Jumatatu, 14 Desemba 2015

LUKUVI AKABIDHIWA OFISI RASMI AAPA KUWAKOMBOA MASIKINI


Waziri wa maendeleo ya nyumba na makazi,William Lukuvi amesema atahakikisha wananchi maskini wanapata haki zao za kumiliki ardhi pamoja na kuwawezesha kuwa na makazi bora ya kuishi na kuwashughulikia wale wote wanaotumika kama mawakala na kudhulumu maeneo yao.


MAZOEZI YA VITENDO WAKATI WA KUHITIMISHA MAFUNZO YA AWALI KWA WAHITIMU WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI YALIYOFANYIKA CHUO CHA UONGOZI JKT KIMBIJI

 Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, wakionyesha jinsi ya kuzima moto wakati wa maonyesho ya kufunga mafunzo ya kozi ya awali ya  Sajini na Askari wa Jeshi hilo,yaliyofanyika Chuo cha Uongozi JKT Kimbiji,jijini Dar es Salaam,mwishoni mwa wiki.

Jumamosi, 28 Novemba 2015

TATIZO LA KUOTA NDEVU KWA WANAWAKE

Kawaida watoto wa kiume na wa kike wanapofikisha umri wa kubalehe ma kuelekea utu uzima ,dalili mbalimbali huanza kujitokeza ikiwemo kuota nywele sehemu mbalimbali za mwili kama kwapani na sehemu za siri ,chunusi usoni,sauti kubadilika na kuwa nzito kwa wavulana na nyororo  kwa wasichana.

Ijumaa, 27 Novemba 2015

KAMANDA MPINGA AZINDUA OPARESHENI YA PAZA SAUTI DAR

 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani,DCP  Mohamed Mpinga, akisalimiana na Mabalozi wa Usalama Barabarani, muda mfupi kabla ya kuzindua Operesheni ijulikanayo kwa jina la “Paza Sauti” yenye lengo la kuwaelimisha abiria ili waweze kutoa taarifa mara wanapoona kuna viashiria vya uvunjifu wa sheria za barabarani. Operesheni hii ilizinduliwa jijini Dar es Salaam leo.

MAHAKAMA KUU TANZANIA KUFUNGUA NJIA KWA WAANDISHI WA HABARI



JAJI  kiongozi wa Mahakama kuu ya Tanzania Shaaban Lila amesema kuwa majaji wa Tanzania wanabusara katika kufanya maamuzi yao na ndio maana hata vyombo vya habari nchini hata vinapowachafua hawaangaiki kufikisha kwenye vyombo vya dola.

ALIYEKUWA MGURUGENZI MSAIDIZI WA SHUGHULI ZA BUNGE BI.HELLEN MBEBA AFARIKI

Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah, anasikitika kutangaza kifo cha mtumishi wa Bunge, Bi. Hellen Stephen Mbeba (36), aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi-Shughuli za Bunge, kilichotokea ghafla leo Ijumaa tarehe 27/11/2015 wakati akipelekwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa matibabu..

WAZIRI MKUU MAJALIWA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA BANDARINI,AWAVUA GAMBA BAADHI YA MAAFISA TRA



Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi maofisa watano na watumishi watatu wa mamlaka ya mapato Tanzania(TRA)kutokana na upotevu wa makontena
349 yenye thamani ya zaidi ya sh.bilioni 80.

Alhamisi, 8 Oktoba 2015

MAKAMU MWENYEKITI NCCR-MAGEUZI ASEMA YEYE BADO KIONGOZI




MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi(Bara) Leticiaa Mosore amesema mpaka sasa bado anaendelea kushikilia wadhifa huo kwani kikao kilichoitishwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa James Mbatia hakikuwa na uhalali wa kikatiba.

KATIBU MKUU KIONGOZI BALOZI OMBENI SEFUE AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA TAKWIMU DAR ES SALAAM LEO.


 

 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (kushoto), akihutubia wakati akifungua mkutano wa wadau wa takwimu Dar es Salaam leo asubuhi. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Profesa Adolph Mkenda na Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk.Albina Chuwa. Mkutano huo uliandaliwa na NBS.   

MAADHIMISHO YA SIKU YA MACHO DUNIANI KUFANYIKA LEO.

IMEELEZWA kuwa takribani watu 945,000 wanasumbuliwa na matatizo  ya kuona kwa viwango mbalimbali hapa nchini idadi yao ikiwa ni mara tatu ya watu wasioona kabisa ambao ni takribani watu 315,000.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii idadi ya watoto wenye matatizo ya kuona duniani ni milioni 19 huku wazee wakiongoza kwa asilimia 82 pia nchi zinazoendelea zinaongoza kwa idadi kubwa ya watu wenye matatizo hayo kwa asilimia 90.

Taarifa hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Dkt.Donan Mmbando,Katibu Mkuu wa wizara hiyo,ikiwa nisehemu ya kuadhimisha siku ya afya ya macho duniani yenye kauli mbiu ya "Afya bora ya macho kwa wote"yenye lengo la kuhamasisha wadau kushirikana katika kuimarisha  upatikanaji wa huduma za macho katika ngazi zote za utoaji huduna za afya.

Imebainika  kuwa kuwa asilimia 80 ya matatizo yote ya kutokuona yanayoikabili dunia yanachangiwa na sababu zinazoweza kuzuilika.

"Inakadiriwa kuwa takribani watu milioni 285 duniani wana matatizo ya kuona,kati ya hao wenye upofu ni milioni 39 na 246 wana uoni hafifu,"inaeleza taarifa hiyo.

Aidha kutokana na taarifa hiyo sababu zinazosababisha upofu unaoweza kuzuilika hapa nchini na dunia kwa ujumla ni pamoja na mtoto wa jicho,makovu kwenye kioo cha jicho,trakoma,upofu wa utotoni unaotokana unaookana na upungufu wa vitamini A.

Pia maambukizi ya surua,maambukizi ya kisonono kutoka kwa mam kwenda kwa mtoto,upungufu wa upeo wa macho kuona,matatizo ya retina pamoja na ugonjwa wa kisukari na umri mkubwa.

Hata hivyo Wizara ya Afya na ustawi wa jamii inatoa wito kwa Watanzania kupima afya ya macho angalau mara moja kwa mwaka pamoja na wadu na mashirika ya kiserikali na watu binafsi kuwekeza katika rasilimali katika huduma ya macho kwa maendeleo ya nchi.

Jumatano, 7 Oktoba 2015

MAAFISA 27 WA JESHI LA MAGEREZA KANDA YA KASKAZINI WATUNUKIWA NISHANI‏MAAFISA 27 WA JESHI LA MAGEREZA KANDA YA KASKAZINI WATUNUKIWA NISHANI‏





 CGP, Agustino Nanyaro, Mkuu wa Magereza Tanzania akiongea na waandishi wa habari
 CGP, Agustino Nanyaro, akikagua gwaride maalimu
 Heshima na Utii
 DCP Chiza Ruvugo, Naibu Mkuu wa Magereza Tanzania akivishwa nishani.
Mambo yanaendelea 

DKT.KIKWETE APOKEA HATI YA UTAMBULISHO WA MABALOZI.


Balozi mteule wa Ubelgiji nchini Tanzania Mhe. Paul Cartier akikabidhi hati ya utambulisho  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete mapema leo, Ikulu jijini Dar es Salaam.

TANESCO:MGAWO WA UMEME MWISHO OKTOBA 20.


Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Mhandisi Felchesmi Mramba akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ambapo alieleza  juhudi zinazofanywa na shirika hilo katika kutatua kero ya umeme nchini.


Jumatatu, 28 Septemba 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AONGOZA WANANCHI KUAGA MWILI WA MAREHEMU CELINA KOMBANI, DAR, KUZIKWA KESHO MOROGORO.


 

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Waziri Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma,  marehemu Celina Kombani, wakati wa shughuli za kuaga mwili huo zilizofanyika leo Septemba 28, 2015 kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Marehemu Kombani alifariki Agosti 24 huko nchini India na anatarajia kuzikwa kesho mkoani Morogoro.

Ijumaa, 11 Septemba 2015

UZINDUZI WA MFULULIZO WA VIPINDI VYA MAMA MISITU KUHUSU UZALISHAJI WA MKAA ENDELEVU WAFANYIKA NEW AFRIKA HOTEL LEO JIJINI DAR ES SALAAM

  Viongozi mbalimbali wakiwa meza kuu, kutoka kushoto Mkurugenzi wa Taasisi ya Natural Resource Forum (TNRF), Joseph Olila, Mkurugenzi, Idara ya Misitu na Nyuki wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Gladness Makamba, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa uzinduzi huo, Msaidizi wa Balozi, Ubalozi wa UFINI ambao ni wafadhili wa mama misitu, Simo-Pekka Parviainen na Ofisa Mradi Ubalozi wa Finland, William Nambiza.


Jumanne, 8 Septemba 2015

MAKAMO WA RAISI DKT.BILALI ATOA TUZO KWA WAGANGA WASTAAFU.

DKT.AFUNGUA WA MWAKA WA WAGANGA WAKUU DAR




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi Mkutano wa mwaka wa Waganga Wakuu wa Mikoa, Halmashauri na Wakurugenzi wa Hospitali za Rufaa, ulioanza leo Sept 8, 2015 na Maadhimisho ya Miaka 40 ya Mpango wa Taifa wa Chanjo uliofanyika kwenye Hoteli ya Blue Peal Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam. 
 

TAKWIMU WATANGAZA MFUMUKO WA BEI MWEZI AGOSTI


 Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Iphrahim Kwesigabo (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana kuhusu mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi Agosti, 2015. Kulia ni Kaimu Meneja wa Idara ya Takwimu za Ajira na Bei, Ruth Minja.

Alhamisi, 3 Septemba 2015



mgombea wa ubunge jimbo la Ubungo kupitia tiketi ya chama cha Mapinduzi(CCM) Dkt Didas Masaburi amewataka Wapinzani wasiweweseke katika kutafuta mtu anayewaloga kwa kuwa mchawi anatoka ndani ya chama chao kwa tabia zao za kukumbatia makapi ambazo haziendani na matakwa ya wananchi.

Dkt Masaburi amemesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Waandishi wa habari kwenye ofisi za jimbo hilo zilizopo kata ya Manzese akikanusha kuhusika kuchochea yaliyofanyika juzi na baadhi ya vijana na kudhibitiwa na polisi.

"Haipo kwenye akili yangu na wala haitakuwepo kuwachochea vijana waandamane ingawa maandamano ya amani sioni kosa lake na kama maandamano yanaashiria kuunga mkono jambo na kama maandamano yale hayaendani na kudhuru wananchi na kuharibu mali zao,"alisema Makaburi.

Amesema kuwa anaunga mkono hoja za Dkt Slaa na kama angekuwa Chadema angeandamana kwa kuwa hoja hizo zilikuwa ni za kweli na atamkaribisha Mbowe na kumpongeza pamoja na wote watakaokuwa  tayari kuhamia kwenye chama chao. 

Amesema kuwa aliwapokea vijana waliochoshwa na vitendo viovu vinavyofanywa na viongozi wanaounda Umoja wa UKAWA kwa kuwalazimisha kujiunga na umoja huo na kuwa wao wanataka kukiona chama chao(Chadema). 

Mgombea huyo anaendelea kufafanua kuwa vijana hao walipelekwa na mgombea Udiwani wa Ubungo kupitia Chadema na ndiye aliyewaongoza kufanya maandamano baada ya kukatwa katika kura za maoni na kuomba kujiunga na CCM.

"Huyu mgonbea mara tu baada ya kura za maoni za Chadema alikuja kwangu na kusema yupo tayari kujiunga na kuwa  walimfanyia njama hivyo nimpokee na ataleta wafuasi wengi wa Chadema ili chama kishinde na amejiandaa vyema ambapo baadaye alitoka na kuanza kusema maneno,"alisema Masaburi.

Wakati huohuo wanachama 13 kutoka CUF na Chadema wamehamia rasmi kwenye Chama cha Mapinduzi(CCM).

Naye Halima Said  ambaye ni mgombea wa  Ujumbe viti maalum(Chadema)alisema kuwa ameamua kuhamia (CCM)kutokana na wamekuwa wakipotoshwa na na kuwa kiongozi ambaye pia ni mlezi wa chama hicho hayupo.

Ijumaa, 14 Agosti 2015

JWTZ YAWAPA ONYO KALI WANASIASA






 



 



JESHI la Wananchi Tanzania (JWTZ), limekanusha kuwanyang'anya kadi za kupigia kura maofisa na askari wake kama ilivyodaiwa na mmoja wa viongozi wa chama kimoja cha siasa na kutolewa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii



 



Amezungumza hayo jana Jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na  waandishi  habari Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kanali Ngemela Lubinga alisema madai hayo siyo ya kweli na kuwa jeshi hilo halijafanya hivyo na wala haliwezi kufanya hivyo.



 



“Wanajeshi hawaruhusiwi kuwa wanachama wa chama chochote cha kisiasa na kuwa mwanajeshi haruhusiwi kuwa shabiki wa chama chochote cha kisiasa”alisema Lubinga.



 



Lubinga alisema Jeshi la Wananchi Tanzania linafanya kazi zake kama 'professional state organ duniani na kuwa mwanajeshi anayekiuka huchukuliwa hatua za kinidhamu za kijeshi wala si za kiraia.



Alisema Jeshi la Wananchi Tanzania limesikitishwa na kauli hiyo iliyotolewa na kiongozi



huyo na amewatakaWananchi na viongozi wa kisiasa wafanye kazi zao za kisiasa na zisianzishwe hoja nje ya maeneo hayo ya kisiasa kwani lugha hizo za upotoshaji zinaweza kuleta hofu, ukakasi na wasiwasi kwa Wananchi.



 



Aliongeza kuwa jeshi hilo linaendelea na shughuli zake kama kawaida halipendi litolewe kauli za upotoshaji, kusikoeleweka ufuatwe utaratibu wa kuuliza kupata majibu ya uhakika kwani Wananchi wanaimani na jeshi lao.

 



Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ),


NAPE:WANAOIKIMBIA CCM NI OIL CHAFU

Na Tinah Reuben

KATIBU mwenezi na itikadi wa CCM Nape Nnauye amekanusha habari zilizozagaa katika mitandao ya kijamii kuwa mgombea wao wa uraisi John Pombe Magufuli amehaidi kuwapatia kompyuta mpakato  kila mwalimu pamoja na kila kijiji kupatiwa milioni 50.

Nape amezungumza hayo leo Jijini Dar es salaam alipokuta na Waandishi wa Habari alipokuwa anatoa taarifa hiyo iliyokanusha na kusema kuwa waliotoa taarifa hiyo wanalengo lakuwachafua na kutaka waonekana wameanza kampeni mapema.

Alisema hakuna sehemu ambayo Magufuli aliwahi kuongea kauli hiyo na anawashangaa watu pamoja na mitandao ya kijamii inayoeneza ujumbe huo ambao sio wa kweli hata kidogo.

Aliongeza kuwa wapo watu wasioitakia mema CCM na kwamba wamebaini mbinu hizo chafu na wanazifanyia kazi.



"Watu walianda waraka ule walidai kuona umeandikwa katika ilani ya CCM kitu ambacho sio kweli kwani Ilani imetoka rasmi jana",alisema Nape.

Akitolea ufanunuzi kuhusu kuhama kwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga Hamis Mgeja,Nape alisema kuwa Mgeja alijitoa baada ya mwanaye wa Kike kushindwa katika mchakato wa Viti maalum mkoa wa Shinyanga.

Alisema kuwa baada ya mwanae kushindwa Mgeja alitaka chama kimbebe mwanae kinyume cha misingi ya chama na alipokataliwa alikasirikia na kutangaza uamuzi wake wa kukihama cham.

"Watu walikimbia CCM wamekimbia kwa mabaya yao pia walionzisha vyama upinzani wote misingi yao ni CCM na kama wanaondoka atushangai.....kwanza walioaznisha hivyo vyama hawajafanikiwa na wanaokwenda hawata fanikiwa,"alisema Nape

Aliongeza kuwa kitendo cha wanachama hao kujiondoa CCM nisawa na fundi anayetoa Dizeli chafu ndani ya injini ya Gari na kuwepa safi.

Alisema kuwa anawashangaa wapinzani wanavyopokea dizeli chafu zinazopelekea injini zao kuwa mbovu na zosizofa kabisa.

Aidha alisema kwa kawadia chama kinautaratibu wa kupokea wanachama wapya hivyo ni kitendo cha kushangaza kuona wapinzani wanapokea wanachama walioshindwa katika vyama vyao.

Ijumaa, 8 Mei 2015

ACT-Wazalendo: Tunasubiri Ukawa watukaribishe kwenye umoja


Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mgwhira amesema hawana matatizo na Ukawa na kwamba wanachosubiri hadi sasa ni majibu ya barua yao kuomba kujiunga na muungano huo.
Alitoa kauli hiyo juzi wakati viongozi wa chama walipofanya ziara ya kutembelea Hospitali ya Meru na kugawa vitu mbalimbali kwenye wodi ya wajawazito.
“Hatuna matatizo na Ukawa, tunaunga mkono muungano wowote wa upinzani ulio halali,” alisema kiongozi huyo.
Alisema tangu wawasilishe maombi yao, bado hawajapata mrejesho, hivyo wanaendelea kusubiri.
Akifafanua kuhusu barua hiyo, alisema waliomba mwongozo wa namna ya kujiunga na Ukawa.
Alisema chama chao kimepata mwitikio mkubwa kutoka kwa wananchi katika mikoa mbalimbali na hilo lilithibitika katika awamu ya kwanza ya ziara yao.
Mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam zimesababisha mafuriko makubwa na kulazimisha baadhi ya wananchi kukimbia makazi yao.

Jumanne, 21 Aprili 2015

TMA YALENGA KUKIDHI MAHITAJI KATIKA SEKTA MBALIMBALI NCHINI

 

 

 Wataalamu  mbalimbali kutoka Mamlaka ya hali ya hewa wakiwa katika picha ya pamoja.

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya hali ya hewa Dkt Agnes Kijazi akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa wastaalamu wa hali ya hewa kutoka vitengo mbalimbali.

Baadhi  ya washiriki wakifuatilia kwa kina mkutano huo uliofanyikia katika ukumbi wa Hotel ya Bluepearl jijini Dar es Salaam


MAMLAKA ya ali ya hewa nchini (TMA) imesema ipo katika mkakati wa kubadilisha mfumo wa kuhifadhi takwimu za hali ya hewa kutoka mfumo wa analogia kwenda digitali.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dk.Agnes Kijazi ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akiongea na waandishi wa habari na kufafanua kuwa katika kutimiza hilo walisaini makubaliano ya kushirikiana na ofisi ya hali ya hewa Uingereza ambapo mambo makuu ilikuwa ni kuhakikisha watumiaji wa huduma za hali ya hewa nchini wanaridhika na huduma zitolewazo lengo ikiwa ni kuboresha mfumo wa kuhifadhi takwimu.

“Kwa kipindi cha miaka ya hivi karibuni TMA imekuwa ikikutana na wadau wa Sekta mbalimbali na kupata maoni yao juu ya huduma zitolewazo pamoja na kubadilisha namna ya uhifadhi wa takwimu za hali ya hewa ambapo kwa kupitia maoni hayo tumeona ni wakati muafaka wa kuwakutanisha wataalamu wa hali ya hewa kutoka vitengo mbalimbali ili kujadili na kupata suluhisho la kuboresha huduma zetu,”amesema Kijazi.

Aidha amesema katika mkutano huo ambao umewahusisha pia wakuu wa kanda kutoka TMA na wasimamizi wa vituo vya hali ya hewa vinavyoendeshwa na mamlaka vilivyopo nchini, washiriki watapata fursa ya kujadili na kutolea maamzi maoni ya wadau wa sekta ya kilimo, nishati, maji, afya na habari na pia kujipanga  katika kuwafikia wadau wengine.

Ameongeza kuwa mbali na changamoto za uwepo wa taarifa nyingi za hali ya hewa zilizo kwenye makaratasi ambazo wanataka kuziweka katika mfumo wa kidigitali pia wanakibiliwa na ukosefu wa ofisi maalumu ya kufanyia kazi suala ambalo wanalishighulikia hivi sasa pamoja na upungufu wa wataalamu na vituo vya hali ya hewa ambapo kwa sasa wanavyo vituo 28 wakati malengo yao ni kuwa na vituo 70.

Kijazi amesema kuwa mara kwa mara wamekuwa wakitumia maoni wanayoyapata kutoka kwa wadau mbalimbali hasa wakulima kwa kuangalia mahitaji binafsi kulingana na sekta yao pale wanapotaka kufahamu vipindi vya mvua ili kujiandaa na shughuli za kilimo alikadhalika vipindi vya ukame.

Amesema mbali na wakulima kutaka kupata taarifa za misimu ya mvua pia huhitaji kujua vipindi vya upepo mkali ili kuweka tahadhari kwa ajili ya kulinda mimea kama migomba na matunda kwa kuweka miti ili isianguke ukiachana na taarifa za jumla kwa ajili ya watu mbalimbali ambazo hutolewa na dawati lao.

Jumapili, 19 Aprili 2015

POLISI WAVAMIA VITUO VYA MAFUNZO YA DINI YA KIISLAM DODOMA.


Jeshi la polisi Mkoa wa Dodoma limeweka chini ya ulinzi na kufanyia uchunguzi vituo vitatu vilivyokusanya watoto 115 kutoka mikoa 13 Nchini kwa lengo la kuwapatia mafunzo ya dini ya kiislamu.

 

Vituo hivyo vyote vipo katika eneo la Nkuhungu,lililopo katika manispaa ya Dodoma.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema wanafanya uchunguzi katika vituo hivyo kutokana na kuhusika  kuendesha vituo vya kulelea watoto bila kusajiliwa na hatarishi.

 

"Jana saa saa sita usiku tulifanya upekuzi katika vituo vitatu,katika kituo cha kwanzatukafanikiwa kupata watoto takribani 63,kati yao 46chini ya miaka 18.

 

Katika  kituo cha pili tulikuta watoto 40,kati yaowalio chini ya umri miaka 18 walikuwa 12 na kituo cha tatu tulikuta  watoto saba  ,kati yao walio chini ya umri miaka 18 ni watano".Alisema Misime.

 

Alisema katika idadi watoto hao,63 wana umri chini ya miaka 18 na wengine 52 umri wao ni miaka 25,na wote ni wanaume wengi  wanatoka Wilaya ya Kondoa ambao ni 50 na 26 wanatokea katika \wilaya ya Dodoma mjini,Chamwino na Mpwapwa.

 

"Watoto wanaosalia wanatokea  mikoa ya Kagera,Dar es Salaam,Kilimanjaro,Zanzibar,Tanga,Tabora

Singida,Pwani,Lindi,Mtwara,Geita,Mwanza na Manyara".Alisema Misime.

 

Alisema watoto hao walikutwa usiku wakiwa wamechanganywa bila kujali umri wao,jambo ambalo ni hatarishi.

 

"Uchunguzi unaendelea na yeyote atayeguswa na ushahidi kuwa amekiuka sharia,atafikishwa mahakamani ikiwepo wazai walioruhusu watoto hao kuwa katika uangalizi amao si wa kutosha kama sharia ya motto ya mwaka 2009 inavyoelekeza".Alisisitiza Misime.

 

Akizungumzia tukio hilo,Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mustafa Rajab,alisema hakuna dhambi yeyote kwa watoto hao kulelewa katika kituo hicho.

 

"Hayo ni mafunzo katika madrasa  ambazo zilianza zamani ulimwenguni kote,polisi haina mamlaka ya kufunga madrasa labda kama watakuta kuna tatizo lolote la kuhatarisha amani"Alisema Rajab.

 

Walikizungumza katika eneo hilo,baadhi ya watoto walisema wapo hapo kwa ajili ya kupatiwa mafunzo ya dini ya kiislam

 

" Mimi nimetoka Kondoa lakini nilipokuja hapa nimeandikishwa Shule ya msingi Nkuhunhu,nikimaliza kusoma dini hapa huwa nakwenda shuleni".Alisema mmoja wa watoto hao

 

Mmoja wa majirani Mama Naomi alisema siku zoteamekuwa akiwaona watotro hao wakishinda hapo na hajawahi kuwaona wakienda shule kusoma.

 

"Chakula na kuni za kupikia huwa wan aletewa na walimu wao,wanajipikia wenyewe,watoto wadogo kazi yao ni kuosha vyombo."Alisema Mama Naomi.

.









 

LOWASA AUNGANA NA WANANCHI KATIKA MATEMBEZI YA KUPINGA MAUAJI YA ALBINO

 




 



 Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa ambaye pia ni Munge wa Monduli akiongoza matembezi  matembezi hayo yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.Matembezi hayo yaliyoandaliwa na vijana wa TEMEKE yaliyoanzia katika uwanja wa Taifa na kumalizika katika viwanja vya  TTC Changombe jijini Dar es Salaam



 



Baadhi ya Wananchi waliojitokeza katika kuunga matembezi hayo ya kulaani na kupinga mauaji ya albino. jijini DAR ES salaam.



Mheshimiwa Lowassa akiwa pamoja na baadhi ya Wananchi katika matembezi hayo.



TEMESA KUWEKA NGUVU KATIKA SOKO LA USHINDANI NCHINI


Pichani Katibu Mkuu wa Wizara  ya ujenzi Eng.Mussa Iyombe(katikati)
 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Mussa Iyombe amezungumzia umuhimu wa Wakala wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA) kutangaza huduma wanazozitoa kwa Wananchi ili jamii iweze kunufaika na huduma hizo kwa wakati na  gharama nafuu.

 Akizungumza na Menejimenti ya TEMESA jijini Dar es salaam leo, Eng. Iyombe amesisitiza Wakala huo kuwa na wafanyakazi wenye weledi, waliokabidhiwa mamlaka kamili na wabunifu ili kuhuisha huduma zinazotolewa kwa wananchi na kujiongezea mapato.

“Hakikisheni mnatumia wataalamu mlionao kuleta tija kwa Wakala na kwa Serikali kwa ujumla ili mfikie malengo yenu na kuipunguzia Serikali mzigo wa kuwahudumia”, alisisitiza Eng. Iyombe. SOKO LA USHINDANI

Aidha Eng. Iyombe ameagiza TEMESA kuimarisha uhusiano wake na jamii hasa sekta binafsi ili kubadili mtazamo uliopo sasa kuwa Wakala huo unatengeneza magari ya Serikali peke yake na hivyo kushindwa kuteka soko la sekta binafsi.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA) Eng. Marceline Magesa amemshukuru Katibu Mkuu kwa kuwapatia vifaa mbalimbali na mitambo na kuahidi kuwa vitatumika vizuri ili kuimarisha utendaji kazi wa TEMESA.

“Asilimia 100 ya mapato kwa baadhi ya mikoa tunayaacha mikoani ili kufufua mitambo iliyoko na kuboresha huduma za Ufundi, hivyo tumieni fursa hii kubuni miradi mingi ya kuongeza mapato”, amesema Eng. Magesa.

Ubunifu, kujitangaza na kutoa motisha kwa wafanyakazi inachangia ari ya kufanya kazi ambapo TEMESA mkoa wa Pwani na Tanga imeelezwa kufanya vizuri na hivyo kuhudumia taasisi mbalimbali binafsi na za umma.

Jumatano, 15 Aprili 2015

AJALI ZA BARABARANI ZAZUA GUMZO

Eneo ilipotokea ajali ya basi la Jordan linalofanya safari za Arusha Mwanza iliyotokea leo .
 
Baadhi ya mashuhuda wa ajali ya basi la Jordan  wakifuatilia kwa karibu .

Basi la kampuni ya Air Jordan linalofanya safari zake Mwanza ,Arusha limepata ajali mbaya iliyotokea eneo la Nzega leo amabapo mtu mmoja amefariki na wengine 28 wamejeruhiwa na chanzo cha ajali hiyo inasemekana ni mwendo kasi wa dereva.

MAGAIDI 10 YAKAMATWA MOROGORO


 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linawashikilia watu kumi kwa tuhuma za kukutwa na silaha za moto zaidi ya 30 pamoja na milipuko.

Watu hao walikamatwa leo eneo la msikiti wa Suni  Kidatu ambapo ndipo walipojifungia huku wameshika bendera yenye maneno ya kiarabu yenye tafsiri ya Mungu ni mmoja pamoja na mavazi ya kijeshi.

Hata hivyo  mmoja  ya  watuhumiwa hao (Ahmad Makwendo) alimjeruhi askari kwa kumkata na jambia eneo la shingoni wakati wa purukushani za kuwakamata watu hao ambapo inasadikika walikuwa wakifanya maandalizi ya ugaidi.

                                                                                                                                                                           
jeshi la polisi Mkoani Morogoro akionyesha vifaa vilivyokamatwa kutoka kwa watuhumiwa hao ni mavazi ya jeshi,milipuko na vifaa vya moto.(PICHANI JUU).