Jumapili, 11 Septemba 2016

Wafanyakazi wa TBL wasafisha mazingira Ilala Mchikichini


us1
Wafanyakazi wa kiwanda cha bia cha Ilala (TBL Group)  wakifanya usafi kwenye mfereji wakupitisha maji machafu uliopo katika Mtaa wa Mission  Kota ya Mchikichini Ilala jijini Dar es Salaam.
us2
Afisa Mwandamizi wa Kiwanda cha bia cha TBL  Ilala jijini Dar es Salaam, Charles Nkondola (kushoto) akibadilishana mikakati ya usafi na  Diwani wa kata ya Mchikichini  Joseph Ngowa ( kulia) . Katikati ni Afisa usalama na Afya wa TBL Group, Khery Gunzarethy.
us3
Afisa Mwandamizi wa kiwanda cha TBL cha Ilala Charles Nkondola akishirikiana na wafanyakazi wenzake kufanya usafi kwenye mtalo wa kupitisha maji machafu wa Mission uliopo katika kata ya Mchikichini jijini Dar es Salaam
us4
Wafanyakazi wa kiwanda cha bia cha TBL Ilala jijini Dar es Salaam, wakiongozwa na Afisa usalama na Afya wa TBL Group, Khery Gunzarethy wakifanya usafi kwenye mtalo wa kupitisha maji machafu   uliopo katika kata ya Mchikichini .
us5
Wafanyakazi wa Kiwanda cha bia cha TBL Ilala jijini Dar es Salaam, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Kata ya Mchikichini mara baada ya kumalizika kwa zoezi la kufanya usafi wa mfereji wa Mission Kota .
……………………………………………………………..
Wafanyakazi wa kampuni ya TBL Group kiwanda cha Ilala jijini Dar es Salaam  jana walitumia sehemu ya muda wao kwa kushiriki kwenye shughuli za jamii ambapo walisafisha maeneo ya Ilala Mchikichini.
Zoezi hilo ni moja ya mkakati wa kampuni wa kutunza mazingira kwa vitendo ambapo pia wafanyakazi wake kutoka viwanda vyake vyote nchini mara kwa mara wamekuwa wakishiriki katika shughuli za usafi mara kwa mara.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni