JUMA NATURE, PETER MSECHU KUTUMBUIZA TAMASHA LA SIKU YA MSANII WA TANZANIA KIJIJI CHA MAKUMBUSHO
Msanii Juma Nature ambaye ni mmoja wa wasanii watakaotumbuiza katika Siku ya Msanii wa Tanzania kesho Septemba 24 kwenye kijiji cha Makumbusho jijini Dar es salaam.
……………………………………………………………………..
Na Herieth Semgaza
Katika kuadhimisha siku ya msanii wa Tanzania , kwa mara ya kwanza hapa nchini Tamasha la sikuMsanii wa Tanzania litafanyika Septemba 24 katika kijiji cha Makumbusho jijini Dar es salaam, Siku hii itawakutanisha wasanii wa sanaa aina mbalimbali katika jukwaa moja .
Augustino Makama ambaye ni mratibu wa Tamasha la Siku ya Msanii wa Tanzania kutoka BASATA ametoa ufafanuzi wa mambo kadhaa wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es salaam
Augustino Makama afisa sanaa BASATA amesema kuwa siku ya msanii inawakutanisha wasanii wa sanaa ya Mziki, Filamu, Ufundi, na Maonyesho.ilikuonyesha umahiri na uwezo wao kwa hadhira wawapo katika jukwaa.
Aidha ameongeza Kuwa mradi huu umebuniwa na Balaza la Sanaa la Taifa BASATA lengo lake kubwa likiwa ni kutambua, kuhamasisha na kuthamini kazi zinazotolewana na wasanii wa Tanzania.
Kauli mbiu ya “Nguvu ya Sanaa”Itakayo jumuisha mtiririko wa matukio ambapo tayari maadhimisho hayo yalishazinduliwa tangu tarehe 26 Mei 2016 na Waziri wa Habari, Sanaa ,Utamaduni na Michezo Mh Nape Nauye.kwa uwakilishi wa katibu wa wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel .
Maadimisho yatafanyika katika kijiji cha Makumbusho ya Taifa Kijitonyama jijini Dar es salaam yakidhaminiwa na kampuni ya HAAK NEEL PRODUCTION LTD
Kilele cha maadhimisho hayo kitakuwa tarehe 29 Ocktoba 2016 ambapo wasanii mbalimbali watapewa tuzo kutokana navigezo vilivyowekwa kwa ajili ya kupata wasanii wenye kazi bora na zenye viwango.
Kilele cha maadhimisho hayo kitakuwa tarehe 29 Ocktoba 2016 ambapo wasanii mbalimbali watapewa tuzo kutokana navigezo vilivyowekwa kwa ajili ya kupata wasanii wenye kazi bora na zenye viwango.
Tamasha hilo litaburudishwa na wasanii Juma Nature, Peter Msechu, Misoji pamoja na wasaniii wengine watakao kuwepo jukwaani ili kuwapa burudani waalikwa watakaohudhuria , Katika Tamasha hilo hakutakuwa na kiingilio ambapo litaanza saa tatu asubuhi mpaka saa tatu usiku
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni