WIZARA YA AFYA KUFANYA UZINDUZI WA KONDOMU MPYA MKOANI MWANZA.
Baada
 ya juzi Agost 30,2016 Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee
 na Watoto, kuzindua aina mpya ya Kondomu iitwayo Zana Kondomu mkoani 
Mbeya, Uzinduzi kama huo unatarajiwa kufanyika mkoani Mwanza Septemba 
05,mwaka huu.
Afisa
 Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza, Atley Kuni (pichani), jana 
alisema mkoa wa Mwanza unatarajia kupokea ugeni kutoka wizara hiyo ambao
 utajumuisha wataalamu mbalimbali wa afya watakaokuwa wakitoa semina na 
elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo kutumia vyombo vya habari, wakielezea 
juu ya uzinduzi wa kondomu hiyo.
Alisema
 miongoni mwa dhumuni la kuzindua aina hiyo mpya ya Kondomu, ni kusaidia
 katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Ukwimwi ambapo 
Wizara itakuwa ikigawa bure kondomu hizo zenye ubora kwa wananchi, kote 
nchini.
 Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza, Atley Kuni
Baadhi ya Wanahabari mkoani Mwanza, wakimsikiliza Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni