Ijumaa, 1 Aprili 2016



POLISI: UHAKIKI WA SILAHA KUENDELEA MIKOA YOTE,


BAADA ya wakazi ya jiji la Dar es Salaam kuanza usajili wa kuhakiki Silaha Jeshi la Polisi nchini limetoa miezi mitatu kwa mikoa mengine nchini  kwa wamiliki wote kufanya uhakiki wa silaha la sivyo sheria itachukua mkondo wake.

Akizungumza jijini hapa jana, Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo, Nsato Malijani, alisema wananchi wamejitokeza kusajili na kuhakiki silaha zao ambapo rais Dk John Magufuli alikuwa wa kwanza kufanya hivyo na kwamba hali ya uhalifu wa makundi bado ipo, kuwataka wananchi wananchi kutoa taarifa endapo wakibainika makundi wanaojihusisha na uhalifu na yenye silaha. 

 

Kamishina wa oparesheni na mafunzo wa makao mkuu ya jeshi la polisi, Nsato Mssanzya akizungumza na waandishi wa habari ( hawapo pichani), kuhusiana na jeshi la polisi nchini kutoa linatoa muda wa miezi mitatau kwa ajili ya kukamilisha zoezi la kuhakiki silaha  kwa nchi nzima.

Kamishina Malijani alisema uamuzi wa kutoa muda huo katika mikoa iliyobaki ni kutokana na kwamba awali walitoa  muda mchache hali ambayo ilisababisha msongamano katika vituo vya polisi.

 Alisema hali hiyo imechangia kwa kiwango kikubwa mchakato huo kutofanyika kwa haraka jambo ambalo limekuwa kero na kuleta mkanganyiko kwa wamiliki pamoja na kupunguza hali ya usalama katika vituo vya polisi.

 "Hivyo ni imani yangu kwamba muda huo utatosha kwani utatoa nafasi kwa watu ambao hawajalipia ada ya umiliki wa silaha zao kulipia na kusajili pamoja na kuondoa msongamano wa watu katika vituo vya polisi waliojitokeza kwaajili ya kusajili silaha zao," alisema.

Alisema jeshi hilo halikuweka wazi idadi kamili ya sialaha ambazo hazikulipiwa na kiwango chake na kuweka wazi kuwa jambo hilo litaelezwa mara baada ya kukamilika kwa mchakato huo na kukusanya taarifa kutoka katika mikoa yote nchini.

Alisema hali ondoa msongamano wa watu katika vituo vya polisi waliojitokeza kwaajili ya kusajili silaha zao," alisema.

Akizungumzia uhalifu na ukamataji wa silaha,alisema hivi karibuni jeshi hilo limefanikiwa kukamata watu katika maeneo mbalimbali wanaojihusisha na uhalifu wa kimakundi ambao bado wanaendelea kufanyiwa uchunguzi.

"Watu hawa wamekamatwa Mafia, jeshi linaendelea kuwafanyia uchunguzi ili tuweze kupata taarifa mbalimbali na kuweza kuwatia

nguvuni wengine ili tutokomeze kabisa suala la uhalifu nchini," alisema

Alisema  wanaendelea kufanya msako katika maeneo yote nchini kuhakikisha vikundi hivyo vinadhibitiwa na kutoa rai kwa wananchi kuongeza ushirikiano ili uwakamata watu hao.

"Jeshi kama jeshi pekeake haliwezi likakakamata wahalifu wote bila kupata ushirikiano wa wananchi kwani wengi wao wapo miongoni mwao hivyo wananafasi kubwa ya kuwaona na kutoa taarifa ili waweze kukamatwa," alisema Malijani.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni