ZIARA ya Mbunge wa 
Rufiji,Mohamed Mchengerwa,(CCM) imebaini uuzwaji wa ardhi iliyokuwa 
imetengwa kwa ajili ya kiwanda cha sukari katika kijiji cha Chumbi 
ambayo imeuzwa kwa hekari moja shilingi 10,000.
Baada
 ya Mbunge huyo kufika katika mkutano wa hadhara wa kushukuru wananchi 
na kusikiliza kero zao juzi katika kijiji cha Chumbi alikutana na kilio 
cha eneo lenye ekari 2400 kuuzwa kwa shilingi milioni 24 pekee.
Wananchi
 wa eneo hilo walimtaja Diwani wa Kata ya Chumbi ambaye pia ni 
Mwenyekiti wa Kijiji cha Chumbi C,Salum Mtimbuko (CCM) kuwa ndiye 
aliyeuza eneo hilo kwa muwekezaji ambaye anamjua mwenyewe na alipewa 
Baraka zote na Mkuu wa Wilaya hiyo Juma Njwayo.
Katibu
 wa Itikadi na Uenezi wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani hapo,Mussa 
Mngeresa,ndiye aliyeeleza jambo hilo huku akishangiliwa na wananchi 
akimtaka mbunge huyo kumpeleka Mkuu wa Mkoa huo,Mhandisi Evarist 
Ndikilo,ili atatue kero hiyo kwani Njwayo ameshindwa.
 ‘’Uuzwaji huu ulifanywa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Chumbi C ambaye pia
 ni Diwani wa Kata ya Chumbi ,Salum Mtimbuko (CCM)  na alipata Baraka 
kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Rufiji,Juma Njwayo,ambaye wananchi 
walimueleza suala hilo kabla lakini hakulifanyia kazi na kuwataka waache
 majungu’’alisema
Alisema
 viongozi hao wamewaudhi wananchi kwa kuuza ardhi kwa muwekezaji ambaye 
wanamjua wenyewe na kwamba ukifanyika uchaguzi wakati wowote kabla 
masuala hayo hayajataftiwa ufumbuzi CCM itapoteza nafasi hivyo kumuomba 
Mbunge huyo kufanya jitihada za kuwaleta viongozi wa mkoa,Wizara ya 
Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Akizungumzia
 suala hilo Mchengerwa alilaani kitendo cha viongozi hao kutaka 
kukwamisha maendeleo ya viwanda jimboni hapo kwani alishazungumza na 
Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage,kuhusu ujenzi wa
 kiwanda cha sukari katika eneo hilo ambalo kwa sasa wananchi wamesema 
halipo.
‘’Jamani
 huku ni kurudishana nyuma na kutotambua juhudi za serikali na 
tunaowatetea haiwezekani viongozi wahusike kuuza ardhi ya 
kiwanda,wananchi tusikubali,sheria inaruhusu kuongea upya  na muwekezaji
 huyo ili atuachie ardhi yetu au aongeze fedha tukatafute eneo 
linguine,kuuza shilingi 10,000 ekari moja ni aibu’’
Akijibu
 tuhuma hizo diwani huyo alisema’’Nyie mnanionea wivu,wengine 
nimewasadia sana kuwalisha na familia zenu alafu mnanisema hapa,au 
kwasababu mnaniona naishi vizuri na wake zangu wawili na nina nyumba na 
magari? Pumbavu’’
Hata
 hivyo majibu ya diwani hiyo yalizua tafrani kwa wananchi kumzoea na 
kumtaka Mchengerwa arudi kwa mara nyingine na Mkuu wa Mkoa wa 
Pwani,Mhandisi Evarist Ndikilo,Ili aweze kutatua kero zilizopo kwani 
viongozi wanauza maeneo kiholela na wanaposhitaki wa Mkuu wa Wilaya 
anakuwa upande wa wauzaji ardhi.
Mchengerwa
 aliwaleza wananchi hao kwamba ameshawasiliana na Mhandisi Ndikilo 
,kuahidi kufanya ziara katika maeneo hayo Desemba 5 mwaka huu .
 
 

 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni