DUMISHENI MICHEZO KUONGEZA UFANISI KATIKA KAZI; KATIBU MKUU KIONGOZI
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi 
……
Na Shamimu Nyaki WHUSM.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John
 Kijazi amewataka Watumishi wa Umma kushiriki katika Michezo mbalimbali 
ili kuwa na afya imara itakayosaidia ufanisi katika kutekeleza kazi zao.
Balozi Kijazi ametoa rai hiyo 
leo Jijini Dar es Salaam katika hotuba yake iliyosomwa na Katibu Mkuu 
Ofisi ya Rais  Utumishi  Dk.Lawrence  Ndombaro katika  Bonanza  la  
Michezo la  ufunguzi wa mashindano  ya thelatini  na nne yanayojulikana 
kama  SHIMIWI  lililofanyika katika Uwanja wa Uhuru wa Jijini  humo.
“Michezo inasaidia mwili kuwa na
 afya njema na kuondoa msongo wa mawazo pamoja na kuleta nguvu na akili 
katika mwili vinavyosaidia  katika utendaji bora wa Mtumishi kwa 
maendeleo ya Taifa”.Alisema Balozi Kijazi.
Aidha Katibu  Mkuu  Kiongozi 
 Balozi  Kijazi  amewataka  Viongozi wa Serikali na Taasisi  zake 
kutenga muda kwa Watumishi  wanamichezo  wa kufanya mazoezi  pamoja na 
kuwapatia  vifaa vya michezo ili waweze kufanikiwa  katika mashindano 
 hayo.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa 
Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel 
amewapongeza Watumishi wake kwa kushiriki Bonanza hilo na kuahidi kuwapa
 muda mzuri wa maandalizi ili wafanye vizuri katika mashindano hayo.
Akifafanua maandalizi ya timu ya
 Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mwenyekiti wa timu hiyo 
Bw. John Manyika ameahidi ushindi kwa timu yake kwani wanaendelea 
kijiandaa vizuri katika mazoezi.
Mashindano ya SHIMIWI 
yanatarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu mjini Dodoma kuanzia 
tarehe 14 ikiwa ni kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius 
Kmbarage Nyerere.
Bonanza hilo lilimalizika kwa 
timu ya Jiji la Dar es Salaam kutwaa Kikombe kwa kuwa na wanamichezo 
wengi ikifuatiwa na Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni