PROF.MBARAWA AZINDUA KIVUKO CHA MV .TANGA NA GATI YA BANDARI YA PANGANI
Mbunge wa Jimbo la Pangani Mhe. 
Jumaa Awesu akizungumza na wananchi wa Jimbo hilo katika uzinduzi wa 
Kivuko cha Mv. Tanga na Gati ya bandari ya Pangani uliofanyika Mkoani 
Tanga.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka 
ya Bandari Tanzania (TPA) Eng.Karim Mattaka akisoma taarifa ya ujenzi wa
 Gati ya bandari ya Pangani kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani) katika uzinduzi wa 
Kivuko cha Mv. Tanga na Gati hiyo uliofanyika  Mkoani Tanga.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Ndg. Martin 
Shigela akielezea taarifa ya utekelezaji wa Miradi ya Miundombinu katika
 Mkoa wa Tanga kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa 
Makame Mbarawa (hayupo pichani) katika uzinduzi wa Kivuko cha Mv. Tanga 
na Gati hiyo uliofanyika  Mkoani Tanga.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akifafanua jambo kwa wananchi wa 
Pangani katika uzinduzi wa Kivuko cha Mv. Tanga na Gati hiyo uliofanyika
  Mkoani Tanga.
Wananchi wa Pangani wakishangilia 
ujio wa Kivuko kipya cha Mv. Tanga Wilayani hapo kinachotoa huduma ya 
usafirishaji kati ya Pangani na Bweni.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa pamoja  na watendaji wa Serikali na 
Wizara wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Kivuko cha Mv. Tanga 
kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pamgani Mhe. Zainabu Abdallah Issa  .
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa pamoja na  watendaji wa Serikali na 
Wizara wakizindua Gati la Bandari ya Tanga.Ukamilifu wa Gati hiyo 
utasaidia Meli mbalimbali  kuweza kutia nanga wilayani Pangani.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa pili kulia) akisafiri na wakazi 
katika Kivuko cha Mv.Tanga kutoka Pangani kwenda Bweni mara baada ya 
uzinduzi. Wanne kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Ujenzi) 
Eng. Joseph Nyamhanga.
…………………………………………………………………
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amezindua kivuko kipya na cha kisasa 
cha Mv. Tanga kinachotoa huduma ya usafirishaji kati ya Pangani na Bweni
 na kuzindua Gati ya Bandari ya Pangani wilayani pangani mkoani Tanga.
Akizungumza katika uzinduzi huo 
Waziri Mbarawa amesema kuwa ujio wa kivuko hicho utafungua fursa za 
kibiashara na kuchochea maendeleo ya kiuchumi wilayani hapo.
“Naamini ujio wa kivuko hiki 
utarahisisha huduma za kijamii na maendeleo ya kiuchumi wilayani hapa, 
hivyo naomba mkitunze vizuri kivuko hiki ili kiweze kudumu kwa muda 
mrefu”, amesema Prof.Mbarawa.50 242
Ameongeza kuwa katika kuhakikisha 
huduma za kivuko zinakuwepo muda wote wilayani hapo, Serikali kupitia 
Wizara hiyo imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa boti ambayo itatumika 
kama mbadala wa usafiri wakati wa usiku katika maeneo hayo ambapo kivuko
 cha Mv.Tanga hakifanyi kazi.
Kuhusu ujenzi wa Gati ya bandari 
ya Pangani Waziri Mbarawa ameseama kuwa ujenzi wa gati hiyo utapelekea 
Meli kubwa kuweza kutia nanga na kurahisisha usafiri wa moja kwa moja 
kutoka Pangani kwenda visiwa vya Unguja na Pemba.
Amefafanua kuwa Serikali kwa 
kushirikiana na wadau mbalimbali wataanzisha huduma ya boti za haraka 
kutoka Pangani kwenda Mkokotoni Zanzibar hivyo kufungua fursa za 
kibiashara na kitalii baina ya Tanga na Zanzibar.
Kwa upande wa huduma za 
mawasiliano ya simu wilayani hapo, Prof.Mbarawa amesema kuwa huduma hiyo
 itaanza mwezi Desemba mwaka huu kwa mkandarasi kufika na kuanza ujenzi 
wa miundombinu ya simu na hivyo kuondoa tatizo la mawasiliano wilayani 
hapo.
Katika hatua nyingine Prof. 
Mbarawa amehahidi kuanza ujenzi wa Barabara ya Tanga-Pangani-Saadani 
hadi Bagamoyo (KM 242) kwa kiwango cha lami ifikapo mwakani.
Amefafanua kuwa ujenzi wa barabara
 hiyo utakuwa wa awamu ili kuweza kuharakisha kukamilika kwake ambapo 
awamu ya kwanza itahusisha kipande cha barabara ya Tanga- Pangani (KM 
50) na kuongeza kuwa ujenzi wa barabara hiyo utafungua fursa za kiuchumi
 kati ya Tanga na Pangani.
“Naahidi kujenga barabara hii 
ambayo ni kiungo kati ya Tanga na Pangani, naamini ukamilifu wake 
utalete maendeleo mkoani hapa”. Amesisitiza Prof. Mbarawa.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa 
Wizara hiyo Eng.Joseph Nyamhanga amezipongeza kampuni za Songoro Marine 
na Alpha Logistic kwa kumaliza kwa wakati ujenzi wa kivuko na Gati ya 
bandari hiyo.
Naye Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala
 wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Eng.Manase Ole-kujan amesema kuwa kivuko 
cha Mv.Tanga kimejengwa kwa sh.bilioni nne ambapo kina uwezo wa kubeba 
tani 50 abiria 100 na magari madogo 6 kwa wakati mmoja.
Ujenzi wa Kivuko cha Mv. Tanga ni 
moja ya utekelezaji wa ahadi ya Mhe.Rais Dkt.John Pombe Magufuli 
aliyoitoa wakati wa kampeni ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 wilayani 
Pangani Mkoani Tanga.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni