Ijumaa, 14 Agosti 2015

NAPE:WANAOIKIMBIA CCM NI OIL CHAFU

Na Tinah Reuben

KATIBU mwenezi na itikadi wa CCM Nape Nnauye amekanusha habari zilizozagaa katika mitandao ya kijamii kuwa mgombea wao wa uraisi John Pombe Magufuli amehaidi kuwapatia kompyuta mpakato  kila mwalimu pamoja na kila kijiji kupatiwa milioni 50.

Nape amezungumza hayo leo Jijini Dar es salaam alipokuta na Waandishi wa Habari alipokuwa anatoa taarifa hiyo iliyokanusha na kusema kuwa waliotoa taarifa hiyo wanalengo lakuwachafua na kutaka waonekana wameanza kampeni mapema.

Alisema hakuna sehemu ambayo Magufuli aliwahi kuongea kauli hiyo na anawashangaa watu pamoja na mitandao ya kijamii inayoeneza ujumbe huo ambao sio wa kweli hata kidogo.

Aliongeza kuwa wapo watu wasioitakia mema CCM na kwamba wamebaini mbinu hizo chafu na wanazifanyia kazi.



"Watu walianda waraka ule walidai kuona umeandikwa katika ilani ya CCM kitu ambacho sio kweli kwani Ilani imetoka rasmi jana",alisema Nape.

Akitolea ufanunuzi kuhusu kuhama kwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga Hamis Mgeja,Nape alisema kuwa Mgeja alijitoa baada ya mwanaye wa Kike kushindwa katika mchakato wa Viti maalum mkoa wa Shinyanga.

Alisema kuwa baada ya mwanae kushindwa Mgeja alitaka chama kimbebe mwanae kinyume cha misingi ya chama na alipokataliwa alikasirikia na kutangaza uamuzi wake wa kukihama cham.

"Watu walikimbia CCM wamekimbia kwa mabaya yao pia walionzisha vyama upinzani wote misingi yao ni CCM na kama wanaondoka atushangai.....kwanza walioaznisha hivyo vyama hawajafanikiwa na wanaokwenda hawata fanikiwa,"alisema Nape

Aliongeza kuwa kitendo cha wanachama hao kujiondoa CCM nisawa na fundi anayetoa Dizeli chafu ndani ya injini ya Gari na kuwepa safi.

Alisema kuwa anawashangaa wapinzani wanavyopokea dizeli chafu zinazopelekea injini zao kuwa mbovu na zosizofa kabisa.

Aidha alisema kwa kawadia chama kinautaratibu wa kupokea wanachama wapya hivyo ni kitendo cha kushangaza kuona wapinzani wanapokea wanachama walioshindwa katika vyama vyao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni