![](file:///C:/Users/MWAIPU~1/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg)
![Text Box: World Change Starts with Educated Children®](file:///C:/Users/MWAIPU~1/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image003.png)
Msingi wa Usomaji bora ni mtoto kujua kusoma kwa
wakati.
Tanzania kama nchi nyingi zinazoendelea bado
inakabiliwa na changamoto kubwa ya kuwa na wananchi wasiojua kusoma na kuandika
ndani ya mfumo wa elimu na nje ya mfumo wa elimu, na hii ndio sababu,
RoomtoRead imeamua kuandaa mjadala huu wa wadau wa usomoji ili tutafakari na
kuweka mikakati ya kuwa na taifa lisilokuwa na wasiojua kusoma
– Peter Mwakabwale: Mkurugenzi mkaazi wa Room to Read Tanzania .
Takwimu
zinaonyesha asilimia 22 Ya watanzania wote hawajui kusoma na kuandika. Takwimu hizi haziishii kuwa takwimu kwa maana
ya namba tu, bali hawa ni watanzania wenzetu, wapiga kura, wateja wa huduma
zetu, wazazi wetu na vijana wetu ambao wataongoza taifa hili kwa miaka kadhaa
ijayo. Watanzania inabidi tujiulize ni
nini kimetokea? Miaka ya 70 na 80 watanzania wengi walikuwa wanajua kusoma na
kuandika, kinyume na sasa ambapo teknolojia imekuwa Zaidi, shule ziko nyingi
Zaidi nk.
“Tatizo
la nchi yetu ni kuweka vipaumbele katika mambo ambayo hayachangii katika
kuondoa umbumbumbu. Mpaka sasa, Asilimia 90% ya watanzania chanzo chao cha
habari ni kusikia na kuona sio kusoma” Professor
Kitila Mkumbo mhadhiri wa chuo kikuu cha Changangombe.
Kutojua kusoma
na kuandika hakukwamishi tu mapambano yetu dhidi umaskini bali kuna athari za
moja kwa moja katika biashara, kwa mujibu wa bwana Noel Mazoya- Meneja wa Masoko
Vodacom, “Taasis kama Vodacom, inatumia muda na pesa nyingi sana kuwafikia
wateja wao ana kwa ana kwa sababu tu baadhi ya wateja wao, hasa wa vijijini
hawajui kusoma na kuandika hivyo kushindwa kuwafikia kwa njia wa ujumbe mfupi
au kidigitali”.
Vyombo vya
habari na wasanii wananafasi kubwa katika kuongeza au kuhakikisha janga hili la
ujinga litatokomezwa. Hapa nchini Tanzania, baadhi ya vyombo vya habari
vinachangia kukuza tatizo la kutojua kusoma “Msingi wa vyombo vya habari ni
kufundisha, kufurahisha na kuhabarisha, ila kwa sasa, kuna vyombo vya habari
pendwa, vinavyotoa habari nyepesi hata kama hazina mwelekeo wa kuikuza jamii
hiyo,”. Victor Eliah – Television ya Taifa
Sanaa ndio kitu
cha kwanza kinachotumika kumfundisha binadamu, kwa mfano, watoto wa shule za
awali wanajifunza kwa michoro na nyimbo. Tunahitaji wasanii wanajua umuhimu wa kusoma
na elimu ili waweze kutunga Sanaa yenye kuijenga jamii. Wananchi wawekuwa
chanzo cha tatizo kwa kutothamini kazi za Sanaa zenye kuelimisha badala yake, huthamini
na kazi za Sanaa zenye kuburudisha tu - Vitalis Maembe (Msaanii
Mkongwe)
Jitihada za
wadau wa elimu katika kuhakikisha kila mtoto anajua kusoma kwa wakati,
zinahitaji mazingira mazuri ya kisera. “Kuwepo
kwa sera mpya ya elimu bure ni jitahada zinazotakiwa kupongezwa” ingiwa
takwimu za taasis mbalimbali zinaonyesha kiwango cha elimu yetu kinashuka,
mfano 16% ya wanafunzi wa darasa la saba hawawezi kusoma habari ya darasa la
pili. John Kallaghe, Mkurugenzi wa Hakielimu Tanzania
Mapendekezo ya Wadau:
1.
Ni lazima tujikite katika
kuwekeza katika watoto walioko nje ya shule, watoto million 2 wako nje ya shule
na hawajui kusoma na kuandika.
2.
Ubora wa elimu hauwezi kuja
bila uwekezaji timilivu. Serikali inabidi iongeze fungu la bajeti ya elimu hasa
bajeti ya elimu elimu ya msingi.
3.
Walimu ndio chachu ya
mabadiliko katika kuboresha ubora wa elimu yetu,Kubadilika kwa mitaala kuendane
moja kwa moja kuwekeza kwenye ubora wa walimu
4.
Kwa namna ya pekee serikali inathamini sana
mchango wa taasis sizizo wa kiserikali katika kuboresha ubora wa elimu nchini Tanzania
– Waziri Simbachawene.
Rejea
Room to Read, ni shirika la kimataifa lisilo la
kiserikali linalolenga kubadilisha maisha ya watoto katika nchi zinazoendelea
kupitia uboreshaji wa mazingira ya kusoma na kujisomea pamoja na elimu bora kwa
watoto wa jinsia zote. Shirika lilianzishwa mwaka 2000 kwa filosofia ya kuwa “Mabadiliko
ya Dunia Yanaanza na Watoto Walioelimika”. Room to Read wanaiona dunia yenye
mazingira yanayomuwezesha kila mtoto kupata elimu bora itakayomuwezesha kukua
na kuweza kutoa mchango katika jamii yake na hata kwa dunia nzima.
Mfumo wa miradi ya Room to Read umejengwa katika Nyanja kuu
mbili:
·
Wakati wa awali wa Elimu ya msingi kwa ajili ya kukuza
usomaji.
Tunafanya kazi na jamii pamoja na serikali kuimarisha stadi
za usomaji na tabia ya kujisomea kwa watoto wa shule za msingi.
·
Wakati wa elimu ya sekondari; kwa elimu ya wasichana:
Tunahakikisha msichana anaweza kumaliza elimu ya sekondari
akiwa na stadi za maisha zinazomuwezesha kuyakabiri mazingira anayoishi.
Room to Read inaendesha miradi yake katika nchi 10 duniani ikiwemo, Bangladesh, Cambodia, India, Laos, Nepal, Afrika ya
Kusini, Sri Lanka, Tanzania, Vietnam na Zambia, na imelenga kuwafikia watoto
milioni 20 ifikapo mwaka 2020.
Nchini
Tanzania, Room to Read imeanza kufanya kazi mwaka 2011, kwa kuanzia Mkoa wa
Morogoro, wilaya ya Mvomero, na baadae kuongeza miradi yake katika mkoa wa
Pwani, katika halmashauri za wilaya ya Bagamoyo, Chalinze na Kibaha.
Miradi
inayotekelezwa nchini Tanzania ipo katika Nyanja kuu tatu:
1. Ujenzi na ukarabati miundombinu shuleni:
·
Ujenzi wa Maktaba na
·
Ujenzi na ukarabati wa vyumba vya
madarasa kwa shule za msingi
2. Stadi za Usomaji:
·
Uandishi wa vitabu vya haditihi za
watoto, vitabu vya walimu vya kufundishia na vya wanafunzi vya kujifunzia.
·
Kuwafunza walimu wa darasa la kwanza na
la pili mbinu za ufundishaji
·
Kuwafundisha na kuwaandaa walimu
wakutubi
3. Elimu ya Stadi za Maisha kwa Wasichana:
·
Kutoa elimu za stadi za maisha kwa
wasichana
·
Kuwasaidia wasichana waliochaguliwa
kuendelea na elimu ya sekondari wanaotoka katika familia zenye uwezo duni.
Mafanikio:
Hadi
leo, Room to Read imeweza kushirikiana na shule za msingi 98 za serikali katika
halmashauri nne za Mvomero,
Bagamoyo, Chalinze and Kibaha vijijini na
kuwa na mafanikio yafuatayo:
·
Kujenga vyumba
113 vya madarasa
·
Kujenga Maktaba
98
·
Kukarabati vyumba
vya madarasa 34
·
Kuandika na
Kuchapisha vitabu 89,000 vya Hadithi za watoto kwa Kiswahili
·
Kununua na Kugawa
vitabu 112,000 vya Hadithi za watoto za kiswahili
·
Kufundisha walimu
35 wa darasa la kwanza
·
Kufundisha walimu
35 wa darasa la pili
·
Kufundisha wakuu
wa shule za msingi zipatazo 77
·
Kufudisha waalimu
wa taaluma 26
·
Kufundisha
waalimu wakutubi wa shule za msingi zipatazo 77 katika Nyanja ya utawala na
uendeshaji shughuli za maktaba
·
Kufundisha
Maafisa elimu wanne wa halmashauri nne za wilaya
·
Kufundisha
wakaguzi elimu wanne wa halmashauri nne za wilaya
·
Kufundisha
Waratibu elimu kata 19
·
Shule 9 za
sekondari zinapata msaada wa elimu kwa wasichana
·
Shule 9 za
sekondari zinapata ruzuku kwa ajili ya masomo ya ziada kwa wasichana
·
Wasichana 1906 wa
sekondari wamenufaika na wanendelea kunufaika na mradi
·
Watoto
wapatao 48000 wa shule ya msingi
wanafaidika na mradi
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni