Ijumaa, 29 Aprili 2016

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA MKUTANO WA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI KATIKA NCHI ZA UKANDA WA MASHARIKI NA KUSUNI MWA AFRIKA

M1 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua mkutano kuhusu kuwezesha wanawake kiuchumi katika nchi za Ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Afrika. Mkutano huo umeandaliwa na Jopo la Ngazi ya Juu la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon alilolituewa Mwanzoni mwa huu, kusaidia kufanya uchambuzi na kutoa mapendekezo ya namna ya kuchagiza kasi ya kuwezesha wanawake kiuchumi ifikapo 2030. Umefanyika Leo April 29,2016 Hyatt Hotel Dar es salaam.
M2 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Jopo la ngazi ya Juu la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa la kuwezesha wanawake kiuchumi Baada ya kufungua mkutano kuhusu kuwezesha wanawake kiuchumi katika nchi za Ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Afrika. Mkutano huo unazungumzia kuhusu kusaidia kufanya uchambuzi na kutoa mapendekezo ya namna ya kuchagiza kasi ya kuwezesha wanawake kiuchumi ifikapo 2030. Umefanyika Leo April 29,2016.
(Picha na OMR

MKUTANO WA WATAALAM WA UTHAMINI WA KUPITIA VIWANGO ELEKEZI VYA BEI YA SOKO LA ARDHI NCHINI 2016

R1 
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Yamungu Kayandabila pamoja na Kaimu Mthamini Mkuu wa Serikali Bi. Evelyin Mugashwa wakifuatilia taarifa ya viwango elekezi vya bei ya soko la Ardhi nchini katika mkutano na wataalam wa Uthamini Aprili 29, 2016.
R2 
Watalaam wa uthamini wa Serikali, Mashirika ya Umma na binafsi wakijadili taarifa ya viwango elekezi vya bei ya soko la Ardhi nchini iliyowasilishwa kwao na ofisi ya mthamini mkuu wa Serikali Aprili 29, 2016.

SHIRIKA LA UMEME TANZANIA TANESCO LAZINDUA "TANESCO UMEME"

By Newsroom on April 29, 2016 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  Mhandisi Felchesmi Mramba (kulia) akizungumza na Waandishi,viongozi wa Tanesco Dar es Salaam jana wakati wa Uzinduzi wa ‘Tanesco Huduma’ zilizoboreshwa kwa wananchi ,wateja wanaotumia simu za mkononi za kisasa katika mfumo uliotengenezwa  COSTECH.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  Mhandisi Felchesmi Mramba (katikati) akizungumza.Wengine  kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH),Hassan Mshinda na Ofisa Mtendaji Mkuu wa DTBi,George Mulamula.
 kiongozi wa Tanesco akizungumza.
 Wataalamu wa COSTECH wakipangalia mtandao.
 Maofisa wa Tanesco wakijadiliana jambo.
 Mtaalamu wa Mtandao COSTECH,Godfrey Magila akizungumza na kufafanua.
 Wataalamu wa Mtandao wa COSTECH
Viongozi wa Tanesco na Tume ya sayansi na Teknolojia COSTECH wakifurahia jambo.
 
Kwa Ufupi.
Tanesco imezindua ‘Tanesco Huduma’ Itakayoboresha huduma kwa  wananchi, kuwasilisha Taarifa kwa kutumia simu za mkononi za kisasa kwa mtu binafsi au kundi katika mitaa wanayohishi.Kutakuwa na mfumo utakaokujulisha mambo mbalimbali ya Shirika hilo,Katika majaribio yameanza kwenye mkoa wa tanesco wa Kinondoni.

Dkt. John Pombe Magufuli alitaka Jeshi la Polisi nchini na Ofisi ya Mwendesha Mashitaka kujirekebisha kwa kutekeleza wajibu wao kwa uzalendo

JA3Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Makamanda wa Polisi, Wanasheria wa Serikali,  Wafawidhi wa Mikoa na Wakuu wa upelelezi wa Mikoa na Vikosi kabla ya kufungua rasmi Kikao kazi cha Makamanda hao wa Polisi katika Ukumbi wa Dodoma Convention Center
…………………………………………………………………………………………
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amelitaka Jeshi la Polisi nchini na Ofisi ya Mwendesha Mashitaka kujirekebisha kwa kutekeleza wajibu wao huku wakitanguliza maslahi ya taifa.
Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo tarehe 29 Aprili, 2016 wakati akifungua kikao cha kazi cha Makamanda wa polisi wa mikoa, Mawakili wafawidhi wa serikali  wa Mikoa na Wakuu wa upelelezi wa Mikoa na Vikosi, kinachofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa Mikutano wa Dodoma uliopo katika eneo la Tambukareli Mjini Dodoma.
Awali kabla ya kutoa hotuba yake Rais Magufuli aliwapa nafasi Makamanda na Mawakili Wafawidhi hao kutoa maoni yao juu ya changamoto zinazowakabili katika kutekeleza wajibu wa kufanya upepelezi na kuendesha mashitaka, hususani kujua sababu za kuchelewesha kesi za makosa ya jinai, ambapo wamedai ufinyu wa bajeti ndio sababu kubwa ya kucheleweshwa kwa kesi za hizo.
Kufuatia kutajwa kwa changamoto hiyo Rais Magufuli ameahidi kuhakikisha anawatafutia fedha kwa ajili ya kukabiliana nazo, lakini ametaka fedha zitakazotafutwa zitumike vizuri kwa kuwa taarifa zinaonesha Jeshi la Polisi limekuwa likihusishwa na matumizi mabaya ya fedha hali inayoongeza ukubwa wa matatizo yanayokwamisha utendaji wake wa kazi.
Ametolea mfano wa taarifa za matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa kwa ajili ya kununulia vifaa na sare za askari, ama mikataba yenye mashaka inayotiwa saini kati ya Polisi na wawekezaji kuwa ni baadhi ya mambo yanayoongeza hali ngumu ya utendaji kazi kwa jeshi hilo.
“Oysterbay pale ni eneo ambalo ni very prime, kila mmoja anajua, mmeingia kwenye mikataba mnayoijua nyinyi, akapewa mtu anawajengea pale, sifahamu kama majengo hayo yanafaa. Palikuwa na ubaya gani eneo la Oysterbay likawa na hati, mkaitumia hiyo hati kwenda kukopa benki na kujenga nyumba hata za ghorofa 20 pale, mkaweka investment  na Polisi wenu wakakaa pale. Nimesema lazima nizungumze kwa uwazi, nisiposema kwa uwazi nitajisikia vibaya nikimaliza mkutano huu, nataka muelewe na muelewe ukweli direction  ninayoitaka mimi” Amesema Rais Magufuli
Aidha, Rais Magufuli ameitaka Ofisi ya mwendesha Mashitaka wa Serikali kujipanga kufanya kazi kwa ufanisi na ameelezea kusikitishwa kwake na vitendo vya serikali kushindwa katika kesi nyingi mahakamani licha ya kuwa na wanasheria mahiri.
“Niwaombe mawakili na polisi wanaohusika na upelelezi mtangulize maslai ya nchi mbele, kwa sababu kumekuwa na usemi kwa baadhi ya wapelelezi na mawakili wachache, nasema wachache, panapokuwa na kesi inayohusiana na pesa pesa, wana misemo yao wanasema dili limepatikana, na saa nyingine kesi inapopelekwa mahakamani wana-collude Mawakili wa serikali na mawakili wanaomtetea  mhalifu, na wanapo-collude siku zote serikali inashindwa. Unapoona hali hiyo ya kila siku serikali inashindwa, halafu siku hiyo unataka serikali ikuwezeshe, kwa vyovyote serikali inapata kigugumizi” amesisitiza Rais Magufuli.
Dkt. Magufuli pia amelitaka Jeshi la Polisi kujiepusha na kashfa ambazo zimekuwa zikisemwa dhidi yake, ikiwemo maafisa wa Polisi kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya na kuazimisha silaha kwa wahalifu wa ujambazi.
Hata hivyo Rais Magufuli amelipongeza Jeshi la Polisi na ofisi ya Mkurugenzi wa  Mashitaka kwa kazi kubwa wanayoifanya na ametaka apelekewe mpango wa mahitaji yao ili atafute namna ya kuimarisha vyombo hivyo.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
29 Aprili, 2016

Tafrija ya mchapalo baada ya Tigo na samaki samaki kuingia Ubia yafana

Wadau wakifurahi usiku wa jana wakati wa hafla ya mchapalo baada ya Tigo na mgahawa wa samaki samaki kuingia Ubia ambapo pande hizo mbili zimekubaliana kufanya kazi pamoja  kwa kuleta  bidhaa/huduma zao kwa wateja wa kila mmoja.
 
Vinywaji murua kabisa 
 
Warembo wa Tigo wakiwa tayari kuhudumia wateja na wageni waalikwa wote 
 
Ulinzi ukiimarihwa kwa  wageni waalikwa na  wateja wote
 
Mtaalamu wa mitandao ya kijamii kutoka Tigo Samira Baamar (kulia ) akiwa katika pozi na wafanyakazi wenzake Ummy Mtiro na Natasha 
 
Mhudumu wa Samaki akitabasamu na kuwakaribisha wageni waalikwa 
 
Blogger na mdau wa mitandao ya kijamii John Kiandika akiwa katika pozi na mkewe wakati wa hafla usiku wa jana 
 
Mmoja ya wageni waalikwa akipata maelezo kuhusu huduma ya Tigo 4g kutoka kwa mhudumu
 
Mkurugenzi wa migahawa ya Samaki Samaki, Bw. Carlos Bastos
 
Meneja wa Huduma za Masoko wa Tigo Oliver Prentout akifurahi jambo na wafanyazi wa tigo wakati wa hafla hii
 
Watangazaji maaruf wa kituo cha Clouds tv Hudson Kamoga na Sam sasali wakiwa pamoja kupata maelekezo kuhusa huduma ya intanet ya kasi ya Tigo 4G kwenye hafla hiyo.
 
 
Mhudumu akiandaa chakula 
 
Wahudumu wa samaki samaki wakiwa katika pozi 
 
wadau wakiwa katika pozi 
 
Taswira ukumbini 
 
Mdau John kiandika na mkewe wakipata maelezo zaidi kuhusu huduma ya Tigo 4g 
wadau wakiwa kwenye picha ya pamoja 
 
 
 Tigo ni kampuni ya mawasiliano ya simu za mikononi yenye ubunifu mkubwa nchini Tanzania,ikijulikana kama“nembo ya maisha ya kidijitale yanayojitosheleza”.
 ………………………………………………………………………………………………………
Inatoa huduma mbalimbali kuanzia huduma ya sauti, ujumbe mfupi, intaneti yenye kasi na huduma za kifedhaza kwenye mitandao ya simu za mikononi, Tigo imeanzisha ubunifu kama vile Facebook ya Kiswahili, Kiunga cha Tigo Pesa kwa watumiaji wa simu za Android & iOS, Tigo Music ( Deezer)na huduma ya kwanza Afrika Mashariki kutuma fedha kwa njia ya simu za mikononi nje ya nchi yenye uwezo wa kubadili sarafu ya nchi husika.
 
Intaneti ya Tigo ya 3G inatoa huduma bora kwa wateja wake katika mikoa yote nchi nzima, na Hivi karibuni Tigo imezindua mtandao wa 4G ambao kwa sasa unapatikana Dar es Salaam nzima, na unatarajiwa kuzindualiwa nchi nzima.  Kati ya mwaka 2013 na mwaka 2014 pekee kampuni ilizindua zaidi ya minara mapya 500 yenye mtandao wa Tigo nakufanya kuwa zaidi ya maeneo 2000 ya mtandao na inapanga kuongeza uwekezaji wake mara mbili ifikapo 2017 katika suala la upatikanaji wa mtandao na kuongezauwezo wa upatikanaji wa mtandao kwa maeneo yasiyofikika kabisa vijijini.  
 
Pamoja na kuwa na zaidi ya wateja milioni 10 waliosajiliwa, Tigo imeajiri zaidi ya watanzania 300,000 ikiwa ni pamoja na mtandao wa wawakilishi wa huduma kwawateja, wafanyabiashara wakubwa wa fedha za kwenye simu za mikononi, mawakala wa mauzo na wasambazaji.
 
 Tigo ni nembo kubwa ya kibiashara ya kampuni ya Millicom, kampuni ya kimataifa  inayoendeleza maisha ya kidijitale katika nchi 11 pamoja na shughuli za kibiashara katika Afrika na Amerika yaKusini na ina ofisi kubwa Ulaya na Marekani.
Ukiwa ni mgahawa unaoongoza kwa vyakula  vinavyotokana na mazao ya baharini  na vinywaji  nchini Tanzania, Samaki Samaki  inamiliki migahawa mitatu  ambayo ipo Mlimani City
(Ubungo/Mwenge), City Centre (kwenye makutano ya Barabara ya Samora na Mirambo) na Samaki Samaki  kwenye Barabara ya Haile Selassie.
Tangu kuanzishwa kwa tawi la Mlimani City mwaka 2007 tumeshuhudia kupanuka kwa  Migahawa  ya Samaki Samaki  hadi matawi miwili  zaidi ndani ya jiji la Dar es Salaam katika kipindi cha miaka mitano ya uendeshaji wake,  kuongezeka kwa wateja ambao wanafikia hadi 1,000 kwa siku ndani ya matawi hayo,  kuongezeka  kuimarika  kwa nembo yetu ya biashara  na kutambuliwa na umma,  kupatikana kwa fursa za ajira kwa wazawa, jamii kutuunga mkono kupitia Mfuko wa Samaki Samaki ( Samaki Samaki Foundation) ambao unalenga kuwasaidia  wahitaji  kwa kutoa misaada ya kuwajibika kwa jamii,  jamii imeweza kutufikia  kwa kutumia  video na muziki uliorekodiwa  katika kukuza  nembo yetu kupitia Samaki Samaki Fleva na kuuza  bidhaa zetu nyingine  ambazo hazihusiani na chakula  zikiwemo kofia, fulana  na CD za muziki.
  Dira ya Samaki Samaki ni   kushikilia nafasi yake  nchini Tanzania  kwa kukua hadi mikoa mingine nchini  na hata baadaye  kusambaa hadi  kona nyingine za Afrika na dunia kwa ujumla. Kwa hivi sasa  inaangalia Mwanza na Arusha  kama vituo vya kuanzia kusambaa hadi mikoa mingine.

Bomba la mafuta kukamilika Juni mwaka 2020.

 
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akielezea uzoefu wa Tanzania kwenye
ujenzi wa miradi  ya mabomba ya gesi na mafuta katika mkutano huo. Kushoto ni Waziri wa Nishati na Maendeleo  ya Madini Nchini   Uganda, Mhandisi  Irene  Muloni na kulia ni  Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Maendeleo  ya Madini Nchini  Uganda, Dk. Fred Kaliisa (kushoto)
akifafanua  jambo katika kikao hicho. Kulia ni Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Nchini   Uganda, Mhandisi Irene Muloni.
Balozi wa Uganda Nchini Tanzania, Dorothy Hyuha akifafanua jambo katika mkutano huo.
 Wataalam kutoka Wizara, taasisi na makampuni ya mafuta kutoka Tanzania na Uganda wakifuatilia
kwa makini mada iliyokuwa inawasilishwa na mwakilishi kutoka kampuni ya Total
katika mkutano huo.

 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari
kuhusu
  utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi katika bandari ya  Tanga nchini
Tanzania. Kulia ni Waziri wa Nishati na Maendeleo  ya Madini Nchini   Uganda, Mhandisi  Irene Muloni.
 Waziri wa Nishati na Maendeleo  ya Madini Nchini   Uganda, Mhandisi  Irene
Muloni (kulia)  akifafanua jambo alipokuwa  akizungumza na waandishi wa
habari mara baada ya kukamilika kwa mkutano huo.  Kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini,
Profesa Sospeter Muhongo.
…………………………………………………………………………………………….
Na Greyson Mwase, Dar es Salaam
Bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi katika bandari  ya Tanga nchini Tanzania linatarajiwa kukamilika  mwezi Juni mwaka  2020.
Hayo yalielezwa na  Waziri wa Nishati na Madini,  Profesa Sospeter Muhongo alipokuwa   akizungumza na waandishi wa habari  mara baada ya kufanyika kwa mkutano kati yake na Waziri wa Nishati na Maendeleo  ya Madini Nchini   Uganda, Mhandisi  Irene  Muloni  aliyeambatana na ujumbe wake katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam
Lengo la mkutano huo lilikuwa ni kujadili mpango wa  mradi wa ujenzi wa bomba la  mafuta kutoka Hoima nchini  Uganda hadi katika  bandari ya  Tanga  nchini Tanzania ambapo ulikutanisha wataalam kutoka nchi zote mbili, ambao ni  wa  ardhi, miundombinu, maji, ujenzi, uchumi,, maji barabara pamoja na makampuni ya  mafuta.
Profesa Muhongo alisema  kuwa mara baada ya marais wa Tanzania na  Uganda kukubaliana kuanza kwa ujenzi wa bomba la mafuta,  kinachofuatia ni utekelezaji wa kasi  ya ajabu ambapo  tayari wameanza kukutana na kuunda kamati  ndogo ndogo  zitakazokuwa na wataalam mbalimbali kwa ajili ya kuanza mara moja kwa utekelezaji  wa mradi huo.
 Profesa Muhongo alisema kuwa  serikali  za nchi zote mbili zimejipanga katika kuhakikisha kuwa  ujenzi huo unakwenda kwa kasi  kubwa, ikiwezekana ujenzi ukamilike mwishoni mwa mwaka   2019.
Aliongeza kuwa serikali ya  Uganda inatarajia kujenga kiwanda kwa ajili  ya kusafisha mafuta ghafi Hoima ambapo  wametoa hisa  40 zenye  thamani  ya Dola za Marekani  bilioni 4.7 kwa nchi  zilizomo ndani ya Jumuiya ya  Afrika Mashariki ambapo kila nchi itaweza kununua asilimia nane ya hisa hizo na kusisitiza kuwa  Tanzania ipo  tayari kununua hisa  nane kwa thamani ya  Dola za Marekani  milioni 150.4
Aliendelea kusema kuwa hisa zitanunuliwa na serikali pamoja na wawekezaji binafsi watakaoonesha nia ya kununua hisa ili waweze kunufaika na mradi huo.
Hata hivyo aliongeza kuwa nchi ya  Uganda pamoja na nchi nyingine zilizomo ndani ya  Jumuiya ya  Afrika Mashariki wameomba  kununua  gesi kutoka nchini  Tanzania  na kusema kuwa kwa kuanzia  serikali inatarajia  kujenga bomba la  gesi hadi nchini Uganda   ili waweze kunufaika na  gesi hiyo.
Alisema kuwa bomba la gesi litasambazwa katika mikoa ya kaskazini na mingineyo ili  uchumi wa nchi uweze kukua kwa kasi na  Tanzania kuwa nchi  yenye  kipato cha kati  ifikapo mwaka  2025 kama   Dira  ya Maendeleo  ya Taifa inavyofafanua.
“ Kila sehemu  yenye  gesi ya kutosha, lazima  tuhakikishe  tunaweka bomba la  gesi ambalo  ni  mkombozi wa uchumi wa nchi,” alisisitiza Profesa Muhongo.
Wakati huo huo Waziri wa Nishati na Maendeleo  ya Madini Nchini   Uganda, Mhandisi  Irene  Muloni, aliishukuru serikali ya  Tanzania kwa kuwa tayari  kushirikiana na Uganda kwa ajili ya mradi mkubwa wa ujenzi wa bomba la mafuta.
Alisema kupitia  uzoefu  wa Tanzania  katika ujenzi wa mabomba ya  gesi na mafuta pamoja na wataalam  waliobobea anaamini kuwa mradi huu  utakwenda kwa kasi  kubwa na kukamilika kwa wakati.
Aliiomba  nchi ya   Tanzania pamoja na  wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na  makampuni ya mafuta, jamii itakayopitiwa na miundombinu  ya  bomba la mafuta kutoa ushirikiano ili mradi uweze kukamilika kwa wakati kama ilivyopangwa.
Alisema kuwa   mkutano  wa pili unatarajiwa kufanyika  Hoima nchini  Uganda tarehe  27 Mei, mwaka huu na kuendelea kufanyika katika  maeneo mbalimbali  yatakayopitiwa na bomba la  mafuta.

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA RASMI KIKAO KAZI CHA MAKAMANDA WA POLISI, WANASHERIA WA SERIKALI WAFAWIDHI WA MIKOA NA WAKUU WA UPELELEZI WA MIKOA NA VIKOSI.

JA1 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Makamanda wa Polisi, Wanasheria wa Serikali,  Wafawidhi wa Mikoa na Wakuu wa upelelezi wa Mikoa na Vikosi kabla ya kufungua rasmi Kikao kazi cha Makamanda hao wa Polisi katika Ukumbi wa Dodoma Convention Center
JA2 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Makamanda wa Polisi, Wanasheria wa Serikali,  Wafawidhi wa Mikoa na Wakuu wa upelelezi wa Mikoa na Vikosi kabla ya kufungua rasmi Kikao kazi cha Makamanda hao wa Polisi katika Ukumbi wa Dodoma Convention Center
JA4 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama pamoja na viongozi wengine wakati wimbo wa Jeshi la polisi ukipigwa. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Charles Kitwanga, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Valentino Mlowola, Kushoto kwake ni Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harison Mwakyembe , Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad  Yusuph Masauni na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Ernest Mangu.
JA5 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye ukumbi wa Mikutano wa Dodoma Convention Center kwa ajili ya ufunguzi wa rasmi Kikao kazi cha Makamanda hao wa Polisi.
JA6 
Baadhi ya Makamanda wa polisi wa Mikoa mbalimbali wakipiga makofi wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia.
JA7 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu kabla ya kufungua kikao kazi hicho.
JA8 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kufungua kikao kazi hicho.
JA9 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Makamanda wa Polisi wa mikoa mara baada ya kufungua kikao kazi chao katika ukumbi wa Dodoma Convention Center mjini Dodoma.
JA10 
Baadhi ya Makamanda wa polisi wa Mikoa mbalimbali wakiimba Wimbo wa Jeshi la Polisi kabla ya ufunguzi wa Kikao kazi hicho.
JA11 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kamanda wa Kikosi cha Usalama barabarani Mohamed Mpinga
JA12 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na baadhi ya Wanasheria wa Serikali, Wafawidhi wa Mikoa na