Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mgwhira amesema hawana 
      matatizo na Ukawa na kwamba wanachosubiri hadi sasa ni majibu ya barua 
      yao kuomba kujiunga na muungano huo.
    
      Alitoa kauli hiyo juzi wakati viongozi wa chama walipofanya ziara ya 
      kutembelea Hospitali ya Meru na kugawa vitu mbalimbali kwenye wodi ya 
      wajawazito.
    
      “Hatuna matatizo na Ukawa, tunaunga mkono muungano wowote wa upinzani 
      ulio halali,” alisema kiongozi huyo.
    
      Alisema tangu wawasilishe maombi yao, bado hawajapata mrejesho, hivyo 
      wanaendelea kusubiri.
    
      Akifafanua kuhusu barua hiyo, alisema waliomba mwongozo wa namna ya 
      kujiunga na Ukawa.
    
      Alisema chama chao kimepata mwitikio mkubwa kutoka kwa wananchi katika 
      mikoa mbalimbali na hilo lilithibitika katika awamu ya kwanza ya ziara 
      yao.
    
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni