PROF. MBARAWA AKAGUA ATHARI ZA MIUNDOMBINU KAGERA
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza na Meneja wa Wakala wa 
Barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Kagera Eng. Andrea Kasamwa wakati 
alipokagua athari za tetemeko la ardhi lililoikumba miundombinu ya 
barabara mkoani humo.
Muonekano wa sehemu ya barabara ya
 Rwamishenye hadi Bandari ya Bukoba yenye urefu wa KM 4.6 ambayo 
imeathirika mita 60 kutokana na tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa mafundi wa 
wanaodhibiti eneo lililoathirika na tetemeko la ardhi katika barabara ya
 Bukoba-Mtukula yenye urefu wa KM 80 ambayo imeathirika kwa mita 200, 
mkoani Kagera.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amekagua athari za tetemeko la ardhi 
lililoikumba miundombinu ya barabara katika mkoa wa Kagera na kujionea 
athari zilizojitokeza katika mkoa huo.
Prof. Mbarawa amejionea athari za 
tetemeko la ardhi katika barabara ya Rwamishenye hadi Bandari ya Bukoba 
yenye urefu wa KM 4.6 ambayo imeathirika mita 60 na barabara ya 
Bukoba-Mtukula yenye urefu wa KM 80 ambayo imeathirika kwa mita 200 na 
kusisitiza kwamba Wizara yake itatekeleza maelekezo yaliyotolewa na 
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ili kukabiliana na changamoto 
zilizojitokeza.
“Tunatoa pole kwa wananchi wa mkoa
 wa Kagera kutokana na maafa yaliyojitokeza hivyo tutafanyia kazi 
maelekezo ya ukarabarati wa miundombinu iliyoathiriwa na tetemeko kadiri
 tulivyoelekezwa na Waziri Mkuu”, amesema Prof. Mbarawa.
Prof. Mbarawa yuko mkoani Kagera 
kukagua athari za uharibifu wa miundombinu kufuatia tetemeko la ardhi 
lililopiga mikoa ya Kagera, Mara na Mwanza Septemba 10 mwaka huu na 
kusababisha vifo vya watu takribani 16, majeruhi zaidi ya 100, 
uharibibifu wa nyumba takribani 800 na miundombinu.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni