Jumamosi, 14 Machi 2015

MAKONDA AWAPATA SIKU SABA TMJ

Na Tina Reuben


Mkuu wa Wilaya ya kinondoni Paul Makonda ameitaka Hospitali ya TMJ kushugulikia kwa haraka urekebishaji wa bomba la kupitishia maji machafu yanayotoka katika Hospitali hiyo   kwani inaweza kusababisha madhara  wakati wa mafuriko.

“Hospitali kubwa lakini inajivunjia heshima kwa kuhindwakudhibiti mifereji ya maji machafu na licha ya uchafu kuna kemikali ambazo zinaweza kusababisha magonjwa ya mlipuko kwa Wakazi wanaoishi kwenye maeneo hayo.”

Makonda ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam katika ziara ya Kukagua barabara na mifereji inayosaidia wakati wa mafuriko tunapopata taarifa kutoka kwa Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchni(TMA)

Ametoa siku saba kwa TMJ kushughulikia hilo wakishindwa hatua za kisheria zitafuatwa na amewataka Wananchi kuacha kutupa taka katika eneo la mtaro kwani unasababisha kuziba kwa kalawati linalopeleka maji hayo baharini na wanaochimba na kuchota mchanga katika ukingo wamtaro kuacha mara moja.

“Nawaomba watu  wanaoishi kwenye maeneo ya bondeni wahame wasisubiri mpaka mvua zianze kunyesha na Wananchi wanaoishi jirani na eneo la mtaro kushirikiana kwa pamoja katika kudhbiti utupaji taka kwenye eneo hilo.

Naye Mhandisi Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni Eng.Baraka Mkuya amesema wapo katika mradi wa kujenga barabara ili kupunguza msongamano wa magari kwani eneo la Kinondoni linaongoza kwa foleni  lina muunganiko wa kutoka Bagamoyo na Mkoa wa Morogoro.

Amezitaja barabara ni Chwaku,SerengetiJournalism,Sanya(inayounganisha Mwai Kibaki na Ali Hassan Mwinyi) zote zimekamilika isipokuwaChwaku ambayo imekwama  kuendelea kujengwa kutokana na mifumo maji taka inayoimamiwa na Shirika la Maji safi na Maji taka (DAWASCO).
Mkuya ametaja changamoto inayowakabili ni mgogoro kati ya Manispaa na Shirika la maji Dar es Salaam(DAWASCO)ambayo inataka kulipwa fidia kiasi cha milioni 139 ili kuhamisha mitambo yao waliyoifunga.

Amesema hayo yanawapa wakati mgumu katika utekelezaji wa kazi zao kwani Wananchi wanailalamikia Manispaa kuwa haitekelezi hivyo kuwalazimu kuwalipa  DAWASCO imeshalipa zaidi ya bilioni 1 ambayo ni kinyume ch sheria ya mwaka 2007 inayowataka kuhamisha mitambo kwa gharama zao na kuifunga maeneo watayoelekezwa na Manispaa kwa vibali maalum.

Vilevile ameyataja mashirika mengine ambayo yako kwenye mgogoro huo ni Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO)na Shirika la Mawasiliano(TTCL).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni