Wafanyakazi wa TBL wasafisha mazingira Ilala Mchikichini
Wafanyakazi wa kiwanda cha bia cha
 Ilala (TBL Group)  wakifanya usafi kwenye mfereji wakupitisha maji 
machafu uliopo katika Mtaa wa Mission  Kota ya Mchikichini Ilala jijini 
Dar es Salaam.
Afisa Mwandamizi wa Kiwanda cha 
bia cha TBL  Ilala jijini Dar es Salaam, Charles Nkondola (kushoto) 
akibadilishana mikakati ya usafi na  Diwani wa kata ya Mchikichini  
Joseph Ngowa ( kulia) . Katikati ni Afisa usalama na Afya wa TBL Group, 
Khery Gunzarethy.
Afisa Mwandamizi wa kiwanda cha 
TBL cha Ilala Charles Nkondola akishirikiana na wafanyakazi wenzake 
kufanya usafi kwenye mtalo wa kupitisha maji machafu wa Mission uliopo 
katika kata ya Mchikichini jijini Dar es Salaam
Wafanyakazi wa kiwanda cha bia cha
 TBL Ilala jijini Dar es Salaam, wakiongozwa na Afisa usalama na Afya wa
 TBL Group, Khery Gunzarethy wakifanya usafi kwenye mtalo wa kupitisha 
maji machafu   uliopo katika kata ya Mchikichini .
Wafanyakazi wa Kiwanda cha bia cha
 TBL Ilala jijini Dar es Salaam, wakiwa katika picha ya pamoja na 
viongozi wa Kata ya Mchikichini mara baada ya kumalizika kwa zoezi la 
kufanya usafi wa mfereji wa Mission Kota .
……………………………………………………………..
Wafanyakazi wa kampuni ya TBL 
Group kiwanda cha Ilala jijini Dar es Salaam  jana walitumia sehemu ya 
muda wao kwa kushiriki kwenye shughuli za jamii ambapo walisafisha 
maeneo ya Ilala Mchikichini.
Zoezi hilo ni moja ya mkakati wa 
kampuni wa kutunza mazingira kwa vitendo ambapo pia wafanyakazi wake 
kutoka viwanda vyake vyote nchini mara kwa mara wamekuwa wakishiriki 
katika shughuli za usafi mara kwa mara.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni