Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi
maofisa watano na watumishi watatu wa mamlaka ya mapato Tanzania(TRA)kutokana
na upotevu wa makontena
349 yenye thamani ya zaidi ya sh.bilioni 80.
Akizungumza na viongozi wa mamlaka ya Bandari pamoja na viongozi wa TRA,katika ziara ya kushtukiza leo,Waziri Mkuu amewataka Kamishna Mkuu wa TRA,Rished Bade na Naibu Kamishna Mkuu wa TRA,Lusekelo Mwasena,wahakikishe wanashirikiana na polisi kufuatilia upotevu huo na na kwamba fesha hizo zinapatikana na zinarudi Serikalini.
Akizungumza na viongozi wa mamlaka ya Bandari pamoja na viongozi wa TRA,katika ziara ya kushtukiza leo,Waziri Mkuu amewataka Kamishna Mkuu wa TRA,Rished Bade na Naibu Kamishna Mkuu wa TRA,Lusekelo Mwasena,wahakikishe wanashirikiana na polisi kufuatilia upotevu huo na na kwamba fesha hizo zinapatikana na zinarudi Serikalini.
Akitangaza uamuzi huo baada ya
kufanya kikao na viongozi wa Serikali bandarini hapo,Waziri Mkuu aliwataja
waliosimamishwa kazi kuwa ni Kamishna wa forodha,Tiagi Masamaki na mkuu wa
kituo cha huduma kwa
wateja, Habibu Mponezya.
“IGP,Ninaagiza watu hawa
wakamatwe na kuisaidia polisi,hati zao za kusafiria zikamatwe na mali zao
zikaguliwe kama zinaendana na utumishi wa umma,”alisema Waziri Mkuu.
Watumishi wengine waliosimamishwa kazi ni Mkuu
wa Kitengo cha TEHAMA,Haruni Mpande,Hamisi Ali Omari(hakutaja anatoka kitengo
gani)pamoja na mkuu wa kitengo cha Bandari Kavu (ICD In –Charge),Eliachi Mrema
na alitaka wawe chini ya polisi lpaka uchunguzi utakapokamilika
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu
amemuagiza Katibu mkuu wa hazina,Dkt.Servacius Likwelile,kuhakikisha kuwa
anapeleka wataalamu kutoka mawakala wa serikali Mtandao(e-Gvt)ili kukagua
mifumo ya taarifa na kubaini jinsi ambavyo wizi huo unafanyika.
“Ninataka uchunguzi uanze mara
moja pia tafuteni njia mabazo zinatumika kama mianya ya wizi kutokea hapa
bandarini pamoja na makontena yatafutwe na fedha zirudishwe serikalini.
Akijibu maswali ya Waziri
Mkuu,Kamishna Mkuu wa TRA,Rished Bade alikiri kuwepo kwa upotevu wa makontena
na kwamba walifanya ukaguzi kwenye ICD moja na kukuta makontena 54 yamepotea
kwa njia ya wizi .
“Hata hivyo tulipoendelea na
ukaguzi namba iliongezeka na kufikia 327.tunaendelea kufuatilia kwa
kushirikiana na TAKUKURU hata hivyo mmiliki wa ICD ametakiwa kulipa faini
sh.bilioni 12.6 na mpaka sasa ameshalipa sh.bilioni2.4,”alifafanua Bade.
Lakini alipoulizwa kuwa ana
majina ya watumishi wanaohusika katika wizi huo hakutoa jibu la moja kwa moja
na badala yake alisema anayo na ampe muda wa kuyatafuta ambapo Waziri mkuu
aliyatoa na akamuonyesha orodha ya makontena yaliyopotea moaka namba za magari
ambayo yalitumika kuyabebea hivyo hakuwa na jinsi na kukiri kuwa ni ya kweli.
Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi kutoka TRA na TPA.
Hapa akionyesha orodha ya makontena yaliyopotea wakati alipofanya ziara ya kushtukiza bandarini.
Waziri mkuu Majaliwa Kassim akiagana na baadhi ya viongozi kutoka TRA na TPA mara baada ya mkutano.
kazi nzuri endelea kukaza buti
JibuFuta