Jumatatu, 4 Aprili 2016

  
NA RAYMOND URIO, Dar
Mshauri wa benchi la ufundi la Taifa Stars ambaye pia ni Kocha wa JKT Ruvu, Abdallah Kibadeni, ametangaza kuwa amepanga kustaafu kufundisha soka hivi karibuni.
Kocha Kibadeni ambaye alicheza kwa mafanikio makubwa ndani ya Simba, Majimaji pamoja na Taifa Stars, amesema kuwa kwa sasa hataki presha ya timu, hivyo anataka apumzike.
Kibadeni amesema kama mchango ametoa wa kutosha katika timu mbalimbali hivyo sasa ni muda wake wa kupumzika.
“imefika kipindi na wakati wa kutulia na kuacha akili kutulia, unajua hizi timu zina presha sana na ukiangalia umri umeenda nimeona ni bora nipumzike.

“Hivi karibuni nitatangaza kuachana na ukocha wa hizi timu za wakubwa nitadili na kituo changu tu cha Kibadeni Sports Academy (Kisa), najua huku hawa watoto pamoja na timu kuwa siyo ya ushindani sitapata presha,” alisema Kibadeni.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni