Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam mara alipotembelea Shirika la Reli Nchini (TRL),Sitta alisema serikali ikidhibitika waliokagua na kudhibitisha kuleta mabehewa hayo watachukuliwa hatua.
“Nchi ni masikini hivyo wote waliohusika katika uingizaji wa mabehewa hayo watachukuliwa hatua za kisheria za nchi ikiwa ni pamoja na kusitisha mkataba huo na hili nitalifuatilia kwa karibu na bodi ya TRL nimeiagiza kufanya hivyo”alisema Sitta.
Sitta alisema amezuia mabehewa 124 kutoka kwa watu walioingia mkataba na Kampuni ya TRL kutokana na kuingia kwa mabehewa yasiyokuwa na ubora Nchini.
Waziri
wa Uchukuzi Samwel Sitta akizungumza na wandishi wa Habari leo jijini Dar es
Salaam,kushoto Naibu Katibu Mkuu wa Uchukuzi,Monica Mwamunyange,kulia ni Naibu
Waziri,Charles Tizeba.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni