Ijumaa, 8 Mei 2015

ACT-Wazalendo: Tunasubiri Ukawa watukaribishe kwenye umoja


Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mgwhira amesema hawana matatizo na Ukawa na kwamba wanachosubiri hadi sasa ni majibu ya barua yao kuomba kujiunga na muungano huo.
Alitoa kauli hiyo juzi wakati viongozi wa chama walipofanya ziara ya kutembelea Hospitali ya Meru na kugawa vitu mbalimbali kwenye wodi ya wajawazito.
“Hatuna matatizo na Ukawa, tunaunga mkono muungano wowote wa upinzani ulio halali,” alisema kiongozi huyo.
Alisema tangu wawasilishe maombi yao, bado hawajapata mrejesho, hivyo wanaendelea kusubiri.
Akifafanua kuhusu barua hiyo, alisema waliomba mwongozo wa namna ya kujiunga na Ukawa.
Alisema chama chao kimepata mwitikio mkubwa kutoka kwa wananchi katika mikoa mbalimbali na hilo lilithibitika katika awamu ya kwanza ya ziara yao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni