Miaka 55 ya Uhuru Jimbo la Igalula linajivunia Mafanikio Makubwa
Na.  Immaculate Makilika – MAELEZO
WANANCHI
 wa Jimbo la Igulula wilayani Uyui Mkoani Tabora wamepongeza hatua na 
jitihada zilizofikiwa na Serikali katika kuboresha miundombinu ya huduma
 za maendeleo ya jamii katika kipindi cha miaka 55 ya uhuru wa Tanzania 
Bara.
Wanazitaja
 huduma hizo ni pamoja na maji, afya, nishati, na elimu ambazo kwa 
kipindi kirefu zilikuwa zikikwamisha maendeleo ya wananchi, na 
kukamilika kwake kunahitimisha ndoto za siku nyingi za kupatikana kwa  huduma muhimu  jimboni  humo.
Wakitolea mfano wanasema mwaka 2015 jimbo hilo  limepata  nishati
 ya umeme kupitia gridi ya Taifa kwa asilimia 70 na hivyo kufanya kata 
za Goeko, Ngololo, Kigwa na Igalula kupata nishati hiyo adhimu sambamba 
na  kufikisha umeme wa mwanga wa jua katika kata za Tara, Loya, na Lutende.
Mbunge
 wa jimbo la Igalula Athumani Mfutakamba akizungumza na mwandishi wa 
habari hii, anaeleza kinagaubaga neema zilizopatikana ndani ya miaka 55 
ya Uhuru katika jimbo hilo na kukiri wazi zinamfanya awe na shauku ya 
kuhadithia kila mara.
Dkt.
 Mfutakamba anasema jitihada hizo za Serikali pamoja na wadau wengine za
 kufikisha umeme katika jimbo la Igalula imekua nyenzo muhimu  kwa uchumi na ustawi wa maendeleo ya jimbo hilo.
“Umeme huu umekua ukitumika si tu kuwashia taa ama kumulika majumbani na mitaani ila hutumika pia  hospitalini, shuleni na katika shughuli mbalimbali zinazotumia nishati hiyo” anasema Dkt Mfutakamba.
Kwa
 mujibu wa Dkt. Mfutakamba anasema jimbo hilo limepata mafanikio makubwa
 katika sekta ya maji kwa kujenga visima virefu viwili vilivyoweza 
kutatua matatizo ya maji katika jimbo hilo.
Dkt.
 Mfutakamaba alisema jimbo hilo pia limefanikiwa kukamilisha ujenzi wa 
zahanati za Imalaseko, Goeko, Ngololo, Igalula na Loya pamoja na kupata 
vitanda ambavyo vinatumika kusaidia wanawake wanaojifungua.
Kuhusu
 sekta ya elimu, Mbunge Mfutakamba alisema kwa miaka mingi jimbo hilo 
halikuwa na shule ya sekondari, ambapo hadi sasa jimbo limeweza kuwa na 
shule ya sekondari Goeko.
Sambamba
 na hayo, Mbunge huyo aliipongeza juhudi zinazoendelea kufanywa na 
Serikali ya Awamu ya Tano ikiwemo za kusimamia kikamilifu rasilimali 
fedha na watu.
“Ni
 lazima tuunge mkono jitihada hizo kwa kulipa kodi ili fedha 
zitakazopatikana zisaidie katika shughuli mbalimbali za kutuletea 
maendeleo, badala ya kutegemea wafadhili pekee” alisema Mbunge huyo
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni