Jumanne, 13 Septemba 2016

Sophia Mjema Akabidhi Msaada Muhimbili Leo


mje1
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akipokea msaada wa kitanda cha wagonjwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kutoka Kikundi cha Itambue Thamani Yako cha jijini Dar es Salaam LEO.
mje2
Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Sophia Mjema akisalimiana na kina mama wa kikundi hicho leo baada ya kupokea msaada wa kitanda hicho.
mje3
Mkuu huyo akitembelea chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) leo katika hospitali hiyo.
mje4
Mwenyekiti wa kikundi hicho, Magreth Makwesa akizungumza na vyombo vya habari leo kabla ya kukabidhi msaada.
mje5
Kinamama wa kikundi hicho wakiwa katika picha ya pamoja leo katika hospitali hiyo.
mje6
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema (aliyefunga kitambaa cha bluu) akiwa katika picha ya pamoja na kinamama wa kikundi cha Itambue Thamani Yako leo.
……………………………………………………………………………….
Na John Stephen, MNH
Dar es Salaam, Tanzania. Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Sophia Mjema amewataka watu wajitokeze katika kusaidia sekta ya afya nchini.
Mkuu huyo wa wilaya ameyasema hayo Leo wakati akipokea msaada wa kitanda kutoka katika Kikundi cha kinamama cha Itambue Thamani Yako cha jijini Dar es Salaam.
“Watu wajitokeze kusaidia vifaa tiba kama walivyofanya wenzetu wa kikundi cha Itambue Thamani Yako. Nawapongeza kina mama kwa jitihada zenu,” amesema mkuu huyo.
Baada ya kupokea msaada huo, Mjema ametembelea chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) na kuona jinsi huduma zinavyotolewa.
 
Naye Mwenyekiti wa kikundi hicho, Magreth Makwesa amesema kwamba kitanda hicho kina thamani ya Sh3.5 milioni.
Amesema malengo ya kikundi hicho ni kina wanachama 40 na kwamba malengo yake ni kusaidiana katika shida na raha, kuinuana kiuchumi na kuisadia jamii.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni