Jumatano, 15 Aprili 2015

MAGAIDI 10 YAKAMATWA MOROGORO


 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linawashikilia watu kumi kwa tuhuma za kukutwa na silaha za moto zaidi ya 30 pamoja na milipuko.

Watu hao walikamatwa leo eneo la msikiti wa Suni  Kidatu ambapo ndipo walipojifungia huku wameshika bendera yenye maneno ya kiarabu yenye tafsiri ya Mungu ni mmoja pamoja na mavazi ya kijeshi.

Hata hivyo  mmoja  ya  watuhumiwa hao (Ahmad Makwendo) alimjeruhi askari kwa kumkata na jambia eneo la shingoni wakati wa purukushani za kuwakamata watu hao ambapo inasadikika walikuwa wakifanya maandalizi ya ugaidi.

                                                                                                                                                                           
jeshi la polisi Mkoani Morogoro akionyesha vifaa vilivyokamatwa kutoka kwa watuhumiwa hao ni mavazi ya jeshi,milipuko na vifaa vya moto.(PICHANI JUU).
 
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni