Jumamosi, 28 Novemba 2015

TATIZO LA KUOTA NDEVU KWA WANAWAKE

Kawaida watoto wa kiume na wa kike wanapofikisha umri wa kubalehe ma kuelekea utu uzima ,dalili mbalimbali huanza kujitokeza ikiwemo kuota nywele sehemu mbalimbali za mwili kama kwapani na sehemu za siri ,chunusi usoni,sauti kubadilika na kuwa nzito kwa wavulana na nyororo  kwa wasichana.


Balehe ni jumla ya mabadiliko yote ya kimwili,kimawazo na kihisia yanayowatokea vijana wote wa kiume na wa kike wanapotoka utotoni na kuingia utu uzima .Kwa mfano misuli ya wavulana hujengeka na kifua kupanuka wakati matiti ya wanawake hukua zaidi. Kutokana na asili katika uumbaji pamoja na ambavyo sisi wanadamu tumezoea kuona, ni kwamba ni jambo la kawaida kwa mwanaume kuota ndevu,endapo ndevu zitaonekana zimeota kwa mwanamke basi   watu huanza kujiuliza ni kwa nini na wengine kuwa mitazamo tofauti juu ya mwanamke huyu ambaye ameota ndevu.
Baadhi yao humckulia mwanamke huyu kama ni mchafu na kumuona kuwa ni asiyejipenda na mitazamo mingine ya tofauti ambayo kwa kiasi fulani huwaathiri kisaikolojia na kujiona ni tofauti na wanawake wengine hasa pale anapojikuta akinyooshewa vidole na baadhi ya watu hata kumcheka.
Wasichana wanapoota ndevu nyingi hukabiliwa na changamoto za kisaikolojia na ulimbwende. Mitazamo na mila nyingi za kijamii katika bara la Afrika, bado zinakumbatia unyanyapaa wa wazi au wa kificho kwa wasichana wanaoota ndevu nyingi mfano,wanaume wengi hawapendi kuoa wanawake wa aina hiyo kwa kigezo kuwa hawana muonekano huku wengine wakidhani ni aibu kuwatambulisha mbele ya marafiki zao kama wafanyavyo wapenzi.
 Msichana mwenye ndevu nyingi anavuta hisia na macho ya watu wengi yaani wanaume na wanawake pia kiasi cha  kumtazama kwa namna ya kumshangaa na wengine kumkejeli kwa kumtania na kumtungia majina ya kumdhihaki kama vile “jike dume”hali ambayo inamnyongonyesha na kumnyima raha.
Katika hali ya kawaida msichana anatazamiwa asiwe na nywele nyingi kwenye kidevu, juu ya mdomo wake, kifuani, tumboni na mgongoni. Na hata akiwa nazo basi ziwe malaika zisizokuwa na rangi nyeusi iliyokolea na kuwa ngumu kama za mwanaume.
Mwanamke anapokuwa na nywele nyingi sehemu hizo humaanisha kuwepo kwa hitilafu za kijenetiki au dosari za ulinganifu wa vichocheo vya jinsia mwilini mwake.
Kwa mujibu wa Dkt.Kalegamye Mlondo , tatizo la mwanamke kuwa na nywele nyingi mwilini kitaalamu hujulikana kama “hirsutism”.
Huu ni ugonjwa ambao wanawake wanaota manyoya sehemu ambazo kikawaida wao hua hawaoti manyoya maeneo hayo mfano ndevu kidevuni, manyoya kifuani, usoni na mgongoni.
Pia mtawanyiko wa nywele mwilini huwa kama wa kiume, mbali  na ndevu pia mwanamke huota nywele kifuani, tumboni, mapajani, mgongoni, miguuni na mikononi kwa wingi. Wengine huota nywele nyingi kwenye makalio na kuzunguka sehemu ya njia ya haja kubwa.
Kikawaida wingi wa manyoya mwilini mwa binadamu hutegemea sana vimelea vya ukoo husika, kitaalamu kama genetics make up lakini mwanamke anapokua na manyoya mengi kama ya mwanaume hasa ndevu kuna mambo makuu mawili kwamba anaumwa au ukoo wake uko hivyo japokua waathirika wengi wa shida hii ni wagonjwa.
Lakini pia mwanamke anapobalehe na kuvunja ungo mwili huanza kutengeneza homoni za kiume na za kike kwa wingi ndio maana manyoya huota kwapani na maeneo ya uke hivyo homoni za kiume zikiwa nyingi kitaalamu kama adrogens mwanamke hupata hali hii ya kuota manyoya sehemu ambazo hazihusiki.
Pamoja na hayo lakini pia ugonjwa huu unatokana na vyanzo vingi kama, Matumizi ya dawa na vipodozi vyenye kemikali: hii ndio chanzo kikuu cha wanawake wengi kuota ndevu na manyoya  hasa kwa kundekeza tabia ya kutumia dawa xenye kemikali  bila kupata  maelekezo ya daktari,siku hizi kuna maduka ya urembo yanauza dawa hizi na kuzigeuza dawa za urembo wakati ni hatari  sana kiafya kwa watumiaji. Kuna dawa kitaalamu zinaitwa steroids huingilia mfumo wa kiungo kinachohusika na utengenezaji wa homoni (adrenal gland) hivyo zikitumika kwa muda mrefu huleta manyoya ambayo sio ya kawaida kwa wanawake mfano vidonge vya predinisolone na cream, sonaderm, candiderm,gentaline c, na dawa zingine zenye mchanganyiko huu ambazo ziko nyingi ila zimetofautishwa kwa majina na viwanda.
Polycystic ovary syndrome: huu ni ugonjwa unaotokana na kutokuwa na uwiano sawa wa homoni za mwanamke kitaalamu kama homornal imbalance hivyo mwanamke hupata mzunguko wa damu ambao sio wa kawaida, kua mgumba,  kunenepa na kupata uvimbe kadhaa kwenye ovari za kutengeneza mayai yake.
Uvimbe unaotokana kansa:kansa kwenye kiungo kilichopo juu ya figo(adrenal gland) huongeza wingi wa homoni hizi kwenye mfumo wa binadamu na kuleta ndevu na manyoya magumu ya mwili.
Congenital adrenal hyperplasia: huu ni ugonjwa wa adrenal gland ambao mtu huzaliwa nao na kuanza kutoa homoni nyingi za uzazi na matokeo yake mtu huota ndevu na manyoya mengi mwilini.
Cushing syndrome: hali hii hutokea baada ya mgonjwa kupata matibabu ya dawa zenye homoni ya  cortisol mwilini mwake kwa muda mrefu. Mfano matumizi ya dawa ya prednisolone vidonge  kwa wagonjwa wa allergy na asthma.
Wakati mwingine ugonjwa huu hutokea bila sababu yeyote hasa kwa jamii za kiarabu na kihindi.
Hata hivyo mwanamke anapopata tatizo hili la ndevu dalili mbalimbali huanza kujitokeza ikiwa ni pamoja na kuota chunusi nyingi.
 Kutokupata damu ya hedhi kama kawaida. Wakati mwingine msichana hupata damu pungufu sana, kutoiona kabisa au kupata hedhi yake bila mpangilio maalumu.

 Kusinyaa kwa matiti na mfuko wa mji wa mimba.
Kuwa na sauti nzito  wakati mwingine kisanduku cha sauti (Adam’s apple) hunenepa kama cha wanaume lakini pia kuongezeka kwa ukubwa wa kinembe kuliko kawaida (enlargement of the clitoris).
Unaweza kutumia njia mbalimbali kupambana na tatizo hili  pia ni vizuri zaidi kutafuta chanzo cha ugonjwa ili kuanza matibabu sahihi.Endapo chanzo hakionekani dawa zifuatazo zinaweza kutumika kupunguza tatizo hilo.
malt maca: hivi ni virutubisho vinavyotengenezwa kiasili na husaidia sana kupanga homoni za uzazi katika hali ya kawaida na vimesaidia wengi, hupatikana kwa wasambazaji maalumu.
Spironolactone: hizi  hutumika kuzuia homoni zinazosababisha manyoya izingatiwe kuwa  dawa hizi zinasababisha madhara kwa kiwango kikubwa  kwa mtoto kama ikitokea  ukibeba  mimba hivyo  wakati unaendelea na dozi hiyo hakikisha unatumia uzazi wa mpango.
Eflornithine:hii ni dawa ya maalum ya kupaka ambayo kitaalamu hutumika kwa kupaka maeneo yalioathirika na nywele nyingi kwani huzuia kasi ya kukua lakini hazitoi manyoya yaliyopo.
 Electrolysis: hii inahusisha kuweka sindano ndogo  maalumu kwa kila shimo la unywele na kuharibu chanzo chake ni moja ya matibabu mazuri ila ina maumivu makali sana na dawa za nganzi za kupakwa hutumika kupunguza maumivu hayo.

Pia unaweza kutumia Veet Cream;ambayo inasaidia sana hasa ukipaka mara kwa mara yenyewe hunyoa manyoya yote japokua haimalizi kabisa tatizo la kuota nywele.
Itambulike kuwa kuwa ndevu sio ulemavu wala sio ajabu kinachotakiwa ni usafi kwa msichana mwenye tatizo kama hilo yaani asiziache zikajaa na kurefukakama za mwanaume cha kufanya ni kujitahidi kuzikata au kuzinyoa kila zinapojitokeza.Hapa unaweza kutumia vifaa kama wembe,mkasi au cream maalum za kuondoa.
Achana na imani potofu za watu kuwa ukizinyoa ndevu zinazidi kuota jambo hilo halina ukweli wowote.Hata hivyo ni bora kujiepusha au kuachana kabisa na matumizi ya vipodozi vyenye viambato vya dawa za zinazosababisha madhara kwenye ngozi.
 Ndevu zising’olewe kwa vidole, hii inaweza kusababisha uambukizo wa bakteria katika ngozi kwa urahisi na kuleta matatizo ya kiafya.
Wasichana waepuke matumizi ya dawa zenye steroid bila kupata ushauri wa kitaalamu toka kwa wahudumu wa afya na maswala ya tiba.

  Endapo nywele zimetapakaa kwa wingi miguuni na mikononi na kuleta muonekano wa kiume ni bora kuvaa nguo ndefu zinazofunika mwili vizuri ili kuepuka msongo wa kisaikolojia ambao unaweza kutokea kutokana na mtazamo hasi wa kijamii.
Vilevile jifunze kupambana na hisia usikubali mitazamo ya watu ikakufanya usijiamini kama msichana aliyekamili wakati wote jivunie kuwa msichana.

Mara zote serikali imekua ikipiga marufuku baadhi ya vipodozi na kuvichoma moto lakini watu wanahisi wanaonewa na kuvitafuta kwa magendo,tena wanaishi huku wakiamini vipodozi hivyo huwafanya waonekane warembo zaidi bila kujua madhara wanayoweza kuyapata ni makubwa na gharama kuyatibu.

Maoni 9 :

  1. hii elimu ni nzuri ungeiendeleza ikawa makala ndefu kdogo uelimishe

    JibuFuta
  2. nimeiona ikiwa ni ndefu ni nzuri sana keep it up

    JibuFuta
  3. I real appreciate your advice to lads the other thing to emphasize is on the genetic makerup. Most of the rural women who are not much exposed to diff.cosmetics it has observed that inheritance is the rootcause of their beads and other abnormal hairs on their body.Yet if happen let them keep on removing them as it may destort their minds because of being diff.from their fellow women.
    Thanks

    JibuFuta
  4. Asante sana nimeelewa maana mimi ni muhanga wa tatizo ilo

    JibuFuta
  5. Asante Sanaa kwa Elimu hiyo na Mimi Ni mhanga wa hili janga

    JibuFuta
  6. Asantee Sana maahiyo ndoshida yanguu kubwa

    JibuFuta
  7. Nahitaj sababu ya kutokutoa ndevu kwa wanaume je nini tatizo na lipi lifanyike ilibziote na je kunamadhara yoyote mwanaume asipokuwa na ndevu?

    JibuFuta
  8. Ni nzuri, nilikuwa naomba makala hii iwafikie wahanga wa hili jambo

    JibuFuta
  9. Dawa ya kuzuia ndevu kwa wanawake tafadhar

    JibuFuta