NA RAYMOND URIO, Dar
KATIKA Kuhakikisha kuwa Shirika la Posta Tanzania
linashiriki na kuchangia kikamilifu jitihada za serikali ya awamu ya Tano za
kuleta maendeleo ya haraka kwa mwanachi, shirika hili kuanzia jumanne litaanza
kutoa huduma ya kupokea barua, nyaraka, taarifa na bidhaa mbalimbali kutoka
ndani ya nje ya nchi na kuzifikisha nyumbani.
Kaimu Poster Master Mkuu wa shirika la Posta Tanzania, Fortunatus Kapinga akizungumza jana na waandishi wa habari jana, jijini Dar es Salaam ( hawapo pichani), kwenye ukumbi za Ofisi hizo, kuhusiana na shirika hilo kufungua huduma ya "Posta Mlangoni" huduma hiyo itazinduliwa Aprill 5 mwaka huu, kushoto ni Meneja mkuu wa rasilimali za shirika la Posta Tanzania, James Sando.
Huduma hii inayojulikana kama “Posta Mlangoni”
itaanza katika baadhi ya kata za hapa jijini Dar es Salaam, Arusha na Dodoma
inaboresha ile iliyokuwapo tangu enzi za ukoloni ya masanduku yaliyoko Ofisini
za Posta ambayo mtumiwa nanlazimika kufuata yeye mwenyewe barua, vifurushi,
taarifa au bidhaa aluizotumiwa kupitia Ofisi za Posta.
Serikali kupitia Ofisi ya Raisi ( TAMISEMI ) tayari
imeweka miundombinu hiyo katika kata 8 za jiji la Arusha, kata 8 za manispaa ya
Dodoma na kata 32 kwa jiji la Dar es Salaam. Miundombinu hiyo ni mitaa kuwekewa
nguzo za kuonesha jina la mtaaa, nyumba zilizopo kwenye mtaa huo kuwekewa
nambari za kiposta.
Baada ya kuznzisha huduma hii jumanne ijayo hapa
Dar es Salaam, Arusha na Dodoma ndani ya kipindi hiki cha mwaka 2015 na 2016, awamu
ya pili itakayotekelezwa katika kipindi cha mwaka 2016 na 2017 itahusu mikoa ya
Shinyanga, Mwanza, Tanga, Morogoro, Kagera, Mtwara, Lindi, Shinyanga, Pwani, Manyara,
Simiyu na Geita pamoja na Tanznia visiwani( Unguja na Pemba).
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar
es Salaam, kwenye ukumbi wa ofisi hizo, Kaimu Posta Masta Mkuu wa Shirika la
Posta nchini, Fortunatus Kapinga, alisema kuwa Huduma hii ni msukumo mpya wa
ndani ya shirika wa kuhakikisha kuwa yanakuweko mabadiliko katika uendeshaji na
utoaji wa huduma za mawasiliano ya Posta nchini ili kukabiliana na kasi ya
teknolojia, kukidhi mahitaji ya soko, kuboresha maisha ya wananchi na kufanya
Tanzania kuwa kinara wa hudumabora za mawasiliano.
“Kupitia huduma hii yamefanyika mabadiliko ya
mifumo ya uendeshaji katika baadhi ya Ofisi ili kuhakikisha kuwa uchambuzi wa
barua unafanyika kwa uhakika zaidi, anwanwi zitatambuliwa ili kuongeza kasi ya
kusafirisha na kusambaza barua,
“Aidha kipindi hiki cha mpito ambapo hapo baadae
ndani ya kipindi cha miaka mitatu shirika litasambaza huduma ya “Posta Mlangoni”
nchi nzima,” alisema Kapinga.
Hata hivyo Kapinga alisema kuwa huduma hii
imeanzishwa sasa kutokana na jitihada zax serikali kuweka miundombinu ya Anwani
za Makazi na Postikodi kupitia wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nchini
( TCRA) na wadau wengine.
“ Miundombinu hii ni pamoja na barabara na Mtaa
kuperwa majina yanayosomeka kwenye nguzo zilizosimikwa pamoja nanyumba kupewa
majina yanasomeka kwenye nguzo zilizo
simikwa na nyumba zilizo pewa namba,” alisema Kapinga.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni