KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI PWANI CHAKUSANYA BIL.2.033
Kamanda wa kitengo cha Usalama barabarani  mkoani Pwani, Abdi Issango pichani.
 (Picha na Mwamvua Mwinyi)
……………..
Na Mwamvua Mwinyi
Kikosi cha usalama barabarani mkoa
 wa Pwani kimeliingizia serikali mapato ya zaidi ya sh.bil.2.033 katika 
kipindi cha januari hadi agosti mwaka huu .
Kikosi hicho kimekusanya mapato hayo kupitia ukamataji wa makosa mbalimbali ya usalama barabarani mkoani humo.
Mkuu wa usalama barabarani mkoani 
Pwani, Abdi Issango alisema  katika kupambana na ajali wameweza 
kuendesha misako na kufanya ukaguzi mbalimbali katika barabara kuu na za
 ndani ya miji.
Alieleza kuwa kwa kipindi miezi 
nane wamekamata jumla ya  makosa 68,109  ambapo yaliyolipiwa kiasi hicho
 cha fedha ni 67,785 mwaka huu.
Kamanda Issango alisema makosa 
hayo yakilinganishwa na ya mwaka jana kipindi hicho kuna ongezeko la 
makosa 20,797 ambayo ni sawa na ongezeko la sh. mil. 569,400 sawa na 
asilimia 38.89.
Alisema kuwa katika kipindi kama 
hicho mwaka 2015 kitengo hicho kilikamata makosa 47,109 na yaliyolipiwa 
ni 46,988 sh.bil. 1,464,150.
Aidha akizungumzia matumizi ya 
speed radar mpya 24 za kisasa walizopewa mwaka jana ambazo zinapiga 
picha na kurekodi wameweza kukamata makosa ya magari yanayokwenda kwa 
mwendo kasi 32,753 .
Kamanda Issango alisema magari 
hayo yaliyokamatwa kwa ajili ya kukimbiza magari yalilipiwa faini sh. 
mil 982,590 kutoka januari hadi agosti mwaka huu.
“Vitendea kazi tulivyonavyo ikiwa 
ni pamoja na speed radar hizi za kisasa, tunaweza kusema sisi Pwani 
tumefanikiwa kudhibiti ajali zitokanazo na mwendo kasi kwa asilimia 100 
hasa mabasi ya abiria”alisema Issango.
Hata hivyo kitengo hicho kuelekea 
maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani wameanza kutoa 
mafunzo mbalimbali kwa waendesha pikipiki,wanafunzi wa shule za msingi 
na sekondari na mikusanyiko ya watu ili kuwapa uelewa wa matumizi sahihi
 ya alama za barabarani.
Issango aliwataka madereva ,abiria
 na watumiaji wengine wa barabara kuu kuzingatia kanuni,sheria na 
taratibu ya matumizi ya njia hizo kuu ili kuendelea kudhibiti ajali.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni