Serikali yaipongeza Quality Group kwa kuanzisha Kituo cha Urithi wa Utamaduni Tanzania (TCCH)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (mwenye suti 
nyeusi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Kituo 
cha Urithi wa Utamaduni Tanzania (TCCH)   wakati wa hafla ya uzinduzi wa
 kituo hicho leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Frank Shija, WHUSM
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akikata utepe 
kuashiria uzinduzi rasmi wa Kituo cha Urithi wa Utamaduni Tanzania 
(TCCH) kilichopo katika jengo la Qaulity Center leo jijini Dar es 
Salaam.Kituo hicho kinamilikiwa na Kampuni ya Quality Group Limited.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (mwenye suti 
nyeusi) akitembelea bidhaa mbalimbali za Sanaa na Utamaduni mara baada 
ya kuzindua rasmi Kituo cha Urithi wa Utamaduni Tanzania (TCCH) 
kilichopo katika jengo la Quality Center leo jijini Dar es Salaam. Kituo
 hicho kinamilikiwa na Kampuni ya Quality Group Limited.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (mwenye suti 
nyeusi) akitembelea bidhaa mbalimbali za Sanaa na Utamaduni mara baada 
ya kuzindua rasmi Kituo cha Urithi wa Utamaduni Tanzania (TCCH) 
kilichopo katika jengo la Quality Center leo jijini Dar es Salaam. Kituo
 hicho kinamilikiwa na Kampuni ya Quality Group Limited.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akifurahia jambo 
na Mke wa Rais wa kwanza wa Zanzibar Mama Fatma Karume walipokutaka 
wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Urithi wa Utamaduni Tanzania 
(TCCH) kilichopo katika jengo la Quality Center leo jijini Dar es 
Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akipokea zawadi 
ya picha kutoka kwa uongozi wa Kituo cha Urithi wa Utamaduni Tanzania 
(TCCH) kilichopo katika jengo la Quality Center leo jijini Dar es 
Salaam.Kituo hicho kinamilikiwa na Kampuni ya Quality Group 
Limited.Kituo hicho ni duka ambalo linauza bidhaa za sanaa na utamaduni 
kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akipokea zawadi 
ya fimbo maarufu kwa jina la Rungu la Kimasai kutoka kwa Mshauri wa 
masuala ya bidhaa za sanaa na utamaduni Bibi. Caroline Kessy wakati wa 
hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Urithi wa Utamaduni Tanzania (TCCH) 
kilichopo katika jengo la Quality Center leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akifurahia jambo 
na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Quality Group Ltd ambao ni wamiliki
 wa Kituo cha Urithi wa Utamaduni Tanzania (TCCH) Bw. Arif Sheikh  
wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kituo jijini Dar es Salaam
………………………………………………………………………………………….
Na: Frank Shija;WHUSM
Serikali yaipongeza Kampuni ya 
Quality Group ltd kwa hatua yake ya kuanzia Kituo cha Uridhi wa 
Utamaduni Tanzania (TCCH) ambapo kupitia kituo hicho bidhaa mbalimbali 
za Sanaa na Utamaduni zinauzwa ndani na nje ya nchi.
Akitoa pongezi hizo kwa niaba ya 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Katibu Mkuu wa Wizara 
hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel amesema kuwa kuanzishwa kwa kituo 
hicho kutaiuza nchi, utamaduni wetu, kazi za sanaa na kuongeza ajira 
miongoni mwa jamii yetu.
Aidha Profesa Gabriel amesema 
kuwa Serikali itaendelea kuwa pamoja nao na kushirikiana na wadau wote 
ili kuhakikisha kwamba wanafikia mafanikio na malengo waliyojiwekea 
katika uwekezaji huo.
Aliongeza kuwa ni vyema sasa 
Kituo hiko kikafikiria kuanzisha vituo vidogo vidogo katika kanda ili 
kurahishisha upatikanaji wa bidhaa hizo na kusaidi wasanii walioko 
pembezoni wapate soko la bidhaa zao kwa Serikali ingependa kuona zaidi 
wasanii wa ndani wakinufaika na uwepo wa Kituo hicho.
Pia ameuomba uongozi wa Kituo 
hicho kuangalia namna ya kushirikiana na Serikali kupitia Wizara ya 
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuwajengea uwezo wasanii hili 
kujenga soko la uhakika,ubora na viwango vya hali ya juu.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji 
Mkuu wa Quality Group Limited Bw. Arif Sheikh ameishukuru Serikali kwa 
kuonyesha ushirikiano kna imekuwa faraja kubwa kwao kwa kiongozi wa 
ngazi ya juu Serikalini kukubali kuja kuzindua Kituo chao.
Sheikh amesema kuwa kuanzishwa 
kwa Kituo hicho kumelenga kukuza sanaa na utamaduni wa Mtanzania kwakuwa
 kinahusika na uuzaji wa bidhaa za sanaa na utamaduni tu, hivyo wasanii 
wanayo fursa ya kujipatia kipato kwa kukiuzia Kituo kazi zao.
Hata hivyo Sheikh alisema kuwa 
kutokana na ushauri uliotolewa Kampuni yao ipo tayari kutoa ushirikiano 
zaidi kwa Serikali pindi watakapohitajika kufanya hivyo ikiwemoi sualaua
 la kuwajengea uwezo wasanii wa kazi za mikono.
Kituo cha Urithi wa Utamaduni Tanzaia ambacho kwa kingereza kinaitwa  Tanzania Center for Cutural Heritage (TCCH) kipo katika jengo la Quality Center, kinamilikiwa na Kampuni ya Qaulity Group Limited ya jijini Dar es Salaam.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni