MJANE WA MWALIMU BABA WA TAIFA MAMA MARIA ATEMBELEA DARAJA LA NYERERE KIGAMBONI LEO
Mama
Maria Nyerere, Mjane wa Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akiwa na
mwanae Mhe. Makongoro Nyerere na msaidizi wake akifurahia mandhari
wakati walipotembelea Daraja la Nyerere Kigamboni jijini Dar es salaam.
Mama Maria, ambae hakujali mvua kubwa iliyokuwa inanyesha, alionekana
mwenye furaha kufika darajani hapo kwani ndoto ya miaka mingi
iliyoanzishwa na hayati mumewe imetimia. Pia alimshukuru sana Dkt John
Pombe Joseph Magufuli kwa kuagiza daraja lipewe jina la Mwalimu na siyo
yeye, jambo ambalo amesema limemfariji sana kwani vizazi vya sasa na
nvijavyo vitamkumbuka mwasisi wa Taifa..
PICHA NA IKULU
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni