Jumapili, 19 Aprili 2015

POLISI WAVAMIA VITUO VYA MAFUNZO YA DINI YA KIISLAM DODOMA.


Jeshi la polisi Mkoa wa Dodoma limeweka chini ya ulinzi na kufanyia uchunguzi vituo vitatu vilivyokusanya watoto 115 kutoka mikoa 13 Nchini kwa lengo la kuwapatia mafunzo ya dini ya kiislamu.

 

Vituo hivyo vyote vipo katika eneo la Nkuhungu,lililopo katika manispaa ya Dodoma.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema wanafanya uchunguzi katika vituo hivyo kutokana na kuhusika  kuendesha vituo vya kulelea watoto bila kusajiliwa na hatarishi.

 

"Jana saa saa sita usiku tulifanya upekuzi katika vituo vitatu,katika kituo cha kwanzatukafanikiwa kupata watoto takribani 63,kati yao 46chini ya miaka 18.

 

Katika  kituo cha pili tulikuta watoto 40,kati yaowalio chini ya umri miaka 18 walikuwa 12 na kituo cha tatu tulikuta  watoto saba  ,kati yao walio chini ya umri miaka 18 ni watano".Alisema Misime.

 

Alisema katika idadi watoto hao,63 wana umri chini ya miaka 18 na wengine 52 umri wao ni miaka 25,na wote ni wanaume wengi  wanatoka Wilaya ya Kondoa ambao ni 50 na 26 wanatokea katika \wilaya ya Dodoma mjini,Chamwino na Mpwapwa.

 

"Watoto wanaosalia wanatokea  mikoa ya Kagera,Dar es Salaam,Kilimanjaro,Zanzibar,Tanga,Tabora

Singida,Pwani,Lindi,Mtwara,Geita,Mwanza na Manyara".Alisema Misime.

 

Alisema watoto hao walikutwa usiku wakiwa wamechanganywa bila kujali umri wao,jambo ambalo ni hatarishi.

 

"Uchunguzi unaendelea na yeyote atayeguswa na ushahidi kuwa amekiuka sharia,atafikishwa mahakamani ikiwepo wazai walioruhusu watoto hao kuwa katika uangalizi amao si wa kutosha kama sharia ya motto ya mwaka 2009 inavyoelekeza".Alisisitiza Misime.

 

Akizungumzia tukio hilo,Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mustafa Rajab,alisema hakuna dhambi yeyote kwa watoto hao kulelewa katika kituo hicho.

 

"Hayo ni mafunzo katika madrasa  ambazo zilianza zamani ulimwenguni kote,polisi haina mamlaka ya kufunga madrasa labda kama watakuta kuna tatizo lolote la kuhatarisha amani"Alisema Rajab.

 

Walikizungumza katika eneo hilo,baadhi ya watoto walisema wapo hapo kwa ajili ya kupatiwa mafunzo ya dini ya kiislam

 

" Mimi nimetoka Kondoa lakini nilipokuja hapa nimeandikishwa Shule ya msingi Nkuhunhu,nikimaliza kusoma dini hapa huwa nakwenda shuleni".Alisema mmoja wa watoto hao

 

Mmoja wa majirani Mama Naomi alisema siku zoteamekuwa akiwaona watotro hao wakishinda hapo na hajawahi kuwaona wakienda shule kusoma.

 

"Chakula na kuni za kupikia huwa wan aletewa na walimu wao,wanajipikia wenyewe,watoto wadogo kazi yao ni kuosha vyombo."Alisema Mama Naomi.

.









 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni