwa mashirika
 binafsi yaliyoko kwenye sekta ya utalii hayana budi kushiriki katika 
kufanya usafi katika mlima huo wa kwanza kwa urefu barani Afrika na 
wapili duniani.
Pia 
ameitaka serikali kusimamia maagizo ya Ofisi Makamu wa Raisi Mazingira 
kwa kupiga marufuku ya matumizi plastiki katika hifadhi za taifa ili 
kuepuka kuchafua mazingira.
Mdau 
wa Masuala ya Utalii ambaye ni Afisa Masoko wa Hoteli ya Kibo Palace 
Jenipher Swai amesema kuwa wameungana na Tanapa kufanya usafi kwa kutoa 
vifaa vya kufanyia usafi pamoja na kushiriki kupanda mlima huo katika 
madhimisho ya miaka kumi ya kuanzishwa kwa hoteli hiyo.
Jumla
 ya Watalii 50000 hutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro na 
kuchangia shilingi bilioni 60,kampeni ya kufanya usafi ya muda wa siku 
10 itanza kesho ikiwashirikisha wapagazi,waongoza watalii na wadau wa 
utalii ,kuhakikisha hali ya usafi katika hifadhi zetu zitasaidia kuvutia
 watalii zaidi.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni