Wafugaji wamwomba Rais Magufuli kuwanusuru ng’ombe wao
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wafugaji 
Tanzania (CCWT), Maghembe Makoye akizungumza na waandishi wa habari 
wakati akifafanua mambo mbalimbali kuhusu wafugaji walionyaganywa mifugo
 yao na uongozi wa hifadhi ya Pori la  akiba Katavi , Kushoto ni mfugaji
 anayelalamikia kunyang’anywa mifugo yake Mayunga Gamasa na kulia ni 
mfugaji  Charles Mtokambali.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wafugaji 
Tanzania (CCWT), Maghembe Makoyeakionyesha hukumu iliyotolewa na 
mahakama kuu Kanda ya Sumbawanga ili wafugaji hao warudishiwe mifugo yao
 kushoto  ni Mayunga Gamasa mfugaji na kulia ni mfugaji  Charles 
Mtokambali.
………………………………………………………………………………
NA MWANDISHI WETU
WAFUGAJI wa mkoa wa Katavi, 
wamemwomba Rais John Magufuli kuwasaidia kurejeshewa mifugo yao 1,600 
ambayo imeshikiliwa na watendaji wa hifadhi ya Katavi.
Wamesema mifugo hiyo aina ya 
ng’ombe ilikamatwa Machi mwaka huu na kufunguliwa kesi lakini baada ya 
kesi hiyo walishinda na kuamliwa kurejeshewa ng’ombe zao lakini mpaka 
sasa amri hiyo haijatekelezwa.
Wakizungumza na waandishi wa 
habari leo jijini Dar es Salaam wamesema, kutokana na unyanyasaji 
wanaofanyiwa na watendaji hao wa hifadhi, Rais Magufuli ambaye ni 
mtetezi wa wanyonge atupie jicho suala lao na kulimaliza.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wafugaji 
Tanzania (CCWT), Maghembe Makoye alisema wafugaji waliochukuliwa mifugo 
yao hivi sasa familia zao zinaishi maisha ya shida kwani hawana njia 
mbadala wa kupata fedha na ufugaji ndiyo tegemeo lao.
“Tunamwomba Rais Magufuli aingilie
 kati jambo hili ili Watanzania hawa wanyomge wapate haki yao. 
 Tunanyanyasika katika nchi yetu, huku chini kuna watu wanaendesha 
serikali zao, hawajui juu kuna Magufuli, tunamwomba sana Rais alione 
hili,” alisema Makoye
Alisema agizo la Rais la kuwataka 
wakuu wote wa mikoa kubaini na kutenga maeneo kwa ajili wafugaji nchini 
limeshindwa kuchukuliwa kwa uzito wake mpaka sasa hivyo umefika wakati 
wa kulifanyia kazi.
Katibu huyo alisema katika 
kufanikisha agizo hilo la Rais Magufuli kwa ufanisi, wameomba 
kushirikishwa ili kumaliza migogoro iliyopo kati ya wafugaji na 
wakulima.
Naye  Mayunga Gamasa alisema kati 
ya ng’ombe hizo 1600 yeye zake ni 552 ambazo kukamatwa kwake zimemfanya 
kuwa masikini huku familia yake yenye watu zaidi ya 70 ikiishi kwa shida
 kwani chanzo cha mapato ndiyo hicho kimeondoka.
“Mimi nina watoto 28, waijukuu 24,
 wake wane  jumla na wasaidizi kama watu 70, sasa ng’ombe hawa ndiyo 
msaada kwangu, lakini uongozi wa hifadhi ya Katavi haitaki kutupatia 
licha ya kushinda kesi, tunaomba Rais atusaidie” alisema Gamasa
Naye Charles Mtokambali mwenye 
ng;ombe zaidi ya 700, alisema kunyimwa kwa ng’ombe hao kumebadili maisha
 yake kwani kwa sasa familia yake haijui kesho yake, kutokana na 
watendaji hao wa hifadhi huku akisema ana imani kubwa na Rais kwamba 
atalishughulikia suala hilo.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni